< 1 Chroniques 18 >

1 Et il arriva, après cela, que David frappa les Philistins et les subjugua, et prit Gath et les villes de son ressort de la main des Philistins.
Baada ya haya Daudi akawashambulia Wafilisti na kuwashinda. Alichukuwa Gathi na vijiji vyake katika utawala wa Wafilisti.
2 Et il frappa Moab, et les Moabites devinrent serviteurs de David: ils lui apportèrent des présents.
Kisha akamshinda Moabu, na Wamoabu wakawa watumishi wa Daudi na wakamlipa ushuru maalumu.
3 Et David frappa Hadarézer, roi de Tsoba, à Hamath, comme il allait pour établir sa puissance sur le fleuve Euphrate.
Daudi kisha akamshinda Hadadezeri, mfalme wa Zoba huko Hamathi, wakati Hadadezeri alipo kuwa akisafiri kuimarisha utawala wake kwa Mto wa Frati.
4 Et David lui prit 1 000 chars, et 7 000 cavaliers, et 20 000 hommes de pied; et David coupa les jarrets [aux chevaux] de tous les chars, mais il réserva 100 attelages.
Daudi akateka magari ya farasi elfu, wanaume wa farasi elfu saba, na wanajeshi wa miguu elfu ishirini. Daudi aliwajeruhi farasi wote wagari, lakini akahifadhi baadhi kwa ajili ya magari ya farasi mia moja.
5 Et les Syriens de Damas vinrent au secours d’Hadarézer, roi de Tsoba; et David frappa 22 000 hommes des Syriens.
Waaramia wa Damasko walipo kuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Zoba, Daudi aliua wanaume elfu ishirini na mbili wa Kiaramia.
6 Et David mit [des garnisons] dans la Syrie de Damas, et les Syriens devinrent serviteurs de David: ils lui apportèrent des présents. Et l’Éternel sauvait David partout où il allait.
Kisha Daudi akaweka vikosi huko Aramu ya Damasko, na Waaramia wakawa watumishi wake na wakamletea ushuru maalaumu. Yahweh alimpatia Daudi ushindi popote alipoenda.
7 Et David prit les boucliers d’or qui étaient aux serviteurs d’Hadarézer, et les apporta à Jérusalem.
Daudi alichukua ngao za dhahabu zilizo kuwa kwa watumishi wa Hadadezeri na kuleta Yerusalemu.
8 Et de Tibkhath et de Cun, villes d’Hadarézer, David prit une grande quantité d’airain, dont Salomon fit la mer d’airain, et les colonnes, et les vases d’airain.
Kutoka Tibhathi na Kuni, miji ya Hadadezeri, Daudi alichukuwa shaba nyingi sana. Ilikuwa shaba hii ambayo baadae Sulemani alifanya saani ya shaba, nguzo, na vifaa vya shaba.
9 Et Tohu, roi de Hamath, apprit que David avait frappé toutes les forces d’Hadarézer, roi de Tsoba;
Wakati Toi, mfalme wa Hamathi, alipo sikia kuwa Daudi ameshinda majeshi yote ya Hadadezeri mfalme wa Zoba,
10 et il envoya Hadoram, son fils, au roi David, pour le saluer et le féliciter de ce qu’il avait fait la guerre à Hadarézer et l’avait battu; car Hadarézer était continuellement en guerre avec Tohu; [il envoya] aussi toutes sortes de vases d’or, et d’argent, et d’airain.
Toi akamtuma Hadoramu mwanae kwa Mfalme Daudi kumsalimia na kumbariki, kwasababu Daudi amepigana na Hadadezeri na kumshinda, na kwasababu Hadadezeri alifanya vita na Toi. Hadoramu alipeleka vifaa vya fedha, dhahabu, na shaba.
11 Ceux-ci aussi, le roi David les consacra à l’Éternel, avec l’argent et l’or qu’il avait emportés de toutes les nations, d’Édom, et de Moab, et des fils d’Ammon, et des Philistins, et d’Amalek.
Mfalme Daudi alivitenga hivi vitu kwa ajili ya Yahweh, pamoja na fedha na dhahabu aliyo ibeba kutoka kwa mataifa yote: Edomu, Moabu, watu wa Amoni, Wafilisti, na Waamaleki.
12 Et Abishaï, fils de Tseruïa, frappa dans la vallée du Sel 18 000 [hommes] d’Édom;
Abishai mwana wa Zeruia akawaua Waedomi elfu kumi na nane katika Bonde la Chumvi.
13 et il mit des garnisons en Édom, et tout Édom fut asservi à David. Et l’Éternel sauvait David partout où il allait.
Alieka vikosi huko Edomu, na Waedomi wote wakawa watumishi wa Daudi. Yahweh alimpa Daudi ushindi pote alipoenda.
14 Et David régna sur tout Israël, et il faisait droit et justice à tout son peuple.
Daudi alitawala Israeli yote, na alitenda haki na utaua kwa watu wote.
15 Et Joab, fils de Tseruïa, était [préposé] sur l’armée; et Josaphat, fils d’Akhilud, était rédacteur des chroniques;
Yoabu mwana wa Zeruia walikuwa mkuu wa jeshi, na Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mtunza kumbukumbu.
16 et Tsadok, fils d’Akhitub, et Abimélec, fils d’Abiathar, étaient sacrificateurs; et Shavsha était scribe;
Zadoki mwana wa Ahitubi na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani, na Shavisha alikuwa mwandishi.
17 et Benaïa, fils de Jehoïada, était [préposé] sur les Keréthiens et les Peléthiens; et les fils de David étaient les premiers à côté du roi.
Benaia mwana wa Yehoiada alikuwa mwangalizi wa Wakerethi na Wapelethi, na wana wa Daudi walikuwa washauri wakuu wa mfalme.

< 1 Chroniques 18 >