< Deutéronome 23 >

1 Celui qui est eunuque, soit pour avoir été froissé, soit pour avoir été taillé, n’entrera point dans la congrégation de l’Éternel.
Mwanamume aliyejeruhiwa kwa kupondwa au kukatwa haruhusiwi kuingia katika kusanyiko la Yahwe.
2 L’enfant illégitime n’entrera pas dans la congrégation de l’Éternel; même sa dixième génération n’entrera pas dans la congrégation de l’Éternel.
Mwana haramu haruhusiwi kuwa miongoni mwa kusanyiko la Yahwe; kutoka hadi kizazi cha kumi cha uzao wake, hakuna kati yao anatakiwa kuwa kwenye kusanyiko la Yahwe.
3 L’Ammonite et le Moabite n’entreront pas dans la congrégation de l’Éternel; même leur dixième génération n’entrera pas dans la congrégation de l’Éternel, à jamais;
Muamori au Mmoabu haruhusiwi kuwa miongoni mwa kusanyiko la Yahwe; kutoka hadi kizazi cha kumi cha uzao wake, hakuna kati yao anatakiwa kuwa kwenye kusanyiko la Yahwe.
4 parce qu’ils ne sont pas venus à votre rencontre avec du pain et de l’eau dans le chemin, lorsque vous sortiez d’Égypte, et parce qu’ils ont loué [à prix d’argent] contre toi, Balaam, fils de Béor, de Pethor, en Mésopotamie, pour te maudire.
Hii ni kwa sababu hawakukutana nanyi kwa mkate na maji barabarani mlipokuwa mmetoka nje ya Misri, na kwa sababu walimkodisha Balaamu mwana wa Beoro kutoka Pethoro kule Aramu Naharaimu, awalaani.
5 Mais l’Éternel, ton Dieu, ne voulut pas écouter Balaam; et l’Éternel, ton Dieu, a changé pour toi la malédiction en bénédiction, car l’Éternel, ton Dieu, t’a aimé.
Lakini Yahwe Mungu wako hakumsikiliza Balaamu; badala yake, Yahwe Mungu wako aligeuza laana kuwa baraka kwenu, kwa sababu Yahwe Mungu wako aliwapenda.
6 Tu ne chercheras jamais leur paix, ni leur prospérité, tous tes jours.
Hamtakiwi kutafuta amani au mafanikio yao, katika siku zenu zote.
7 – Tu n’auras pas en abomination l’Édomite, car il est ton frère; tu n’auras pas en abomination l’Égyptien, car tu as séjourné comme étranger dans son pays.
Hutakiwi kumchukia Muedomi, kwa maana ni kaka yako; hutakiwi kumchukia Mmisri, kwa maana ulikuwa mgeni katika nchi yake.
8 Les fils qui leur naîtront, à la troisième génération, entreront dans la congrégation de l’Éternel.
Wazawa wa kizazi cha tatu wanaozaliwa kwao wanaweza kuwa katika kusanyiko la Yahwe.
9 Lorsque le camp sortira contre tes ennemis, garde-toi de toute chose mauvaise.
Utakapotembea kijeshi dhidi ya maadui zako, basi unapaswa kujitenga na kila aina ya uovu.
10 S’il y a parmi toi un homme qui ne soit pas pur, pour quelque accident de nuit, il sortira hors du camp; il n’entrera pas dans l’intérieur du camp;
Iwapo miongoni mwenu kuna mwanamume ambaye sio msafi kwa sababu ya jambo lililofanyika kwake usiku, basi anatakiwa atoke nje ya kambi ya jeshi; hatakiwi kurudi kambini.
11 et sur le soir il se lavera dans l’eau; et au coucher du soleil il entrera dans l’intérieur du camp.
Jioni ikifika, anatakiwa ajiogeshe kwa maji; na jua likizama atarudi ndani kambini.
12 Et tu auras un endroit hors du camp, et tu sortiras là dehors;
Pia unatakiwa kuwa na eneo nje ya kambi ambayo utakwenda;
13 et tu auras, outre tes armes, un pieu; et il arrivera, quand tu t’assiéras dehors, que tu creuseras avec ce [pieu], et tu te retourneras, et tu couvriras ce qui est sorti de toi.
na utakuwa na kitu katika zana zako cha kuchimbia; utakapochuchumaa kujisaidia, unapaswa kuchimbia nacho na kisha kurudishia udongo na kufunika kile kilichotoka kwako.
14 Car l’Éternel, ton Dieu, marche au milieu de ton camp pour te délivrer et pour livrer tes ennemis devant toi; et ton camp sera saint, afin qu’il ne voie parmi toi rien de malséant, et qu’il ne se détourne d’avec toi.
Kwa maana Yahwe Mungu wako anatembea miongoni mwa kambi yenu kuwapa ushindi na kuwapa maadui zenu mkononi mwenu. Kwa hiyo kambi yenu lazima iwe takatifu, ili kwamba asione kitu chochote kichafu miongoni mwenu na kuwaacha.
15 Tu ne livreras point à son maître le serviteur qui se sera sauvé chez toi d’auprès de son maître;
Hutakiwi kumrudishia bwana mtumwa aliyetoroka kwake.
16 il habitera avec toi, au milieu de toi, dans le lieu qu’il choisira en l’une de tes portes, là où bon lui semble: tu ne l’opprimeras pas.
Mruhusu aishi pamoja nawe, katika mji wowote atakaochagua. Usimuonee.
17 Il n’y aura, d’entre les filles d’Israël, aucune femme vouée à la prostitution, et il n’y aura, d’entre les fils d’Israël, aucun homme voué à la prostitution.
Hapatakiwi kuwa na kahaba wa kidhehebu miongoni mwa mabinti wa Israeli, na wala hapatakiwi kuwa na kahaba wa kidhehebu miongoni mwa wana wa kiume wa Israeli.
18 Tu n’apporteras point dans la maison de l’Éternel, ton Dieu, pour aucun vœu, le salaire d’une prostituée, ni le prix d’un chien; car ils sont tous les deux en abomination à l’Éternel, ton Dieu.
Hautakiwi kuleta mshahara wa kahaba au mshahara wa mbwa katika nyumba ya Yahwe Mungu wako kwa kiapo chochote; kwa maana vyote hivi na machukizo mbele ya Yahwe Mungu wako.
19 Tu ne prendras pas d’intérêt de ton frère, intérêt d’argent, intérêt de vivres, intérêt de quelque chose que ce soit qu’on prête à intérêt.
Hutakiwi kumkopesha Muisraeli mwenzako kwa riba – riba ya fedha, riba ya chakula, au riba ya kitu chochote kinachokopeshwa kwa riba.
20 Tu prendras un intérêt de l’étranger, mais de ton frère tu ne prendras pas d’intérêt; afin que l’Éternel, ton Dieu, te bénisse en tout ce à quoi tu mets la main, dans le pays où tu entres pour le posséder.
Kwa mgeni unaweza kukopesha kwa riba; lakini kwa Muisraeli mwenzako haupaswi kukopesha kwa riba, ili kwamba Yahwe Mungu wako aweze kukubariki katika kila jambo uwekalo mkono wako, katika nchi ambayo mnaenda kumiliki.
21 Quand tu voueras un vœu à l’Éternel, ton Dieu, tu ne tarderas pas à l’acquitter; car l’Éternel, ton Dieu, le redemandera certainement de ta part, et il y aura du péché sur toi;
Unapofanya kiapo kwa Yahwe Mungu wako, haupaswi kukawia kuikamilsha, kwa maana Yahwe Mungu wako hakika atadai kiapo hicho; itakuwa dhambi kako usipokamilisha.
22 mais si tu t’abstiens de faire un vœu, il n’y aura pas du péché sur toi.
Lakini iwapo utajizuia kutoa kiapo, haitakuwa dhambi kwako.
23 Ce qui sera sorti de tes lèvres, l’offrande volontaire que tu auras promise de ta bouche, tu prendras garde à le faire, comme tu auras voué à l’Éternel, ton Dieu.
Kile ambacho kimetoka kinywani mwako unapaswa kukifuata na kukitekeleza; kulingana na kiapo ulichotamka kwa Yahwe Mungu wako, chochote ulichotamka kwa hiari kwa kinywa chako.
24 Si tu entres dans la vigne de ton prochain, tu pourras manger des raisins selon ton appétit et te rassasier; mais tu n’en mettras pas dans ta corbeille.
Utakapokwenda katika shamba la mizabibu la jirani yako, unatakiwa kula mizabibu idadi yoyote unayotaka, lakini hautakiwi kuhifadhi yoyote katika kikapu chako.
25 Si tu entres dans les blés de ton prochain, tu pourras arracher des épis avec ta main; mais tu ne lèveras pas la faucille sur les blés de ton prochain.
Utakapokwenda katika shamba la zao lililoiva la jirani yako, unaweza kuvuna kichwa cha mavuno kwa mkono wako, lakini haupaswi kutumia mundu kuvuna zao lililoiva la jirani yako.

< Deutéronome 23 >