< 2 Chroniques 3 >
1 Et Salomon commença de bâtir la maison de l’Éternel à Jérusalem, sur la montagne de Morija, où [l’Éternel] était apparu à David, son père, sur l’emplacement que David avait préparé dans l’aire d’Ornan, le Jébusien.
Kisha Selemani akaanza kuijenga nyumba ya Yahwe katika Yerusalemu juu ya Mlima Moria, ambako Yahwe alimtokea Daudi baba yake. Aliandaa sehemu ambayo Daudi aliikusudia, katika sakafu ya kupuria ya Arauna Myebusi.
2 Et il commença de bâtir le second [jour] du second mois, en la quatrième année de son règne.
Alianza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili, katika mwaka wa nne wa utawala wake.
3 Et c’est ici le fondement que Salomon posa pour bâtir la maison de Dieu: la longueur, en coudées, d’après l’ancienne mesure, était de 60 coudées, et la largeur, de 20 coudées.
Sasa hivi ndinyo vipimo vya ule msingi ambao Selemani alijenga kwa ajili ya nyumba ya Mungu. Akitumia mtindo wa vipimo vya zamani, urefu ulikuwa mikono sitini, na upana ulikuwa mikono ishirini.
4 Et le portique qui était devant avait 20 coudées de longueur, selon la largeur de la maison; et sa hauteur était de 120 [coudées]; et il le recouvrit à l’intérieur d’or pur.
Urefu wa ukumbi mbele ya nyumba ulikuwa mikono ishirini, ukilingana na upana wa nyumba, urefu wake kwenda juu pia ulikuwa mikono ishirini, na Selemani akaifunika sehemu ya ndani kwa dhahabu halisi.
5 Et la grande maison, il la revêtit de bois de cyprès; et il la revêtit d’or fin, et il y fit des palmiers et des chaînes.
Akailitengeneza paa la ukumbi mkuu kwa miti ya miberoshi, ambayo aliifunika kwa dhahabu halisi, na ambayo aliifunika kwa miti ya mitende na minyororo.
6 Et il recouvrit la maison de pierres précieuses, pour [son] ornement; et l’or était de l’or de Parvaïm.
Akaipamba nyumba kwa vito vya thamani; dhahabu ilikuwa dhahabu kutoka Parvaimu.
7 Et il revêtit d’or la maison, les solives, les seuils, et ses murs, et ses portes; et il entailla des chérubins sur les murs.
Pia akazifunika boriti zake, vizingiti, kuta, na milango kwa dhahabu; akachonga makerubi juu ya kuta zake.
8 Et il fit la maison du lieu très saint: sa longueur, selon la largeur de la maison, de 20 coudées, et sa largeur de 20 coudées; et il la revêtit d’or fin, se montant à 600 talents.
Akaijenga sehemu ya patakatifu pa patakatifu. Urefu wake ulilingana na upana wa nyumba, mikono ishirini, na upana wake pia ulikuwa mikono ishirini. Aliifunika kwa dhahabu halisi, thamani yake ilikuwa talanta mia sita.
9 Et le poids des clous se montait à 50 sicles d’or; et il revêtit d’or les chambres hautes.
Uzito wa misumari ulikuwa shekeli hamsini za dhahabu. Alizifunika sehemu za juu kwa dhahabu.
10 Et il fit dans la maison du lieu très saint deux chérubins, d’ouvrage de statuaire, et on les recouvrit d’or.
Akachonga makerubi wawili kwa ajili ya sehemu za patakatifu pa patakatifu, wahunzi wakayafunika kwa dhahabu. (Maandishi ya kale yanasema: makerubi wawili waliochongwa kwenye mbao).
11 Et les ailes des chérubins avaient 20 coudées de long; une aile de l’un, de cinq coudées, touchait le mur de la maison; et l’autre aile, de cinq coudées, touchait l’aile de l’autre chérubin.
Mabawa ya makerubi yalikuwa na urefu wa mikono ishirini yote kwa pamoja; bawa la kerubi mmoja lilikuwa na urefu wa mikono mitano, lilifikia kwenye ukuta wa chumba; bawa jingine lilikuwa na urefu wa mikono mitano pia.
12 Et l’aile de l’autre chérubin, de cinq coudées, touchait le mur de la maison; et l’autre aile, de cinq coudées, joignait l’aile de l’autre chérubin.
Bawa la kerubi mwingine lilikuwa mikono mitano, likifikia kwenye ukuta wa chumba; bawa lake jingine lilikuwa mikono mitano pia, likigusana na bawa la kerubi wa kwanza.
13 Les ailes de ces chérubins, déployées, [avaient] 20 coudées; et ils se tenaient debout sur leurs pieds, et leurs faces [regardaient] vers la maison.
Mabawa ya makerubi hawa yalienea jumla ya mikono mitano. Makerubi yalisimama kwa miguu yake, na nyuso zake zikiuelekea ukumbi mkuu.
14 Et il fit le voile de bleu, et de pourpre, et de cramoisi, et de byssus, et mit dessus des chérubins.
Akatengeneza pazia la samawati, dhambarau, na sufu nyekundu, na kitani safi, na akachora makerubi juu yake.
15 Et devant la maison il fit deux colonnes de 35 coudées de hauteur; et le chapiteau qui était sur leur sommet était de cinq coudées.
Selemani pia akatengeneza nguzo mbili, kila moja ikiwa na urefu wa mikono thelathini na tano kwenda juu, kwa maana mbele ya nyumba; taji ambazo zilikuwa juu ya nguzo zilikuwa na urefu wa mikono mitano kwenda juu.
16 Et il fit des chaînes [comme] dans l’oracle, et les mit sur le sommet des colonnes; et il fit 100 grenades, et les mit aux chaînes.
Akatengeneza minyororo kwa ajili ya nguzo na akaiweka juu yake, pia akatengeneza maakomamanga mia moja na akayaunganisha kwenye minyororo.
17 Et il dressa les colonnes devant le temple, l’une à droite, l’autre à gauche; et il appela le nom de celle qui était à droite, Jakin; et le nom de celle qui était à gauche, Boaz.
Akazisimamisha nguzo mbele ya hekalu, mkono wa kulia, na nyingine mkono wa kushoto; akaiita nguzo ya kulia Yakini, na nguzo ya kushoto akaiita Boazi.