< 2 Chroniques 17 >

1 Et Josaphat, son fils, régna à sa place; et il se fortifia contre Israël,
Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake na akajiimarisha dhidi ya Israeli.
2 et mit des troupes dans toutes les villes fortes de Juda, et mit des garnisons dans le pays de Juda et dans les villes d’Éphraïm qu’Asa, son père, avait prises.
Akaweka jeshi katika miji yote ya Yuda yenye ngome na kuweka askari walinzi katika Yuda na katika miji ya Efraimu ile ambayo baba yake Asa alikuwa ameiteka.
3 Et l’Éternel fut avec Josaphat, car il marcha dans les premières voies de David, son père, et ne rechercha point les Baals,
Bwana Mungu alikuwa na Yehoshafati kwa sababu katika miaka yake ya mwanzoni alienenda katika njia za Daudi baba yake. Hakutafuta Mabaali
4 mais il rechercha le Dieu de son père, et marcha dans ses commandements, et non comme faisait Israël.
bali alimtafuta Mungu wa baba yake na kuzifuata amri zake badala ya kufuata desturi za watu wa Israeli.
5 Et l’Éternel affermit le royaume dans sa main; et tout Juda fit des présents à Josaphat, et il eut beaucoup de richesses et de gloire.
Kwa hiyo Bwana akauimarisha ufalme chini ya uongozi wake, nao Yuda wote wakamletea Yehoshafati zawadi, hivyo akawa na utajiri mwingi na heshima.
6 Et il prit courage dans les voies de l’Éternel, et de plus, il ôta de Juda les hauts lieux et les ashères.
Moyo wake ukawa hodari katika njia za Bwana na zaidi ya yote, akaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu na nguzo za Maashera katika Yuda.
7 Et la troisième année de son règne, il envoya ses chefs, Ben-Haïl, et Abdias, et Zacharie, et Nethaneël, et Michée, pour enseigner dans les villes de Juda;
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa akatuma maafisa wake ambao ni: Ben-Haili, Obadia, Zekaria, Nethaneli na Mikaya ili kufundisha katika miji ya Yuda.
8 et avec eux les lévites, Shemahia, et Nethania, et Zebadia, et Asçaël, et Shemiramoth, et Jonathan, et Adonija, et Tobija, et Tob-Adonija, lévites; et avec eux Élishama et Joram, sacrificateurs;
Pamoja nao walikuwepo Walawi fulani nao ni: Shemaya, Nethania, Zebadia, Asaheli, Shemiramothi, Yehonathani, Adoniya, Tobia, Tob-Adonia, pamoja nao walikuwepo makuhani Elishama na Yehoramu.
9 et ils enseignèrent en Juda, ayant avec eux le livre de la loi de l’Éternel; et ils firent le tour de toutes les villes de Juda, et enseignèrent parmi le peuple.
Wakafundisha Yuda yote, wakiwa wamechukua Kitabu cha Sheria ya Bwana wakazunguka miji yote ya Yuda na kufundisha watu.
10 Et la frayeur de l’Éternel fut sur tous les royaumes des pays qui étaient autour de Juda, et ils ne firent pas la guerre à Josaphat.
Hofu ya Bwana ikawa juu ya falme zote za nchi zilizozunguka Yuda, hivyo hawakufanya vita na Yehoshafati.
11 Et il y eut des Philistins qui apportèrent à Josaphat des présents, et de l’argent comme tribut; les Arabes aussi lui amenèrent du menu bétail, 7 700 béliers et 7 700 boucs.
Baadhi ya Wafilisti wakamletea Yehoshafati zawadi na fedha kama ushuru, nao Waarabu wakamletea mifugo: kondoo dume 7,700 na mbuzi 7,700.
12 Et Josaphat alla grandissant jusqu’au plus haut degré. Et il bâtit en Juda des châteaux et des villes à entrepôts.
Yehoshafati akaendelea kupata nguvu zaidi na zaidi, akajenga ngome na miji ya hazina katika Yuda
13 Et il eut beaucoup de travail dans les villes de Juda, et des hommes de guerre forts et vaillants dans Jérusalem.
na akawa na wingi mkubwa wa vitu katika miji ya Yuda. Pia aliweka askari wa vita wenye uzoefu huko Yerusalemu.
14 Et c’est ici leur recensement, selon leurs maisons de pères: pour Juda, les chefs de milliers, Adna, le chef, et avec lui 300 000 hommes forts et vaillants;
Wakaandikishwa katika jamaa zao kama ifuatavyo: Kutoka Yuda, majemadari wa vikosi vya elfu: Jemadari Adna akiwa na askari wa vita 300,000;
15 et à côté de lui, Jokhanan, le chef, et avec lui 280 000;
aliyefuata ni jemadari Yehohanani, akiwa na askari 280,000 walio tayari kwa vita;
16 et à côté de lui, Amasia, fils de Zicri, qui s’était volontairement donné à l’Éternel, et avec lui 200 000 hommes forts et vaillants.
aliyefuata ni Amasia mwana wa Zikri, ambaye alijitolea kwa ajili ya kazi ya Bwana, akiwa na askari 200,000.
17 Et de Benjamin, l’homme fort et vaillant, Éliada, et avec lui 200 000 [hommes] armés de l’arc et de l’écu;
Kutoka Benyamini: Eliada, askari shujaa akiwa na watu 200,000 wenye silaha za nyuta na ngao;
18 et à côté de lui, Jozabad, et avec lui 180 000 [hommes] équipés pour l’armée.
aliyefuata ni Yehozabadi, akiwa na askari 180,000 wenye silaha za vita.
19 Ce sont là ceux qui servaient le roi, outre ceux que le roi avait mis dans les villes fortes, dans tout Juda.
Hawa ndio waliomtumikia mfalme, mbali na wale mfalme aliweka katika miji yenye ngome huko Yuda yote.

< 2 Chroniques 17 >