< 2 Chroniques 12 >

1 Et il arriva que, quand le royaume de Roboam fut affermi, et qu’il se fut fortifié, il abandonna la loi de l’Éternel, et tout Israël avec lui.
Baada ya nafasi ya Rehoboamu kuimarika na kuwa na nguvu, yeye na Israeli yote waliiacha sheria ya Bwana Mungu.
2 Et parce qu’ils avaient péché contre l’Éternel, il arriva, en la cinquième année du roi Roboam, que Shishak, roi d’Égypte, monta contre Jérusalem,
Kwa sababu hawakuwa waaminifu kwa Bwana, Shishaki mfalme wa Misri akashambulia Yerusalemu katika mwaka wa tano wa utawala wa Mfalme Rehoboamu.
3 avec 1 200 chars et 60 000 cavaliers; et le peuple qui vint avec lui d’Égypte, Libyens, Sukkiens, et Éthiopiens, était sans nombre;
Akiwa na magari ya vita 1,200 na wapanda farasi 60,000 na idadi isiyohesabika ya majeshi ya Walibia, Wasukii na Wakushi yaliyokuja pamoja naye kutoka Misri.
4 et il prit les villes fortes qui étaient à Juda, et vint jusqu’à Jérusalem.
Akateka miji ya Yuda yenye ngome akaendelea mpaka Yerusalemu.
5 Et Shemahia, le prophète, vint vers Roboam et vers les chefs de Juda qui s’étaient assemblés à Jérusalem, fuyant Shishak, et leur dit: Ainsi dit l’Éternel: Vous m’avez abandonné, et moi je vous ai aussi abandonnés aux mains de Shishak.
Ndipo nabii Shemaya akaja kwa Rehoboamu na kwa viongozi wa Yuda waliokuwa wamekusanyika huko Yerusalemu kwa ajili ya hofu ya Shishaki naye akawaambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, ‘Ninyi mmeniacha mimi, kwa hiyo, mimi nami sasa ninawaacha ninyi mkononi mwa Shishaki.’”
6 Et les chefs d’Israël et le roi s’humilièrent, et dirent: L’Éternel est juste.
Viongozi wa Israeli na mfalme wakajinyenyekeza na kusema, “Bwana Mungu ni mwenye haki.”
7 Et quand l’Éternel vit qu’ils s’étaient humiliés, la parole de l’Éternel vint à Shemahia, disant: Ils se sont humiliés, je ne les détruirai pas; je leur donnerai un peu de délivrance, et ma fureur ne se déversera pas sur Jérusalem par le moyen de Shishak;
Bwana Mungu alipoona kwamba wamejinyenyekeza, neno hili la Bwana likamjia Shemaya: “Maadamu wamejinyenyekeza, sitawaangamiza bali hivi karibuni nitawapatia wokovu. Ghadhabu yangu haitamwagwa juu ya Yerusalemu kwa kupitia Shishaki.
8 mais ils lui seront asservis, et ils connaîtront ce que c’est que mon service, et le service des royaumes des pays.
Hata hivyo, watamtumikia Shishaki ili wapate kujifunza tofauti kati ya kunitumikia mimi na kuwatumikia wafalme wa nchi nyingine.”
9 Et Shishak, roi d’Égypte, monta contre Jérusalem, et prit les trésors de la maison de l’Éternel et les trésors de la maison du roi: il prit tout. Et il prit les boucliers d’or que Salomon avait faits.
Shishaki mfalme wa Misri alipoishambulia Yerusalemu, alichukua hazina za Hekalu la Bwana na hazina za jumba la kifalme. Akachukua kila kitu, pamoja na zile ngao za dhahabu ambazo Solomoni alikuwa amezitengeneza.
10 Et le roi Roboam fit à leur place des boucliers d’airain, et les confia aux mains des chefs des coureurs qui gardaient l’entrée de la maison du roi.
Kwa hiyo Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba badala ya zile za dhahabu na kuzikabidhi kwa majemadari wa ulinzi wa zamu kwenye ingilio la jumba la mfalme.
11 Et toutes les fois que le roi entrait dans la maison de l’Éternel, il arrivait que les coureurs venaient et les portaient, puis ils les rapportaient dans la chambre des coureurs.
Kila wakati mfalme alipokwenda katika Hekalu la Bwana walinzi walikwenda pamoja naye wakiwa wamebeba hizo ngao na baadaye walizirudisha kwenye chumba cha ulinzi.
12 Et quand il s’humilia, la colère de l’Éternel se détourna de lui, et il ne le détruisit pas entièrement; et aussi il y avait en Juda de bonnes choses.
Kwa sababu Rehoboamu alijinyenyekeza, hasira ya Bwana ikageukia mbali naye, hakuangamizwa kabisa. Kukawa na hali nzuri katika Yuda.
13 Et le roi Roboam se fortifia dans Jérusalem, et régna. Or Roboam était âgé de 41 ans lorsqu’il commença de régner; et il régna 17 ans à Jérusalem, la ville que l’Éternel avait choisie d’entre toutes les tribus d’Israël pour y mettre son nom; et le nom de sa mère était Naama, une Ammonite.
Mfalme Rehoboamu akajiweka imara katika Yerusalemu na akaendelea kuwa mfalme. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na saba, mji ambao Bwana alikuwa ameuchagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli ili aliweke Jina lake humo. Mama yake aliitwa Naama, alikuwa Mwamoni.
14 Mais il fit le mal; car il n’appliqua pas son cœur à rechercher l’Éternel.
Rehoboamu akatenda maovu kwa sababu hakuuelekeza moyo wake katika kumtafuta Bwana Mungu.
15 Et les actes de Roboam, les premiers et les derniers, ne sont-ils pas écrits dans les paroles de Shemahia, le prophète, et d’Iddo, le voyant, dans les registres généalogiques? Et il y eut des guerres continuelles entre Roboam et Jéroboam.
Kwa habari ya matukio katika utawala wa Rehoboamu, tangu mwanzo mpaka mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Shemaya na mwonaji Ido zinazohusiana na vizazi? Kulikuwako na vita mara kwa mara kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.
16 Et Roboam s’endormit avec ses pères, et il fut enterré dans la ville de David; et Abija, son fils, régna à sa place.
Rehoboamu akalala na baba zake, akazikwa katika Mji wa Daudi. Naye Abiya mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Chroniques 12 >