< 2 Rois 12 >

1 La septième année de Jéhu, Joas commença de régner; et il régna 40 ans à Jérusalem; et le nom de sa mère était Tsibia, de Beër-Shéba.
Katika mwaka wa saba wa utawala wa Yehu, Yoashi alianza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka arobaini. Jina la mama yake aliitwa Sibia, kutoka Beer-Sheba.
2 Et Joas fit ce qui est droit aux yeux de l’Éternel, tous les jours que Jehoïada, le sacrificateur, l’instruisit.
Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana miaka yote ambayo Yehoyada kuhani alikuwa akimwelekeza.
3 Seulement les hauts lieux ne furent pas ôtés; le peuple sacrifiait encore et faisait fumer de l’encens sur les hauts lieux.
Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
4 Et Joas dit aux sacrificateurs: Tout l’argent des choses saintes qui est apporté dans la maison de l’Éternel, l’argent de tout homme qui passe [par le dénombrement], l’argent des âmes selon l’estimation de chacun, tout argent qu’il monte au cœur de chacun d’apporter dans la maison de l’Éternel,
Yoashi akawaambia makuhani, “Kusanyeni fedha zote ambazo zitaletwa kama sadaka takatifu kwenye Hekalu la Bwana, yaani fedha zilizokusanywa kama kodi, fedha zilizopokelewa kutokana na nadhiri za watu binafsi, na fedha zilizoletwa kwa hiari hekaluni.
5 que les sacrificateurs le prennent, chacun de la part [des gens] de sa connaissance, et qu’ils réparent les brèches de la maison, partout où il se trouvera des brèches.
Kila kuhani na apokee fedha kutoka kwa mmoja wa watunza hazina, nazo zitumike kukarabati uharibifu wowote unaoonekana katika Hekalu.”
6 Et il arriva, la vingt-troisième année du roi Joas, que les sacrificateurs n’avaient point réparé les brèches de la maison.
Lakini ikawa kufikia mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake Mfalme Yoashi, makuhani walikuwa bado hawajalikarabati Hekalu.
7 Et le roi Joas appela Jehoïada, le sacrificateur, et les [autres] sacrificateurs, et il leur dit: Pourquoi n’avez-vous pas réparé les brèches de la maison? Et maintenant, ne prenez pas d’argent de vos connaissances, mais vous le donnerez pour les brèches de la maison.
Kwa hiyo Mfalme Yoashi akamwita Yehoyada kuhani na makuhani wengine, akawauliza, “Kwa nini hamtengenezi uharibifu uliofanyika hekaluni? Msichukue fedha zaidi kutoka kwa watunza hazina wenu kwa ajili ya matumizi yenu, lakini kuanzia sasa ni lazima fedha yote itumike kwa ajili ya kukarabati Hekalu.”
8 Et les sacrificateurs consentirent à ne plus prendre d’argent de la part du peuple, et que seulement on répare les brèches de la maison.
Makuhani wakakubali kuwa hawatakusanya tena fedha kutoka kwa watu na kwamba hawatakarabati Hekalu wenyewe.
9 Et Jehoïada, le sacrificateur, prit un coffre et fit un trou dans son couvercle, et le mit à côté de l’autel, à droite quand on entre dans la maison de l’Éternel; et les sacrificateurs qui gardaient le seuil mettaient là tout l’argent qui était apporté à la maison de l’Éternel.
Yehoyada kuhani akachukua kisanduku na akatoboa tundu kwenye kifuniko chake. Akakiweka kando ya madhabahu upande wa kulia unapoingia hekaluni mwa Bwana. Makuhani waliolinda ingilio wakaweka ndani ya kisanduku fedha zote ambazo zililetwa katika Hekalu la Bwana.
10 Et il arrivait que, lorsqu’ils voyaient qu’il y avait beaucoup d’argent dans le coffre, le secrétaire du roi montait, et le grand sacrificateur, et ils serraient et comptaient l’argent qui était trouvé dans la maison de l’Éternel;
Kila mara walipoona kuwa kuna kiasi kikubwa cha fedha ndani ya kisanduku, mwandishi wa mfalme na kuhani mkuu walikuja, wakazihesabu fedha hizo zilizoletwa katika Hekalu la Bwana, na kuziweka katika mifuko.
11 et ils remettaient l’argent pesé entre les mains de ceux qui faisaient l’ouvrage, qui étaient établis sur la maison de l’Éternel, et ceux-ci le livraient aux charpentiers et aux constructeurs qui travaillaient à la maison de l’Éternel,
Wakiisha kuthibitisha kiasi cha hizo fedha, waliwapa watu walioteuliwa kusimamia kazi katika Hekalu. Kwa fedha hizo, wakawalipa wale watu waliofanya kazi katika Hekalu la Bwana: yaani, maseremala na wajenzi,
12 et aux maçons, et aux tailleurs de pierres, pour acheter des bois et des pierres de taille, afin de réparer les brèches de la maison de l’Éternel, et pour tout ce qui se dépensait pour la maison afin de la réparer.
waashi na wakata mawe. Walinunua mbao na mawe ya kuchongwa kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana, na kulipia gharama nyingine zote za kulitengeneza.
13 Toutefois on ne fit pas pour la maison de l’Éternel des écuelles d’argent, des couteaux, des bassins, des trompettes, ni aucun ustensile d’or ou ustensile d’argent, avec l’argent qu’on apportait dans la maison de l’Éternel;
Fedha zilizoletwa kwenye Hekalu hazikutumiwa kutengenezea masinia ya fedha, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, tarumbeta wala vyombo vingine vyovyote vya dhahabu au fedha kwa ajili ya Hekalu la Bwana;
14 mais on le donnait à ceux qui faisaient l’ouvrage, et ils l’employaient à réparer la maison de l’Éternel.
zililipwa kwa wafanyakazi, ambao walizitumia kwa kukarabati Hekalu.
15 Et on ne comptait pas avec les hommes entre les mains desquels on remettait l’argent pour le donner à ceux qui faisaient l’ouvrage, car ils agissaient fidèlement.
Wao hawakudai kupewa hesabu ya fedha kutoka kwa wale waliowapa ili kuwalipa wafanyakazi, kwa sababu walifanya kwa uaminifu wote.
16 L’argent des sacrifices pour le délit et l’argent des sacrifices pour le péché n’était point apporté dans la maison de l’Éternel; il était pour les sacrificateurs.
Fedha zilizopatikana kutokana na sadaka za hatia na sadaka za dhambi hazikuletwa katika Hekalu la Bwana; zilikuwa mali ya makuhani.
17 Alors Hazaël, roi de Syrie, monta, et fit la guerre contre Gath, et la prit; et Hazaël tourna sa face pour monter contre Jérusalem.
Wakati huu Hazaeli mfalme wa Aramu akapanda kuishambulia Gathi, akaiteka. Kisha akageuka ili kuishambulia Yerusalemu.
18 Et Joas, roi de Juda, prit toutes les choses saintes, que Josaphat, et Joram, et Achazia, ses pères, rois de Juda, avaient consacrées, et celles qu’il avait lui-même consacrées, et tout l’or qui se trouvait dans les trésors de la maison de l’Éternel et de la maison du roi, et les envoya à Hazaël, roi de Syrie: et il se retira de devant Jérusalem.
Lakini Yoashi mfalme wa Yuda akavichukua vyombo vyote vitakatifu vilivyowekwa wakfu na baba zake, yaani Yehoshafati, Yehoramu na Ahazia, wafalme wa Yuda, zawadi ambazo yeye mwenyewe alikuwa ameziweka wakfu pamoja na dhahabu yote iliyokutwa katika hazina za Hekalu la Bwana na katika jumba la kifalme, akazipeleka kwa Hazaeli mfalme wa Aramu, ambaye hatimaye aliondoka Yerusalemu.
19 Et le reste des actes de Joas, et tout ce qu’il fit, cela n’est-il pas écrit au livre des chroniques des rois de Juda?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Yoashi na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
20 Et ses serviteurs se levèrent et firent une conspiration, et frappèrent Joas dans la maison de Millo, à la descente de Silla.
Maafisa wake wakafanya shauri baya dhidi yake, nao wakamuulia Yoashi huko Beth-Milo, kwenye barabara iteremkayo kuelekea Sila.
21 Et Jozacar, fils de Shimhath, et Jozabad, fils de Shomer, ses serviteurs, le frappèrent, et il mourut; et on l’enterra avec ses pères dans la ville de David. Et Amatsia, son fils, régna à sa place.
Maafisa waliomuua walikuwa Yozabadi mwana wa Shimeathi, na Yehozabadi mwana wa Shomeri. Akafa na akazikwa pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi. Naye Amazia mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Rois 12 >