< Ecclésiaste 10 >

1 Les mouches mortes font sentir mauvais, elles font fermenter l’huile du parfumeur; [ainsi fait] un peu de folie, [à l’égard de] celui qui est estimé pour sa sagesse et sa gloire.
Kama vile nzi waliokufa huacha harufu mbaya kwenye manukato, ndivyo upumbavu kidogo huzidi nguvu hekima na heshima.
2 Le cœur du sage est à sa droite, et le cœur du sot, à sa gauche;
Moyo wa mwenye hekima huelekea kuume, lakini moyo wa mpumbavu huelekea kushoto.
3 et même, quand l’insensé marche dans le chemin, le sens lui manque, et il dit à chacun qu’il est un insensé.
Hata anapotembea barabarani, mpumbavu hukosa ufahamu na kudhihirisha kwa kila mmoja jinsi alivyo mpumbavu.
4 Si l’esprit du gouverneur s’élève contre toi, ne quitte pas ta place; car la douceur apaise de grands péchés.
Kama hasira ya mtawala ikiwaka dhidi yako, usiache mahali pako, utulivu huweza kuzuia makosa mengi.
5 Il est un mal que j’ai vu sous le soleil, comme une erreur provenant du gouverneur:
Kuna ubaya niliouona chini ya jua, aina ya kosa litokalo kwa mtawala:
6 le manque de sens est placé dans de hautes dignités, et les riches sont assis dans une position basse.
Wapumbavu kuwekwa kwenye nafasi nyingi za juu, wakati matajiri hushika nafasi za chini.
7 J’ai vu des serviteurs sur des chevaux, et des princes marchant sur la terre comme des serviteurs.
Mimi nimeona watumwa wamepanda farasi, wakati wakuu wakitembea kwa miguu kama watumwa.
8 Qui creuse une fosse y tombe; et qui renverse une clôture, un serpent le mord.
Yeye achimbaye shimo aweza kutumbukia ndani yake, yeyote abomoaye ukuta anaweza kuumwa na nyoka.
9 Qui remue des pierres en sera meurtri; qui fend du bois se met en danger.
Yeyote apasuaye mawe inawezekana yakamuumiza, yeyote apasuaye magogo inawezekana yakamuumiza.
10 Si le fer est émoussé, et que [celui qui l’emploie] n’en aiguise pas le tranchant, il aura des efforts à faire; mais la sagesse est profitable pour amener le succès.
Kama shoka ni butu na halikunolewa, nguvu nyingi zinahitajika, lakini ustadi utaleta mafanikio.
11 Si le serpent mord parce qu’il n’y a pas de charme, celui qui a une langue ne vaut pas mieux.
Kama nyoka akiuma kabla ya kufanyiwa uaguzi, mwaguzi hatahitajika tena.
12 Les paroles de la bouche du sage sont pleines de grâce, mais les lèvres d’un sot l’engloutissent.
Maneno yatokayo kinywani mwa mtu mwenye hekima yana neema, bali mpumbavu huangamizwa na midomo yake mwenyewe.
13 Le commencement des paroles de sa bouche est folie, et la fin de son discours est un mauvais égarement.
Mwanzoni maneno yake ni upumbavu, mwishoni ni wazimu mbaya,
14 Et l’insensé multiplie les paroles: l’homme ne sait pas ce qui arrivera; et ce qui sera après lui, qui le lui déclarera?
naye mpumbavu huzidisha maneno. Hakuna yeyote ajuaye linalokuja, ni nani awezaye kueleza ni jambo gani litakalotokea baada yake?
15 Le travail des sots les lasse, parce qu’ils ne savent pas aller à la ville.
Kazi ya mpumbavu humchosha mwenyewe, hajui njia iendayo mjini.
16 Malheur à toi, terre qui as pour roi un jeune garçon, et dont les princes mangent dès le matin!
Ole wako, ee nchi ambayo mfalme wako alikuwa mtumwa na ambayo wakuu wako hufanya karamu asubuhi.
17 Bienheureuse toi, terre qui as pour roi le fils des nobles, et dont les princes mangent au temps convenable, pour [réparer] leurs forces, et non pour le [plaisir de] boire!
Heri wewe, ee nchi ambayo mfalme wako ni wa uzao wenye kuheshimika na ambayo wakuu wako hula chakula kwa wakati unaofaa: ili kupata nguvu na si kwa ajili ya ulevi.
18 À cause de la paresse, la charpente s’affaisse; et à cause des mains lâches, la maison a des gouttières.
Kama mtu ni mvivu paa la nyumba huinama, kutokana na mikono milegevu, nyumba huvuja.
19 On fait un repas pour s’égayer, et le vin rend la vie joyeuse; mais l’argent répond à tout.
Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko, nao mvinyo hufurahisha maisha, lakini fedha ni jawabu la mambo yote.
20 Ne maudis pas le roi, même dans ta pensée, et ne maudis pas le riche dans la chambre où tu couches, car l’oiseau des cieux en emporterait la voix, et ce qui a des ailes en divulguerait les paroles.
Usimshutumu mfalme hata ikiwa ni katika mawazo yako, au kumlaani tajiri katika chumba chako cha kulala, kwa sababu ndege wa angani wanaweza kuchukua maneno yako, naye ndege anayeruka anaweza kutoa taarifa ya yale uliyosema.

< Ecclésiaste 10 >