< 1 Chroniques 23 >

1 Et David était vieux et rassasié de jours, et il établit Salomon, son fils, roi sur Israël.
Daudi alipokuwa mzee aliyeshiba siku, akamfanya Solomoni mwanawe kuwa mfalme juu ya Israeli.
2 Et il assembla tous les chefs d’Israël, et les sacrificateurs, et les Lévites.
Pia akawakusanya pamoja viongozi wote wa Israeli, pamoja na makuhani na Walawi.
3 Et on dénombra les Lévites, depuis l’âge de 30 ans et au-dessus; et leur nombre, par tête, par homme, fut de 38 000.
Walawi waliokuwa na umri wa miaka thelathini au zaidi walihesabiwa, nayo hesabu ya wanaume ilikuwa 38,000.
4 Il y en eut d’entre eux 24 000 pour diriger l’œuvre de la maison de l’Éternel, et 6 000 intendants et juges,
Daudi akasema, “Miongoni mwa hawa, 24,000 watasimamia kazi ya Hekalu la Bwana na 6,000 watakuwa maafisa na waamuzi,
5 et 4 000 portiers, et 4 000 qui louaient l’Éternel avec les instruments, que j’ai faits, [dit David, ] pour louer.
na 4,000 watakuwa mabawabu, na wengine 4,000 watamsifu Bwana kwa ala za uimbaji nilizotoa kwa ajili ya kusudi hilo.”
6 Et David les distribua en classes d’après les fils de Lévi, Guershon, Kehath, et Merari.
Daudi akawagawa Walawi katika makundi kufuatana na wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
7 Des Guershonites: Lahdan et Shimhi.
Wana wa Wagershoni walikuwa wawili: Ladani na Shimei.
8 Les fils de Lahdan: Jekhiel, le premier, et Zétham, et Joël, trois.
Wana wa Ladani walikuwa watatu: Yehieli wa kwanza, Zethamu na Yoeli.
9 Les fils de Shimhi: Shelomith, et Haziel, et Haran, trois. Ce sont les chefs des pères de Lahdan.
Wana wa Shimei walikuwa watatu: Shelomothi, Hazieli na Harani. Hawa watatu walikuwa viongozi wa jamaa za Ladani.
10 Et les fils de Shimhi: Jakhath, Ziza, et Jehush, et Beriha: ce sont les quatre fils de Shimhi.
Nao wana wa Shimei walikuwa wanne: Yahathi, Zina, Yeushi na Beria.
11 Et Jakhath était le chef, et Ziza, le second. Mais Jehush et Beriha n’eurent pas beaucoup de fils; et, par maison de père, ils furent comptés pour une seule classe.
Yahathi alikuwa wa kwanza na Ziza wa pili, lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi; kwa hiyo walihesabiwa kama jamaa moja, wakapewa wajibu kwa pamoja.
12 Les fils de Kehath: Amram, Jitsehar, Hébron, et Uziel, quatre.
Wana wa Kohathi walikuwa wanne: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
13 Les fils d’Amram: Aaron et Moïse; et Aaron fut séparé pour qu’il soit sanctifié comme très saint, lui et ses fils, à toujours, pour faire fumer [ce qui se brûle] devant l’Éternel, pour faire son service, et pour bénir en son nom, à toujours.
Wana wa Amramu walikuwa: Aroni na Mose. Aroni waliwekwa wakfu, yeye na wazao wake milele, wawe wakiweka wakfu vitu ambavyo ni vitakatifu mno, kutoa dhabihu mbele za Bwana, kuhudumu mbele zake na kutamka baraka katika Jina la Bwana milele.
14 – Et quant à Moïse, homme de Dieu, ses fils furent attribués à la tribu de Lévi.
Wana wa Mose mtu wa Mungu walihesabiwa kama sehemu ya kabila la Lawi.
15 Fils de Moïse: Guershom et Éliézer.
Wana wa Mose walikuwa: Gershomu na Eliezeri.
16 Fils de Guershom: Shebuel, le chef.
Wazao wa Gershomu: Shebueli alikuwa wa kwanza.
17 Et les fils d’Éliézer étaient: Rekhabia, le chef; et Éliézer n’eut pas d’autres fils; mais les fils de Rekhabia furent très nombreux.
Wazao wa Eliezeri: Rehabia alikuwa wa kwanza. Eliezeri alikuwa na mwana mmoja tu, lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana.
18 – Fils de Jitsehar: Shelomith, le chef.
Wana wa Ishari: Shelomithi alikuwa wa kwanza.
19 Fils de Hébron: Jerija, le chef; Amaria, le second; Jakhaziel, le troisième; et Jekamham, le quatrième.
Wana wa Hebroni walikuwa: Yeria alikuwa wa kwanza, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli, na wa nne Yekameamu.
20 Fils d’Uziel: Michée, le chef, et Jishija, le second.
Wana wa Uzieli walikuwa: Mika wa kwanza na Ishia wa pili.
21 Les fils de Merari: Makhli et Mushi. Fils de Makhli: Éléazar et Kis.
Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Wana wa Mahli walikuwa: Eleazari na Kishi.
22 Et Éléazar mourut, et n’eut point de fils, mais des filles; et les fils de Kis, leurs frères, les prirent [pour femmes].
Eleazari akafa bila ya kuwa na wana: alikuwa na binti tu. Binamu zao, wana wa Kishi, wakawaoa.
23 Fils de Mushi: Makhli, et Éder, et Jerémoth, trois.
Wana wa Mushi: Mahli, Ederi na Yeremothi; wote walikuwa watatu.
24 Ce sont là les fils de Lévi, selon leurs maisons de pères, les chefs des pères, selon qu’ils furent recensés, en comptant les noms par tête; ils faisaient l’œuvre du service de la maison de l’Éternel, depuis l’âge de 20 ans, et au-dessus;
Hawa walikuwa wazao wa Lawi kwa jamaa zao. Wakuu wa jamaa kama walivyoandikwa kwa majina yao na kuhesabiwa kila mmoja, yaani, wenye uwezo wa kufanya kazi kuanzia miaka ishirini au zaidi, waliohudumu katika Hekalu la Bwana.
25 car David dit: L’Éternel, le Dieu d’Israël, a donné du repos à son peuple, et il demeurera à Jérusalem pour toujours;
Kwa maana Daudi alikuwa amesema, “Kwa vile Bwana, Mungu wa Israeli amewapa watu wake raha na amekuja kuishi Yerusalemu milele,
26 et les Lévites aussi n’auront plus à porter le tabernacle, ni tous les ustensiles pour son service.
Walawi hawahitaji tena kubeba Maskani wala chombo chochote cha utumishi wake.”
27 Car c’est selon les dernières paroles de David que se fit le dénombrement des fils de Lévi, depuis l’âge de 20 ans et au-dessus.
Kulingana na maagizo ya mwisho ya Daudi, Walawi waliohesabiwa ni wale wa kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi.
28 Car leur place était à côté des fils d’Aaron pour le service de la maison de l’Éternel, [pour veiller] sur les parvis et les chambres, et sur la purification de toutes les choses saintes, et sur l’œuvre du service de la maison de Dieu:
Wajibu wa Walawi ulikuwa kuwasaidia wazao wa Aroni kuhudumu katika Hekalu la Bwana: Kuwa wasimamizi wa nyua, vyumba vya pembeni, kutakasa vyombo vitakatifu na utendaji mwingine wowote katika nyumba ya Mungu.
29 pour les pains à placer en rangées, et la fleur de farine pour le gâteau et les galettes sans levain, et [ce qui se cuit sur] la plaque, et ce qui est mêlé [avec de l’huile], et toutes les mesures de capacité et de longueur;
Walikuwa wasimamizi wa mikate iliyowekwa mezani, unga kwa ajili ya sadaka za nafaka, mikate isiyotiwa chachu, uokaji na uchanganyaji, pamoja na vipimo vyote vya wingi na ukubwa.
30 et pour se tenir là chaque matin, afin de célébrer et de louer l’Éternel, et de même chaque soir;
Pia ulikuwa wajibu wao kila asubuhi kumshukuru na kumsifu Bwana. Iliwapasa pia kufanya hivyo jioni
31 et [pour être de service] pour tous les holocaustes qu’on offrait à l’Éternel, aux sabbats, aux nouvelles lunes, et aux jours solennels, en nombre, conformément à l’ordonnance à leur égard, continuellement, devant l’Éternel.
na wakati wowote sadaka za kuteketezwa zilipotolewa kwa Bwana siku za Sabato na kwenye sikukuu za Mwezi Mwandamo na katika sikukuu nyingine zilizoamriwa. Iliwapasa kuhudumu mbele za Bwana mara kwa mara kwa idadi maalum na kwa namna waliyokuwa wamepewa maelekezo.
32 Et ils vaquaient à leur charge à l’égard de la tente d’assignation, et à leur charge à l’égard du lieu saint, et à leur charge à l’égard des fils d’Aaron, leurs frères, pour le service de la maison de l’Éternel.
Hivyo Walawi wakafanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, katika Mahali Patakatifu chini ya uongozi wa ndugu zao wazao wa Aroni, kwa ajili ya utumishi katika Hekalu la Bwana.

< 1 Chroniques 23 >