< 1 Chroniques 9 >

1 Et tous ceux d’Israël furent enregistrés par généalogies; et voici, ils sont inscrits dans le livre des rois d’Israël. Et Juda fut transporté à Babylone à cause de ses péchés.
Waisraeli wote waliorodheshwa katika koo zilizoandikwa kwenye kitabu cha wafalme wa Israeli. Watu wa Yuda walichukuliwa mateka kwenda Babeli kwa sababu ya kukosa uaminifu kwa Mungu.
2 Et les premiers habitants qui étaient dans leurs possessions, dans leurs villes, étaient Israël, les sacrificateurs, les lévites, et les Nethiniens.
Basi watu wa kwanza kurudi kukaa kwenye milki zao katika miji yao walikuwa baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi na watumishi wa Hekalu.
3 Et à Jérusalem habitèrent des fils de Juda, et des fils de Benjamin, et des fils d’Éphraïm et de Manassé:
Wale waliotoka Yuda, Benyamini, Efraimu na Manase ambao waliishi Yerusalemu walikuwa:
4 Uthaï, fils d’Ammihud, fils d’Omri, fils d’Imri, fils de Bani, des fils de Pérets, fils de Juda.
Uthai mwana wa Amihudi, mwana wa Omri, mwana wa Imri, mwana wa Bani, wa wana wa Peresi, mwana wa Yuda.
5 Et des Shilonites: Asçaïa, le premier-né, et ses fils.
Wazao wa Washiloni waliorudi ni: Asaya mzaliwa wa kwanza na wanawe.
6 Et des fils de Zérakh: Jehuel, et ses frères, 690.
Kwa wana wa Zera: Yeueli. Watu wa Yuda jumla yao walikuwa watu 690.
7 Et des fils de Benjamin: Sallu, fils de Meshullam, fils d’Hodavia, fils d’Hassenua;
Kwa Benyamini walikuwa: Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Hodavia, mwana wa Hasenua;
8 et Jibneïa, fils de Jerokham; et Éla, fils d’Uzzi, fils de Micri; et Meshullam, fils de Shephatia, fils de Rehuel, fils de Jibnija;
Ibneya mwana wa Yerohamu, Ela mwana wa Uzi, mwana wa Mikri; na Meshulamu mwana wa Shefatia, mwana wa Reueli, mwana wa Ibniya.
9 et leurs frères, selon leurs générations, 956. Tous ces hommes-là étaient chefs des pères de leurs maisons de pères.
Watu kutoka Benyamini kama walivyoorodheshwa katika koo zao jumla yao ni 956. Watu hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa zao.
10 Et des sacrificateurs: Jedahia, et Joïarib, et Jakin;
Wa jamaa za makuhani walikuwa: Yedaya, Yehoyaribu na Yakini;
11 et Azaria, fils de Hilkija, fils de Meshullam, fils de Tsadok, fils de Meraïoth, fils d’Akhitub, prince de la maison de Dieu;
Azaria mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu aliyekuwa afisa kiongozi wa nyumba ya Mungu.
12 et Adaïa, fils de Jerokham, fils de Pashkhur, fils de Malkija; et Mahçaï, fils d’Adiel, fils de Jakhzéra, fils de Meshullam, fils de Meshillémith, fils d’Immer;
Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya; Maasai, mwana wa Adieli, mwana wa Yahzera, mwana wa Meshulamu, mwana wa Meshilemithi, mwana wa Imeri.
13 et leurs frères, chefs de leurs maisons de pères, 1 760 hommes forts et vaillants, pour l’œuvre du service de la maison de Dieu.
Makuhani waliokuwa viongozi wa jamaa zao walikuwa 1,760. Walikuwa watu wenye uwezo, waliowajibika kuhudumu katika nyumba ya Mungu.
14 Et des lévites: Shemahia, fils de Hashub, fils d’Azrikam, fils de Hashabia, des fils de Merari;
Jamaa za Walawi walikuwa: Shemaya, mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, wa wana wa Merari.
15 et Bakbakkar, Héresh, et Galal; et Matthania, fils de Michée, fils de Zicri, fils d’Asaph;
Bakbakari, Hereshi, Galali na Matania mwana wa Mika, mwana wa Zikri, mwana wa Asafu.
16 et Abdias, fils de Shemahia, fils de Galal, fils de Jeduthun; et Bérékia, fils d’Asa, fils d’Elkana, qui habitait dans les villages des Netophathites.
Obadia mwana wa Shemaya, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni. Berekia mwana wa Asa, mwana wa Elikana, ambao waliishi katika vijiji vya Wanetofathi.
17 Et les portiers: Shallum, et Akkub, et Talmon, et Akhiman, et leurs frères; Shallum était le chef.
Mabawabu katika Hekalu la Bwana waliorudi walikuwa: Shalumu, Akubu, Talmoni, Ahimani na ndugu zao. Shalumu alikuwa mlinzi wao mkuu.
18 Et [ils sont] jusqu’à maintenant à la porte du roi, au levant; ils étaient les portiers des camps des fils de Lévi.
Walikuwa wamewekwa katika lango la mfalme lililokuwa upande wa mashariki, mpaka wakati huu. Hawa walikuwa mabawabu wa kutoka kwenye kambi ya Walawi.
19 Et Shallum, fils de Koré, fils d’Ébiasaph, fils de Coré, et ses frères, les Corites, de la maison de son père, étaient [préposés] sur l’œuvre du service, gardant les seuils de la tente: et leurs pères avaient été [préposés] sur le camp de l’Éternel, gardant l’entrée;
Shalumu mwana wa Kore, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora, pamoja na mabawabu wenzake kutoka jamaa yake ya Kora waliwajibika kulinda malango ya Hema, kama vile baba zao walivyokuwa wamewajibika kulinda ingilio la Maskani ya Bwana.
20 et Phinées, fils d’Éléazar, fut autrefois prince sur eux: l’Éternel était avec lui.
Hapo zamani Finehasi mwana wa Eleazari alikuwa kiongozi wa mabawabu, naye Bwana alikuwa pamoja naye:
21 Zacharie, fils de Meshélémia, était portier à l’entrée de la tente d’assignation.
Zekaria mwana wa Meshelemia alikuwa bawabu katika ingilio la Hema la Kukutania.
22 Tous ceux-là, choisis pour portiers des seuils, étaient 212; ils furent enregistrés par généalogies dans leurs villages; David et Samuel, le voyant, les avaient établis dans leur charge.
Jumla ya waliochaguliwa kuwa mabawabu katika sakafu za kupuria nafaka walikuwa watu 212. Waliandikishwa kwa koo zao kwenye vijiji vyao. Mabawabu hawa waliwekwa katika nafasi zao za kuaminiwa na Daudi pamoja na mwonaji Samweli.
23 Et eux, et leurs fils, étaient [établis] aux portes de la maison de l’Éternel, de la maison de la tente, pour y faire la garde.
Wao na wazao wao walikuwa viongozi wa kulinda malango ya nyumba ya Bwana, nyumba iliyoitwa Hema.
24 Les portiers étaient vers les quatre vents, à l’orient, à l’occident, au nord, et au midi.
Mabawabu walikuwa pande zote nne: mashariki, magharibi, kaskazini na kusini.
25 Et leurs frères, dans leurs villages, devaient venir de sept jours en sept jours, d’un terme à l’autre, auprès d’eux;
Ndugu zao katika vijiji vyao walikuwa wakija mara kwa mara na kuwasaidia katika kazi zao kwa vipindi mbalimbali vya siku saba.
26 car, dans leur charge, ces quatre furent les principaux portiers: ils étaient Lévites; et ils étaient [préposés] sur les chambres et sur les trésors de la maison de Dieu,
Lakini mabawabu wanne wakuu, waliokuwa Walawi, walikabidhiwa wajibu kwa ajili ya vyumba na hazina katika nyumba ya Mungu.
27 et ils se tenaient la nuit autour de la maison de Dieu, car la garde leur en appartenait, et ils en avaient la clé, [pour ouvrir] chaque matin.
Walikesha mahali walipowekwa kuizunguka nyumba ya Mungu, kwa sababu iliwapasa kuilinda. Pia walitunza funguo kwa ajili ya kufungua mlango kila siku asubuhi.
28 Il y en avait aussi quelques-uns d’entre eux [qui étaient préposés] sur les ustensiles du service; car ils les rentraient en les comptant, et ils les sortaient en les comptant.
Baadhi yao walikuwa viongozi wa kutunza vifaa vilivyotumika katika huduma ndani ya Hekalu; walivihesabu kila vilipoingizwa ndani na kila vilipotolewa.
29 Et il y en avait qui étaient préposés sur les vases, et sur tous les ustensiles du lieu saint, et sur la fleur de farine, et sur le vin, et sur l’huile, et sur l’encens, et sur les aromates.
Wengine walipangiwa kutunza mapambo na vifaa vingine vya patakatifu, pamoja na unga, divai, mafuta, uvumba na vikolezo.
30 Et c’étaient des fils des sacrificateurs qui composaient les parfums avec les aromates.
Lakini baadhi ya makuhani walifanya kazi ya kuchanganya vikolezo.
31 Et Matthithia, d’entre les Lévites, premier-né de Shallum, le Corite, avait la charge de l’ouvrage des [gâteaux] cuits sur la plaque;
Mlawi aliyeitwa Matithia, mwana mzaliwa wa kwanza wa Shalumu, wa ukoo wa Kora, alikabidhiwa wajibu kwa ajili ya kuoka mikate ya sadaka.
32 et des fils des Kehathites, d’entre leurs frères, [étaient chargés] des pains à placer en rangées, pour les apprêter chaque sabbat.
Baadhi ya ndugu zao wa ukoo wa Kohathi walikuwa viongozi wa kuandaa mikate ya Wonyesho kwa ajili ya kila Sabato, mikate iliyokuwa inawekwa mezani.
33 Et ce sont là les chantres, chefs des pères des Lévites, qui étaient dans les chambres, étant exempts d’autres fonctions, parce que, jour et nuit, ils étaient à l’œuvre.
Wale waliokuwa waimbaji, viongozi wa jamaa za Walawi, waliishi katika vyumba vya Hekalu, nao hawakufanya shughuli nyingine yoyote kwa sababu iliwapasa kuwajibika kwa kazi hiyo usiku na mchana.
34 Ce sont les chefs des pères des Lévites, selon leurs générations, des chefs; ceux-là habitèrent à Jérusalem.
Hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa za Walawi, wakuu kama walivyoorodheshwa katika koo zao, nao waliishi Yerusalemu.
35 Et à Gabaon habita le père de Gabaon, Jehiel; et le nom de sa femme était Maaca.
Yeieli alikuwa baba yake Gibeoni naye aliishi huko Gibeoni. Mke wake aliitwa Maaka,
36 Et son fils premier-né: Abdon; et Tsur, et Kis, et Baal, et Ner, et Nadab,
mwanawe mzaliwa wa kwanza alikuwa Abdoni, akafuatiwa na Suri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu,
37 et Guedor, et Akhio, et Zacharie, et Mikloth.
Gedori, Ahio, Zekaria na Miklothi.
38 Et Mikloth engendra Shimeam. Et eux aussi habitèrent à côté de leurs frères à Jérusalem, avec leurs frères.
Miklothi akamzaa Shimeamu. Wao pia waliishi karibu na jamaa zao huko Yerusalemu.
39 – Et Ner engendra Kis; et Kis engendra Saül; et Saül engendra Jonathan, et Malki-Shua, et Abinadab, et Eshbaal.
Neri akamzaa Kishi, Kishi akamzaa Sauli. Sauli akamzaa Yonathani, Malki-Shua, Abinadabu na Esh-Baali.
40 – Et le fils de Jonathan fut Merib-Baal; et Merib-Baal engendra Michée.
Yonathani akamzaa Merib-Baali, naye Merib-Baali akamzaa Mika.
41 Et les fils de Michée: Pithon, et Mélec, et Thakhréa.
Wana wa Mika walikuwa: Pithoni, Meleki, Tarea, na Ahazi.
42 – Et Achaz engendra Jahra; et Jahra engendra Alémeth, et Azmaveth, et Zimri. Et Zimri engendra Motsa;
Ahazi akamzaa Yara, Yara akawazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri, naye Zimri akamzaa Mosa.
43 et Motsa engendra Binha: et Rephaïa, son fils; Elhasça, son fils; Atsel, son fils.
Mosa akamzaa Binea, Binea akamzaa Refaya, na mwanawe huyo ni Eleasa, na mwanawe huyo ni Aseli.
44 Et Atsel eut six fils, et ce sont ici leurs noms: Azrikam, Bocru, et Ismaël, et Shearia, et Abdias, et Hanan; ce furent là les fils d’Atsel.
Aseli alikuwa na wana sita, na haya ndiyo majina yao: Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hanani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Aseli.

< 1 Chroniques 9 >