< 2 Rois 16 >

1 La dix-septième année de Pékakh, fils de Remalia, Achaz, fils de Jotham, roi de Juda, commença de régner.
Katika mwaka wa kumi na saba wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, Ahazi mwana wa Yothamu mfalme wa Yuda alianza kutawala.
2 Achaz était âgé de 20 ans lorsqu’il commença de régner; et il régna 16 ans à Jérusalem. Et il ne fit pas ce qui est droit aux yeux de l’Éternel, son Dieu, comme [avait fait] David, son père;
Ahazi alikuwa na miaka ishirini alipoanza kutawala, akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na sita. Tofauti na Daudi baba yake, hakufanya yaliyo mema machoni pa Bwana, Mungu wake.
3 mais il marcha dans la voie des rois d’Israël, et même il fit passer son fils par le feu, selon les abominations des nations que l’Éternel avait dépossédées devant les fils d’Israël.
Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, na hata akamtoa mwanawe kafara katika moto, akifuata njia za machukizo za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele ya Waisraeli.
4 Et il sacrifiait et faisait fumer de l’encens sur les hauts lieux, et sur les collines, et sous tout arbre vert.
Akatoa kafara na kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu, juu ya vilima, na chini ya kila mti uliotanda.
5 Alors Retsin, roi de Syrie, et Pékakh, fils de Remalia, roi d’Israël, montèrent à Jérusalem pour lui faire la guerre; et ils assiégèrent Achaz; mais ils ne purent pas le vaincre.
Kisha Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli wakaondoka kwenda kupigana dhidi ya Yerusalemu na kumzunguka Ahazi kwa jeshi, lakini hawakuweza kumshinda.
6 En ce temps-là, Retsin, roi de Syrie, recouvra Élath pour la Syrie; et il expulsa d’Élath les Juifs; et les Syriens entrèrent à Élath, et ils y ont habité jusqu’à ce jour.
Wakati ule, Resini mfalme wa Aramu akaurudisha Elathi kwa Aramu kwa kuwafukuza watu wa Yuda. Kisha Waedomu wakahamia Elathi, nao wanaishi huko mpaka leo.
7 Et Achaz envoya des messagers à Tiglath-Piléser, roi d’Assyrie, disant: Je suis ton serviteur et ton fils; monte, et sauve-moi de la main du roi de Syrie et de la main du roi d’Israël qui s’élèvent contre moi.
Ahazi akatuma wajumbe kumwambia Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru kwamba, “Mimi ni mtumishi na mtumwa wako. Njoo na uniokoe kutoka mkononi mwa mfalme wa Aramu na wa mfalme wa Israeli, ambao wananishambulia.”
8 Et Achaz prit l’argent et l’or, ce qui s’en trouva dans la maison de l’Éternel et dans les trésors de la maison du roi, et l’envoya en présent au roi d’Assyrie.
Naye Ahazi akachukua fedha na dhahabu zilizopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme, na kuzituma kama zawadi kwa mfalme wa Ashuru.
9 Et le roi d’Assyrie l’écouta; et le roi d’Assyrie monta à Damas, et la prit, et en transporta [les habitants] à Kir, et fit mourir Retsin.
Mfalme wa Ashuru akamwitikia kwa kushambulia Dameski na kuiteka. Akawahamishia wenyeji wake huko Kiri, na kumuua Resini.
10 Et le roi Achaz s’en alla à la rencontre de Tiglath-Piléser, roi d’Assyrie, à Damas; et il vit l’autel qui était à Damas; et le roi Achaz envoya à Urie, le sacrificateur, la forme de l’autel et son modèle, selon toute sa façon.
Kisha Mfalme Ahazi akaenda Dameski kukutana na Tiglath-Pileseri wa Ashuru. Akaona madhabahu huko Dameski, naye akamtumia Uria kuhani mchoro wa hayo madhabahu, pamoja na maelezo ya mpango kamili wa ujenzi wake.
11 Et Urie, le sacrificateur, bâtit l’autel selon tout ce que le roi Achaz avait envoyé de Damas; Urie, le sacrificateur, le fit ainsi, en attendant que le roi Achaz revienne de Damas.
Kwa hiyo Uria kuhani akajenga madhabahu kulingana na mipango yote ambayo Mfalme Ahazi alikuwa ameituma kutoka Dameski, na akamaliza ujenzi kabla ya Mfalme Ahazi kurudi.
12 Et le roi revint de Damas, et le roi vit l’autel, et le roi s’approcha de l’autel, et y offrit;
Mfalme aliporudi kutoka Dameski na kuona hayo madhabahu, akayasogelea na kutoa sadaka juu yake.
13 et il fit fumer sur l’autel son holocauste et son offrande de gâteau, et versa sa libation, et fit aspersion du sang de ses sacrifices de prospérités.
Akatoa sadaka yake ya kuteketezwa na sadaka ya nafaka, akamimina sadaka ya kinywaji na kunyunyizia damu ya sadaka zake za amani juu ya hayo madhabahu.
14 Et quant à l’autel d’airain qui était devant l’Éternel, il le fit avancer de devant la maison, d’entre [son] autel et la maison de l’Éternel, et le mit à côté de [son] autel, vers le nord.
Mfalme Ahazi akayaondoa madhabahu ya zamani ya shaba kutoka hapo mbele ya Hekalu la Bwana, yaliyokuwa yamesimama kati ya ingilio la Hekalu na hayo madhabahu mapya, naye akayaweka upande wa kaskazini mwa hayo madhabahu mapya.
15 Et le roi Achaz commanda à Urie, le sacrificateur, disant: Fais fumer sur le grand autel l’holocauste du matin et l’offrande de gâteau du soir, et l’holocauste du roi et son offrande de gâteau, et l’holocauste de tout le peuple du pays, et leur offrande de gâteau, et leurs libations; et tu feras aspersion de tout le sang des holocaustes et de tout le sang des sacrifices sur cet autel; et l’autel d’airain sera pour moi, afin d’y consulter.
Ndipo Mfalme Ahazi akatoa amri zifuatazo kwa Uria kuhani: “Juu ya hayo madhabahu kubwa mapya, toa sadaka ya asubuhi ya kuteketezwa na sadaka ya jioni ya nafaka, sadaka ya mfalme ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa ya watu wote wa nchi, pamoja na sadaka yao ya nafaka na sadaka yao ya kinywaji. Unyunyize juu ya hayo madhabahu damu yote ya sadaka za kuteketezwa na dhabihu. Lakini mimi nitatumia hayo madhabahu ya zamani ya shaba kwa ajili ya kutafuta uongozi.”
16 Et Urie, le sacrificateur, fit selon tout ce que le roi Achaz avait commandé.
Naye Uria kuhani akafanya kama Mfalme Ahazi alivyoagiza.
17 Et le roi Achaz enleva les panneaux des bases, et ôta les cuves qui étaient dessus; et il fit descendre la mer de dessus les bœufs d’airain qui étaient sous elle, et la mit sur un pavé de pierre.
Mfalme Ahazi akaondoa mbao za pembeni na kuondoa masinia kwenye vile vishikilio vilivyohamishika. Akaondoa ile Bahari kutoka kwenye mafahali wa shaba walioishikilia, na kuiweka kwenye kitako cha jiwe.
18 Et il changea, dans la maison de l’Éternel, le portique du sabbat, qu’on avait bâti dans la maison, et l’entrée extérieure du roi, à cause du roi d’Assyrie.
Kwa heshima ya mfalme wa Ashuru, akaliondoa pia pazia la Sabato lililokuwa limewekwa ndani ya Hekalu, na akaondoa ile njia ya kifalme ya kuingia kwenye Hekalu la Bwana.
19 Et le reste des actes d’Achaz, ce qu’il fit, cela n’est-il pas écrit dans le livre des chroniques des rois de Juda?
Matukio mengine ya utawala wa Ahazi na yale aliyoyafanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
20 Et Achaz s’endormit avec ses pères, et fut enterré avec ses pères dans la ville de David; et Ézéchias, son fils, régna à sa place.
Ahazi akalala na baba zake, naye akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Naye Hezekia mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Rois 16 >