< 2 Samuel 2 >
1 Et il arriva, après cela, que David interrogea l’Éternel, disant: Monterai-je dans une des villes de Juda? Et l’Éternel lui dit: Monte. Et David dit: Où monterai-je? Et il dit: À Hébron.
Ikawa baada ya mambo haya, Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nipande kwenda katika mojawapo ya miji ya Yuda?” Bwana akasema, “Panda.” Daudi akauliza, “Je, niende wapi?” Bwana akajibu, “Nenda Hebroni.”
2 Et David y monta, et ses deux femmes aussi, Akhinoam, la Jizreélite, et Abigaïl, femme de Nabal, le Carmélite.
Basi Daudi akakwea kwenda huko pamoja na wake zake wawili, Ahinoamu wa Yezreeli na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
3 Et ses hommes qui étaient avec lui, David les fit monter, chacun avec sa maison, et ils habitèrent dans les villes de Hébron.
Pia Daudi akawachukua watu waliokuwa pamoja naye, kila mmoja na jamaa yake, nao wakaishi huko Hebroni na miji yake.
4 Et les hommes de Juda vinrent et oignirent là David pour roi sur la maison de Juda. Et on rapporta à David, disant: Ce sont les hommes de Jabès de Galaad qui ont enterré Saül.
Ndipo watu wa Yuda wakaja Hebroni, huko wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda. Daudi alipoambiwa kuwa ni watu wa Yabeshi-Gileadi waliomzika Sauli,
5 Et David envoya des messagers aux hommes de Jabès de Galaad, et leur fit dire: Bénis soyez-vous de l’Éternel, de ce que vous avez usé de cette bonté envers votre seigneur Saül, et de ce que vous l’avez enterré!
akatuma wajumbe kwa watu wa Yabeshi-Gileadi kuwaambia, “Bwana awabariki kwa kuonyesha wema huu kwa kumzika Sauli bwana wenu.
6 Et maintenant, que l’Éternel use envers vous de bonté et de vérité! Et moi aussi je vous rendrai ce bien, parce que vous avez fait cela.
Sasa Bwana na awaonyeshe wema na uaminifu, nami pia nitawaonyesha wema ule ule kwa kuwa mmefanya jambo hili.
7 Et maintenant, que vos mains se fortifient, et soyez des hommes vaillants; car votre seigneur Saül est mort, et de plus, c’est moi que la maison de Juda a oint pour roi sur elle.
Sasa basi, kuweni hodari na mashujaa, kwa maana bwana wenu Sauli amekufa, nayo nyumba ya Yuda imenitia mafuta niwe mfalme juu yao.”
8 Et Abner, fils de Ner, chef de l’armée de Saül, prit Ish-Bosheth, fils de Saül, et le fit passer à Mahanaïm
Wakati huo Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Sauli, alikuwa amemchukua Ish-Boshethi mwana wa Sauli na kumleta hadi Mahanaimu.
9 et l’établit roi sur Galaad, et sur les Ashurites, et sur Jizreël, et sur Éphraïm, et sur Benjamin, et sur Israël tout entier.
Akamweka awe mfalme juu ya nchi ya Gileadi, Waasheri, Yezreeli, Efraimu, Benyamini na Israeli yote.
10 Ish-Bosheth, fils de Saül, était âgé de 40 ans lorsqu’il régna sur Israël, et il régna deux ans. Toutefois la maison de Juda suivit David.
Ish-Boshethi mwana wa Sauli alikuwa na umri wa miaka arobaini alipoanza kutawala Israeli, naye akatawala miaka miwili. Hata hivyo, nyumba ya Yuda ikamfuata Daudi.
11 Et le nombre des jours, pendant lesquels David fut roi à Hébron sur la maison de Juda, fut de sept ans et six mois.
Muda ambao Daudi alikuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda huko Hebroni ilikuwa miaka saba na miezi sita.
12 Et Abner, fils de Ner, et les serviteurs d’Ish-Bosheth, fils de Saül, sortirent de Mahanaïm vers Gabaon;
Abneri mwana wa Neri, pamoja na watu wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, wakatoka Mahanaimu kwenda Gibeoni.
13 et Joab, fils de Tseruïa, et les serviteurs de David, sortirent aussi; et ils se rencontrèrent ensemble près du réservoir de Gabaon; et ceux-ci s’assirent d’un côté du réservoir, et ceux-là de l’autre côté du réservoir.
Yoabu mwana wa Seruya na watu wa Daudi wakatoka na kukutana nao kwenye bwawa la Gibeoni. Kikundi kimoja kiliketi upande mmoja wa bwawa, na kikundi kingine upande wa pili.
14 Et Abner dit à Joab: Que les jeunes hommes se lèvent donc et jouent [entre eux] devant nous! Et Joab dit: Qu’ils se lèvent.
Ndipo Abneri akamwambia Yoabu, “Tuwaweke baadhi ya vijana wasimame na wapigane ana kwa ana mbele yetu.” Yoabu akasema, “Sawa, na wafanye hivyo.”
15 Et ils se levèrent et passèrent, au nombre de douze pour Benjamin et pour Ish-Bosheth, fils de Saül, et de douze d’entre les serviteurs de David.
Kwa hiyo vijana wakasimama, wakahesabiwa: watu wa Benyamini na wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli kumi na wawili, na upande wa Daudi kumi na wawili.
16 Et chacun saisit son adversaire par la tête, et [passa] son épée dans le flanc de son adversaire, et ils tombèrent [tous] ensemble. Et on appela ce lieu-là Helkath-Hatsurim, qui est en Gabaon.
Kisha kila mtu akakamatana na mpinzani wake kichwani na kuchomana kwa upanga, nao wakaanguka chini pamoja. Kwa hiyo mahali pale katika Gibeoni pakaitwa Helkath-Hasurimu.
17 Et le combat fut très rude ce jour-là; et Abner et les hommes d’Israël furent battus devant les serviteurs de David.
Siku hiyo vita vilikuwa vikali sana, naye Abneri na watu wa Israeli wakashindwa na watu wa Daudi.
18 Et il y avait là trois fils de Tseruïa, Joab, et Abishaï, et Asçaël. Et Asçaël était léger de ses pieds comme une des gazelles qui sont dans les champs.
Wana watatu wa Seruya walikuwako huko: nao ni Yoabu, Abishai na Asaheli. Basi huyo Asaheli alikuwa na mbio kama paa.
19 Et Asçaël poursuivit Abner, et il ne se détourna pas d’Abner pour aller à droite ou à gauche.
Asaheli akamfukuza Abneri, pasipo kugeuka kulia wala kushoto wakati akimfuata.
20 Et Abner regarda derrière lui, et dit: Est-ce toi, Asçaël? Et il dit: C’est moi.
Abneri akaangalia nyuma na kumuuliza, “Ni wewe, Asaheli?” Akamjibu, “Ndiyo.”
21 Et Abner lui dit: Détourne-toi à droite ou à gauche, et saisis-toi de l’un des jeunes hommes et prends pour toi son armure. Mais Asçaël ne voulut pas se détourner de lui.
Ndipo Abneri akamwambia, “Geuka upande wa kulia au kushoto. Mchukue mmoja wa vijana wa kiume na umvue silaha zake.” Lakini Asaheli hakuacha kumfukuza.
22 Et Abner dit encore à Asçaël: Détourne-toi de moi! Pourquoi te jetterais-je mort par terre? Et comment lèverais-je ma face devant Joab, ton frère?
Abneri akamwonya tena Asaheli akimwambia, “Acha kunifukuza! Kwa nini nikuue? Je, nitawezaje kumtazama ndugu yako Yoabu usoni?”
23 Mais il refusa de se détourner, et Abner le frappa au ventre avec la hampe de sa lance, et sa lance lui sortit par-derrière, et il tomba là et mourut sur place. Et tous ceux qui venaient à l’endroit où Asçaël était tombé et était mort, s’arrêtaient.
Lakini Asaheli alikataa kuacha kumfuatia, kwa hiyo Abneri akamchoma Asaheli tumboni kwa ncha butu ya mkuki wake, mkuki ukamtoboa ukatokea mgongoni mwake. Akaanguka na kufa papo hapo. Ikawa kila mtu alisimama alipofika mahali pale Asaheli alipoanguka na kufa.
24 Et Joab et Abishaï poursuivirent Abner; et le soleil se couchait quand ils arrivèrent à la colline d’Amma, qui est devant Guiakh, sur le chemin du désert de Gabaon.
Lakini Yoabu na Abishai walimfuata Abneri, na jua lilipokuwa linatua, wakafika kwenye kilima cha Ama, karibu na Gia kwenye njia ya kuelekea kwenye nyika ya Gibeoni.
25 Et les fils de Benjamin se rassemblèrent derrière Abner; et ils formèrent une seule troupe, et se tinrent sur le sommet d’une colline.
Ndipo watu wa kabila la Benyamini wakakusanyika tena nyuma ya Abneri. Wakaunda kikosi na kujiimarisha juu ya kilima.
26 Et Abner cria à Joab et dit: L’épée dévorera-t-elle à toujours? Ne sais-tu pas qu’il y aura de l’amertume à la fin? et jusques à quand ne diras-tu pas au peuple de revenir de la poursuite de ses frères?
Abneri akamwita Yoabu, akamwambia, “Je, ni lazima upanga uendelee kuangamiza milele? Hutambui kwamba jambo hili litaishia katika uchungu? Utaacha kuwaagiza watu wako waache kuwafuatilia ndugu zao hata lini?”
27 Et Joab dit: Dieu est vivant, que, si tu n’avais parlé, dès le matin [déjà] le peuple se serait retiré, chacun de la poursuite de son frère!
Yoabu akajibu, “Hakika kama aishivyo Mungu, kama hukusema, hawa watu wangeendelea kuwafuatia ndugu zao mpaka asubuhi.”
28 Et Joab sonna de la trompette, et tout le peuple s’arrêta; et ils ne poursuivirent plus Israël, et ils ne continuèrent plus à se battre.
Basi Yoabu akapiga tarumbeta, nao watu wote wakasimama, hawakuwafuata Israeli tena, wala hawakuwapiga tena.
29 Et Abner et ses hommes marchèrent toute cette nuit-là dans la plaine, et traversèrent le Jourdain, et marchèrent par tout le Bithron, et vinrent à Mahanaïm.
Usiku ule wote Abneri na watu wake wakatembea kupitia Araba. Wakavuka Mto Yordani, wakaendelea wakipitia nchi yote ya Bithroni wakafika Mahanaimu.
30 Et Joab s’en retourna de la poursuite d’Abner et rassembla tout le peuple; et, des serviteurs de David, il manquait 19 hommes et Asçaël.
Basi Yoabu akarudi kutoka kumfuatia Abneri, na kuwakusanya watu wake wote. Pamoja na Asaheli, watu kumi na tisa wa Daudi walikuwa wamepotea.
31 Et les serviteurs de David avaient frappé à mort 360 hommes de Benjamin et des hommes d’Abner.
Lakini watu wa Daudi walikuwa wamewaua watu wa kabila la Benyamini 360 waliokuwa pamoja na Abneri.
32 Et ils enlevèrent Asçaël, et l’enterrèrent dans le sépulcre de son père, qui était à Bethléhem; et Joab et ses hommes marchèrent toute la nuit; et il faisait jour lorsqu’ils [arrivèrent] à Hébron.
Wakamchukua Asaheli, wakamzika katika kaburi la baba yake huko Bethlehemu. Kisha Yoabu na watu wake wakatembea usiku kucha na kufika huko Hebroni wakati wa mapambazuko.