< Exode 23 >
1 Tu ne feras pas courir de faux bruits. Tu ne donneras pas la main au méchant, pour être un témoin inique.
“Usieneze habari za uongo. Usimsaidie mtu mwovu kwa kuwa shahidi mwenye nia ya kudhuru wengine.
2 Tu n’iras pas après la foule, pour mal faire; et tu ne répondras pas dans un procès en penchant du côté de la foule, pour faire fléchir [le jugement].
“Usifuate umati wa watu katika kutenda mabaya. Unapotoa ushahidi kwenye mashtaka, usipotoshe haki ukijumuika na umati wa watu,
3 Et tu ne favoriseras pas le pauvre dans son procès.
nawe usimpendelee mtu maskini katika mashtaka yake.
4 Si tu rencontres le bœuf de ton ennemi, ou son âne, égaré, tu ne manqueras pas de le lui ramener.
“Kama ukikutana na maksai au punda wa adui yako anapotea, hakikisha umemrudisha kwake.
5 Si tu vois l’âne de celui qui te hait couché sous son fardeau, tu te garderas de l’abandonner; tu ne manqueras pas de le délier avec lui.
Ukiona punda wa mtu anayekuchukia ameanguka na mzigo wake, usimwache hapo alipoangukia; hakikisha kuwa umemsaidia.
6 Tu ne feras pas fléchir le jugement de ton indigent dans son procès.
“Usiwanyime haki watu wako walio maskini katika mashtaka yao.
7 Tu t’éloigneras de la parole de mensonge, et tu ne tueras pas l’innocent et le juste; car je ne justifierai pas le méchant.
Ujiepushe na mashtaka ya uongo, wala usimuue mtu asiye na hatia au mtu mwaminifu, kwa maana sitamhesabia hana hatia yeye aliye na hatia.
8 Et tu ne recevras pas de présent; car le présent aveugle ceux qui voient clair, et pervertit les paroles des justes.
“Usipokee rushwa, kwa kuwa rushwa hupofusha wale waonao, na kupinda maneno ya wenye haki.
9 Tu n’opprimeras pas l’étranger; car vous savez ce qu’est le cœur d’un étranger, car vous avez été étrangers dans le pays d’Égypte.
“Usimwonee mgeni; ninyi wenyewe mnajua jinsi mgeni anavyojisikia, kwa sababu mlikuwa wageni Misri.
10 Pendant six années tu sèmeras ta terre, et tu en recueilleras le rapport;
“Kwa muda wa miaka sita mtapanda mashamba yenu na kuvuna mazao,
11 et la septième, tu la laisseras en jachère, et tu la laisseras inculte, et les indigents de ton peuple en mangeront, et ce qu’ils laisseront de reste, les bêtes des champs le mangeront. Tu en feras de même pour ta vigne et pour ton olivier.
lakini katika mwaka wa saba usiilime ardhi wala kuitumia, ili watu walio maskini miongoni mwenu waweze kupata chakula kutoka kwenye hayo mashamba, nao wanyama pori wapate chakula kwa yale mabaki watakayobakiza. Utafanya hivyo katika shamba lako la mizabibu na la mizeituni.
12 – Six jours tu feras ton ouvrage, et le septième jour tu te reposeras, afin que ton bœuf et ton âne aient du repos, et que le fils de ta servante et l’étranger respirent.
“Kwa siku sita fanya kazi zako, lakini siku ya saba usifanye kazi, ili maksai wako na punda wako wapate kupumzika, naye mtumwa aliyezaliwa nyumbani mwako, pamoja na mgeni, wapate kustarehe.
13 Vous prendrez garde à tout ce que je vous ai dit; et vous ne mentionnerez pas le nom d’autres dieux; on ne l’entendra point de ta bouche.
“Uzingatie kutenda kila kitu nilichokuambia. Usiombe kwa majina ya miungu mingine, wala usiyaruhusu kusikika kinywani mwako.
14 Trois fois l’an tu me célébreras une fête.
“Mara tatu kwa mwaka utanifanyia sikukuu.
15 – Tu garderas la fête des pains sans levain; pendant sept jours, au temps fixé du mois d’Abib, tu mangeras des pains sans levain, comme je t’ai commandé, car en ce [mois] tu es sorti d’Égypte; et on ne paraîtra pas à vide devant ma face;
“Utaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu; kwa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu kama nilivyokuagiza. Fanya jambo hili kwa wakati uliopangwa katika mwezi wa Abibu, ndio mwezi wa nne, kwa sababu katika mwezi huo ulitoka Misri. “Mtu yeyote asije mbele yangu mikono mitupu.
16 – et la fête de la moisson des premiers fruits de tes travaux, de ce que tu auras semé dans le champ; – et la fête de la récolte, à la fin de l’année, quand tu recueilleras du champ [les fruits de] tes travaux.
“Utaadhimisha Sikukuu ya Mavuno kwa malimbuko ya mazao yako uliyopanda katika shamba lako. “Utaadhimisha Sikukuu ya Kukusanya mavuno mwishoni mwa mwaka, unapokusanya mavuno yako toka shambani.
17 – Trois fois l’an tous tes mâles paraîtront devant la face du Seigneur, l’Éternel.
“Mara tatu kwa mwaka wanaume wote watakuja mbele za Bwana Mwenyezi.
18 Tu n’offriras point le sang de mon sacrifice avec du pain levé; et la graisse de ma fête ne passera pas la nuit jusqu’au matin.
“Msitoe damu ya dhabihu kwangu pamoja na kitu chochote kilicho na chachu. “Mafuta ya mnyama wa sadaka ya sikukuu yangu yasibakizwe mpaka asubuhi.
19 Tu apporteras à la maison de l’Éternel, ton Dieu, les prémices des premiers fruits de ta terre. – Tu ne cuiras pas le chevreau dans le lait de sa mère.
“Utaleta malimbuko bora ya ardhi yako katika nyumba ya Bwana Mungu wako. “Usimchemshe mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.
20 Voici, j’envoie un ange devant toi, pour te garder dans le chemin, et pour t’amener au lieu que j’ai préparé.
“Tazama, ninamtuma malaika akutangulie mbele yako akulinde njiani na kukuleta mpaka mahali nilipoandaa.
21 Prends garde à toi à cause de sa présence, et écoute sa voix; ne l’irrite pas; car il ne pardonnera point votre transgression, car mon nom est en lui.
Mtamtii na kusikiliza kile anachokisema. Usiasi dhidi yake; hatakusamehe uasi wako, kwa maana Jina langu limo ndani yake.
22 Mais si tu écoutes attentivement sa voix, et si tu fais tout ce que je dirai, je serai l’ennemi de tes ennemis et l’adversaire de tes adversaires.
Kama ukitii kweli kweli kile asemacho na kufanya yote nisemayo, nitakuwa adui wa adui zako, na nitawapinga wale wakupingao.
23 Car mon Ange ira devant toi, et t’amènera vers l’Amoréen, et le Héthien, et le Phérézien, et le Cananéen, le Hévien, et le Jébusien, et je les exterminerai.
Malaika wangu atatangulia mbele yako na kukuleta katika nchi ya Waamori, Wahiti, Waperizi, Wakanaani, Wahivi na Wayebusi, nami nitawafutilia mbali.
24 Tu ne te prosterneras point devant leurs dieux, et tu ne les serviras point, et tu ne feras pas selon leurs œuvres; mais tu les détruiras absolument, et tu briseras entièrement leurs stèles.
Usiisujudie miungu yao, au kuiabudu, wala kufuata desturi yao. Utayabomoa kabisa na kuvunjavunja mawe yao ya ibada vipande vipande.
25 Vous servirez l’Éternel, votre Dieu, et il bénira ton pain et tes eaux, et j’ôterai la maladie du milieu de toi.
Utamwabudu Bwana Mungu wako, na baraka zake zitakuwa juu ya vyakula vyako na maji yako. Nami nitaondoa maradhi miongoni mwako,
26 Il n’y aura pas de femelle qui avorte, ou qui soit stérile dans ton pays; j’accomplirai le nombre de tes jours.
na hakuna atakayeharibu mimba wala atakayekuwa tasa katika nchi yako. Nami nitakupa maisha makamilifu.
27 J’enverrai ma frayeur devant toi, et je mettrai en déroute tout peuple contre lequel tu iras, et je ferai que tous tes ennemis tourneront le dos devant toi.
“Nitapeleka utisho wangu mbele yako na kufadhaisha kila taifa utakalolifikia. Nitafanya adui zako wote wakupe kisogo na kukimbia.
28 Et j’enverrai des frelons devant toi, et ils chasseront le Hévien, le Cananéen et le Héthien de devant toi.
Nitatanguliza manyigu mbele yako kuwafukuza Wahivi, Wakanaani na Wahiti waondoke njiani mwako.
29 Je ne les chasserai pas devant toi en une année, de peur que le pays ne devienne un désert et que les bêtes des champs ne se multiplient contre toi;
Lakini sitawafukuza kwa mara moja, kwa sababu nchi itabaki ukiwa na wanyama pori watakuwa wengi mno kwako.
30 je les chasserai peu à peu devant toi, jusqu’à ce que tu croisses en nombre, et que tu hérites le pays.
Nitawafukuza kidogo kidogo mbele yako, mpaka uwe umeongezeka kiasi cha kutosha kuimiliki nchi.
31 Et j’ai établi tes limites depuis la mer Rouge jusqu’à la mer des Philistins, et depuis le désert jusqu’au fleuve; car je livrerai entre tes mains les habitants du pays, et tu les chasseras de devant toi.
“Nitaweka mipaka ya nchi yako kuanzia Bahari ya Shamu hadi Bahari ya Wafilisti, na kuanzia jangwani hadi Mto Frati. Nitawatia watu wanaoishi katika nchi hizo mikononi mwako, nawe utawafukuza watoke mbele yako.
32 Tu ne traiteras point alliance avec eux, ni avec leurs dieux.
Usifanye agano lolote nao wala na miungu yao.
33 Ils n’habiteront pas dans ton pays, de peur qu’ils ne te fassent pécher contre moi, car tu servirais leurs dieux; certainement ce serait un piège pour toi.
Usiwaache waishi katika nchi yako, la sivyo watakusababisha utende dhambi dhidi yangu, kwa sababu ibada ya miungu yao hakika itakuwa mtego kwako.”