< Lévitique 21 >

1 Yahweh dit à Moïse: « Parle aux prêtres, fils d’Aaron, et dis-leur: Nul ne se rendra impur au milieu de son peuple pour un mort,
Bwana akamwambia Mose, “Sema na makuhani, wana wa Aroni, uwaambie: ‘Kamwe kuhani asijitie unajisi kwa utaratibu wa kiibada kwa ajili ya mtu wake yeyote anayekufa,
2 excepté pour son parent du même rang, pour sa mère, pour son père, pour son fils, pour sa fille, pour son frère,
isipokuwa jamaa wake wa karibu, kama vile mama yake au baba yake, mwanawe au binti yake, ndugu yake,
3 et pour sa sœur vierge, qui vit auprès de lui, n’étant pas encore mariée; pour elle il se rendra impur.
au dada yake asiyeolewa ambaye anamtegemea kwa kuwa hana mume, kwa ajili ya hao aweza kujitia unajisi.
4 Chef de maison parmi son peuple, il ne se souillera pas et ne profanera pas sa dignité.
Kamwe asijitie unajisi mwenyewe kutokana na wale watu ambao anahusiana nao kwa kuoana, na hivyo kujitia unajisi.
5 Les prêtres ne se raseront pas la tête, ils n’enlèveront pas les côtés de leur barbe, et ils ne feront pas d’incisions dans leur chair.
“‘Kamwe makuhani wasinyoe nywele za vichwa vyao wala wasinyoe pembeni mwa ndevu zao, au kuweka chale kwenye miili yao.
6 Ils seront saints pour leur Dieu, et ils ne profaneront pas le nom de leur Dieu, car ils offrent à Yahweh des sacrifices consumés par le feu, le pain de leur Dieu: ils seront saints.
Lazima wawe watakatifu kwa Mungu wao, na kamwe wasilinajisi jina la Mungu wao. Kwa sababu ndio wanaotoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Bwana, chakula cha Mungu wao, hivyo lazima wawe watakatifu.
7 Ils ne prendront point une femme prostituée ou déshonorée; ils ne prendront point une femme répudiée par son mari, car le prêtre est saint pour son Dieu.
“‘Kamwe wasioe wanawake waliojinajisi kwa ukahaba, au waliopewa talaka na waume wao, kwa sababu makuhani ni watakatifu kwa Mungu wao.
8 Tu le tiendras pour saint, car il offre le pain de ton Dieu; il sera saint pour toi, car je suis saint, moi Yahweh, qui vous sanctifie.
Waoneni kuwa watakatifu, kwa sababu ndio wanaotoa chakula cha Mungu wenu. Kumbukeni kuwa ni watakatifu, kwa sababu Mimi Bwana ni mtakatifu, Mimi niwafanyaye ninyi kuwa watakatifu.
9 Si la fille d’un prêtre se déshonore en se prostituant, elle déshonore son père: elle sera brûlée au feu.
“‘Ikiwa binti wa kuhani anajitia unajisi kwa kufanya ukahaba, anamwaibisha baba yake; lazima achomwe kwa moto.
10 Le grand prêtre qui est au-dessus de ses frères, sur la tête duquel a été répandue l’huile d’onction, et qui a été installé pour revêtir les vêtements sacrés, ne découvrira pas sa tête et ne déchirera pas ses vêtements.
“‘Kuhani mkuu, yule miongoni mwa ndugu zake ambaye amekwisha kutiwa mafuta kwa kumiminiwa juu ya kichwa chake, na ambaye amewekwa wakfu kuvaa mavazi ya ukuhani, kamwe asiache nywele zake bila kufunikwa, wala asirarue nguo zake.
11 Il n’approchera d’aucun mort; il ne se rendra impur ni pour son père, ni pour sa mère.
Kamwe asiingie mahali palipo maiti ndani. Kamwe asijitie unajisi, hata kwa ajili ya baba yake au mama yake,
12 Il ne sortira pas du sanctuaire, et ne profanera pas le sanctuaire de son Dieu, car l’huile d’onction de son Dieu est un diadème sur lui. Je suis Yahweh.
wala asiondoke mahali patakatifu pa Mungu wake au kupanajisi, kwa sababu amewekwa wakfu kwa mafuta ya Mungu wake. Mimi ndimi Bwana.
13 Il prendra pour femme une vierge.
“‘Mwanamke kuhani atakayemwoa lazima awe bikira.
14 Il ne prendra ni une veuve, ni une femme répudiée, ni une femme déshonorée ou prostituée; mais il prendra pour femme une vierge du milieu de son peuple.
Kamwe asimwoe mjane, au mwanamke aliyepewa talaka, wala mwanamke aliyejinajisi kwa ukahaba, bali atamwoa tu bikira kutoka miongoni mwa watu wake,
15 Il ne déshonorera pas sa postérité au milieu de son peuple; car je suis Yahweh, qui le sanctifie. »
na hivyo hatawatia unajisi watoto wake miongoni mwa watu wake. Mimi ndimi Bwana, nimfanyaye mtakatifu.’”
16 Yahweh parla à Moïse, en disant:
Bwana akamwambia Mose,
17 « Parle à Aaron, et dis- lui: Nul homme de ta race, dans toutes les générations, qui aura une difformité corporelle, n’approchera pour offrir le pain de ton Dieu.
“Mwambie Aroni: ‘Kwa vizazi vijavyo, hakuna mzao wako mwenye dosari atakayekaribia kutoa chakula cha Mungu wake.
18 Car nul homme qui a une difformité corporelle n’approchera: un homme aveugle ou boiteux, ou qui aura une mutilation ou une excroissance;
Hakuna mtu mwenye dosari yoyote awezaye kukaribia: hakuna mtu aliye kipofu au kiwete, au aliyeharibika uso au asiye na viungo kamili,
19 ou un homme qui aura une fracture au pied ou à la main;
hakuna mtu mwenye mguu au mkono uliolemaa,
20 qui sera bossu ou nain, ou qui aura une tache à l’œil, la gale, une dartre ou les testicules écrasés.
au mwenye kibiongo au aliyedumaa, au aliye na tatizo la macho, au aliye na uvimbe wenye usaha au majipu, au aliyehasiwa.
21 Nul homme de la race du prêtre Aaron qui aura une difformité corporelle, ne s’approchera pour offrir à Yahweh les sacrifices faits par le feu; il a une difformité corporelle: qu’il ne s’approche point pour offrir le pain de son Dieu.
Hakuna mzao wa kuhani Aroni mwenye kilema chochote atakayekaribia kutoa sadaka kwa Bwana ya kuteketezwa kwa moto. Kama ana kilema, kamwe asikaribie kutoa chakula cha Mungu wake.
22 Il pourra manger le pain de son Dieu, des choses très saintes et des choses saintes.
Anaweza kula chakula kitakatifu sana cha Mungu wake, pia hata chakula kitakatifu.
23 Mais il n’ira point vers le voile et ne s’approchera point de l’autel, car il a une difformité corporelle; il ne profanera point mes sanctuaires, car je suis Yahweh; qui les sanctifie. »
Lakini kwa sababu ya kilema chake, kamwe asikaribie karibu na pazia wala kukaribia madhabahu, asije akanajisi mahali patakatifu pangu. Mimi ndimi Bwana, niwafanyaye watakatifu.’”
24 Ainsi parla Moïse à Aaron et à ses fils, et à tous les enfants d’Israël.
Basi Mose akamwambia Aroni jambo hili na wanawe, pamoja na Waisraeli wote.

< Lévitique 21 >