< Psaumes 26 >

1 De David. Rends-moi justice, Yahweh, car j’ai marché dans mon innocence; je me confie en Yahweh, je ne chancellerai pas.
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
2 Éprouve-moi, Yahweh, sonde-moi, fais passer au creuset mes reins et mon cœur:
Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
3 car ta miséricorde est devant mes yeux, et je marche dans ta vérité.
kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
4 Je ne me suis pas assis avec les hommes de mensonge, je ne vais pas avec les hommes dissimulés;
Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
5 Je hais l’assemblée de ceux qui font le mal, je ne siège pas avec les méchants.
ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
6 Je lave mes mains dans l’innocence, et j’entoure ton autel, Yahweh,
Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
7 pour faire entendre une voix de louange; et raconter toutes tes merveilles.
nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
8 Yahweh, j’aime le séjour de ta maison, le lieu où ta gloire réside.
Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
9 N’enlève pas mon âme avec celle des pécheurs, ma vie avec celle des hommes de sang,
Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
10 qui ont le crime dans les mains, et dont la droite est pleine de présents.
ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
11 Pour moi, je marche en mon innocence: délivre-moi et aie pitié de moi!
Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
12 Mon pied se tient sur un sol uni: je bénirai Yahweh dans les assemblées.
Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.

< Psaumes 26 >