< Lévitique 16 >

1 Yahweh parla à Moïse, après la mort des deux fils d’Aaron, qui furent frappés lorsqu’ils s’approchèrent de la face de Yahweh.
Bwana akasema na Mose baada ya kifo cha wale wana wawili wa Aroni waliokufa walipokaribia mbele za Bwana.
2 Yahweh dit à Moïse: « Parle à ton frère Aaron, afin qu’il n’entre pas en tout temps dans le sanctuaire, au-dedans du voile, devant le propitiatoire qui est sur l’arche, de peur qu’il ne meure; car j’apparais dans la nuée sur le propitiatoire.
Bwana akamwambia Mose: “Mwambie ndugu yako Aroni asije wakati wowote atakavyo yeye ndani ya Patakatifu pa Patakatifu, nyuma ya pazia pale mbele ya kiti cha rehema kile kilichoko juu ya Sanduku la Agano, la sivyo atakufa, kwa sababu huwa ninatokea ndani ya wingu juu ya kile kiti cha rehema.
3 Voici le rite suivant lequel Aaron entrera dans le sanctuaire. Il prendra un jeune taureau pour le sacrifice pour le péché et un bélier pour l’holocauste.
“Hivi ndivyo Aroni atakavyoingia katika mahali patakatifu: atachukua fahali mchanga kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.
4 Il se revêtira de la sainte tunique de lin et mettra sur sa chair des caleçons de lin; il se ceindra d’une ceinture de lin et se couvrira la tête d’une tiare de lin: ce sont les vêtements sacrés qu’il revêtira, après avoir baigné son corps dans l’eau.
Atavaa koti takatifu la kitani, pamoja na nguo za ndani za kitani; atafunga mshipi wa kitani kiunoni, na kuvaa kilemba cha kitani. Haya ni mavazi matakatifu, kwa hiyo ni lazima aoge kwa maji kabla ya kuyavaa mavazi hayo.
5 Il recevra de l’assemblée des enfants d’Israël deux boucs pour le sacrifice pour le péché, et un bélier pour l’holocauste.
Atachukua mbuzi dume wawili kutoka kwa jumuiya ya Israeli kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.
6 Aaron offrira son taureau pour le péché, et il fera l’expiation pour lui et pour sa maison.
“Aroni atamtoa huyo fahali kwa ajili ya sadaka yake ya dhambi ili afanye upatanisho kwa ajili yake mwenyewe na nyumba yake.
7 Puis il prendra les deux boucs et, les placera devant Yahweh, à l’entrée de la tente de réunion.
Kisha atawachukua wale mbuzi dume wawili na kuwaleta mbele za Bwana kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
8 Aaron jettera le sort sur les deux boucs, un sort pour Yahweh et un sort pour Azazel.
Aroni atapiga kura kwa ajili ya hao mbuzi wawili, mmoja kwa ajili ya Bwana na mwingine kwa ajili ya kubebeshwa dhambi.
9 Aaron fera approcher le bouc sur lequel sera tombé le sort pour Yahweh et l’offrira en sacrifice pour le péché.
Aroni atamleta yule mbuzi ambaye kura ya Bwana imemwangukia na kumtoa dhabihu kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
10 Et le bouc sur lequel sera tombé le sort pour Azazel, il le placera vivant devant Yahweh, afin de faire l’expiation sur lui et de le lâcher dans le désert pour Azazel.
Lakini mbuzi aliyechaguliwa kwa kura kuwa wa kubebeshwa dhambi atatolewa akiwa hai mbele za Bwana, atumike kwa kufanya upatanisho kwa kumwacha aende jangwani akiwa amebebeshwa dhambi.
11 Aaron offrira donc le taureau du sacrifice pour le péché qui est pour lui, et il fera l’expiation pour lui et pour sa maison. Après avoir égorgé son taureau pour le péché,
“Aroni atamleta yule fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi yake mwenyewe, ili kufanya upatanisho kwa ajili yake na nyumba yake, naye atamchinja huyo fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi yake mwenyewe.
12 il prendra un encensoir plein de charbons ardents de dessus l’autel, de devant Yahweh, et deux poignées de parfum odoriférant en poudre; et ayant porté ces choses au-delà du voile,
Atachukua chetezo kilichojaa makaa yanayowaka kutoka madhabahuni mbele za Bwana, na konzi mbili za uvumba laini uliosagwa vizuri wenye harufu, na kuvipeleka nyuma ya pazia.
13 il mettra le parfum sur le feu devant Yahweh, afin que la nuée du parfum couvre le propitiatoire qui est sur le témoignage, et qu’il ne meure pas.
Ataweka uvumba juu ya moto mbele za Bwana, na moshi wa uvumba utafunika kile kiti cha rehema kilicho juu ya Ushuhuda, ili asife.
14 Il prendra du sang du taureau, et en fera aspersion avec son doigt sur la face orientale du propitiatoire, et il fera avec son doigt sept fois aspersion du sang devant le propitiatoire.
Atachukua sehemu ya damu ya fahali, na kwa kidole chake atanyunyiza sehemu ya mbele ya kiti cha rehema; kisha atanyunyiza sehemu ya hiyo damu kwa kidole chake mara saba mbele ya kiti cha rehema.
15 Il égorgera le bouc du sacrifice pour le péché qui est pour le peuple, et il en portera le sang au delà du voile et, faisant de ce sang comme il a fait du sang du taureau, il en fera l’aspersion une fois sur le propitiatoire et sept fois devant le propitiatoire.
“Kisha atamchinja mbuzi wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya watu, na kuichukua damu yake nyuma ya pazia, na aifanyie kama alivyofanya kwa damu ya fahali: Atanyunyiza juu ya kiti cha rehema na mbele yake.
16 C’est ainsi qu’il fera l’expiation pour le sanctuaire à cause des souillures des enfants d’Israël et de toutes leurs transgressions, selon qu’ils ont péché. Il fera de même pour la tente de réunion, qui demeure avec eux au milieu de leurs souillures.
Kwa njia hii atafanya upatanisho kwa ajili ya Patakatifu pa Patakatifu kwa sababu ya unajisi na uasi wa Waisraeli, kwa dhambi zao zozote. Atafanya hivyo kwa ajili ya Hema la Kukutania, ambalo liko miongoni mwao katikati ya unajisi wao.
17 Qu’il n’y ait personne dans la tente de réunion lorsqu’il entrera pour faire l’expiation dans le sanctuaire, jusqu’à ce qu’il en sorte. Il fera l’expiation pour lui, pour sa maison et pour toute l’assemblée d’Israël.
Mtu yeyote haruhusiwi kuwa ndani ya Hema la Kukutania, kuanzia wakati Aroni anapoingia kufanya upatanisho katika Patakatifu pa Patakatifu, hadi atakapotoka nje, baada ya kujifanyia upatanisho yeye mwenyewe na nyumba yake, pamoja na jumuiya yote ya Israeli.
18 Il ira en sortant vers l’autel qui est devant Yahweh, et fera l’expiation pour l’autel: ayant pris du sang du taureau et du sang du bouc, il en mettra sur les cornes de l’autel tout autour.
“Kisha atatoka aje kwenye madhabahu yaliyo mbele za Bwana na kufanya upatanisho kwa ajili yake. Atachukua sehemu ya damu ya fahali na sehemu ya damu ya mbuzi, na kuiweka kwenye pembe za madhabahu.
19 Il fera sur l’autel, avec son doigt, sept fois aspersion du sang; il le purifiera et le sanctifiera des souillures des enfants d’Israël.
Atanyunyiza baadhi ya hiyo damu juu ya madhabahu kwa kidole chake mara saba, ili kuitakasa na kuiweka wakfu kutokana na unajisi wa Waisraeli.
20 Lorsqu’il aura achevé de faire l’expiation pour le sanctuaire, pour la tente de réunion et pour l’autel, il présentera le bouc vivant.
“Aroni atakapokuwa amemaliza kufanya upatanisho kwa ajili ya Patakatifu pa Patakatifu, Hema la Kukutania na madhabahu, atamleta mbele yule mbuzi aliye hai.
21 Ayant posé ses deux mains sur la tête du bouc vivant, Aaron confessera sur lui toutes les iniquités des enfants d’Israël et toutes leurs transgressions, selon qu’ils ont péché; il les mettra sur la tête du bouc et il l’enverra ensuite au désert par un homme tout prêt.
Aroni ataweka mikono yake miwili juu ya kichwa cha mbuzi aliye hai na kuungama juu yake uovu wote na uasi wa Waisraeli, yaani dhambi zao zote, ili kuziweka juu ya kichwa cha huyo mbuzi. Atamwachia huyo mbuzi akimbilie jangwani kwa uangalizi wa mtu aliyepewa wajibu huo.
22 Le bouc emportera sur lui toutes leurs iniquités dans une terre inhabitée, et l’homme lâchera le bouc dans le désert.
Yule mbuzi atachukua juu yake dhambi zao zote mpaka mahali pasipo na watu; naye yule mtu atamwachia akimbilie jangwani.
23 Alors Aaron entrera dans la tente de réunion; il quittera les vêtements de lin qu’il avait revêtus pour entrer dans le sanctuaire et, les ayant déposés là,
“Kisha Aroni ataenda ndani ya Hema la Kukutania na kuvua yale mavazi ya kitani aliyoyavaa kabla ya kuingia katika Patakatifu pa Patakatifu, naye atayaacha pale.
24 il baignera son corps dans l’eau en un lieu saint et reprendra ses vêtements.
Ataoga kwa maji katika mahali patakatifu na kuvaa mavazi yake ya kawaida. Kisha atatoka na kutoa dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yake na sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya watu, ili kufanya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe, na kwa ajili ya watu.
25 Il sortira ensuite, offrira son holocauste et celui du peuple, fera l’expiation pour lui et pour le peuple, et fera fumer sur l’autel la graisse du sacrifice pour le péché.
Pia atachoma mafuta ya mnyama wa sadaka ya dhambi juu ya madhabahu.
26 Celui qui aura lâché le bouc pour Azazel lavera ses vêtements et baignera son corps dans l’eau; après quoi, il rentrera dans le camp.
“Yule mtu anayemwachia yule mbuzi wa kubebeshwa dhambi ni lazima afue nguo zake na kuoga kwa maji; baadaye anaweza kuingia kambini.
27 On emportera hors du camp le taureau pour le péché et le bouc pour le péché, dont le sang aura été porté dans le sanctuaire pour faire l’expiation, et l’on consumera par le feu leur peau, leur chair et leurs excréments.
Yule fahali na mbuzi waliotolewa kwa ajili ya sadaka za dhambi, ambao damu yao ilikuwa imeletwa Patakatifu pa Patakatifu kwa ajili ya kufanya upatanisho, ni lazima watolewe nje ya kambi. Ngozi zao, nyama, na matumbo pamoja na mavi vitateketezwa kwa moto.
28 Celui qui les aura brûlés lavera ses vêtements et baignera son corps dans l’eau; après quoi, il rentrera dans le camp.
Mtu atakayevichoma ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji; baadaye ataweza kuingia kambini.
29 Ceci sera pour vous une loi perpétuelle: au septième mois, le dixième jour du mois, vous affligerez vos âmes et ne ferez aucun ouvrage, ni l’indigène, ni l’étranger qui séjourne au milieu de vous.
“Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu: Katika siku ya kumi ya mwezi wa saba ni lazima mfunge, wala msifanye kazi yoyote, iwe mzawa au mgeni anayeishi miongoni mwenu,
30 Car en ce jour on fera l’expiation pour vous, afin de vous purifier; vous serez purs de tous vos péchés devant Yahweh.
kwa sababu siku hii upatanisho utafanyika kwa ajili yenu ili kuwatakasa. Kisha mtakuwa safi mbele za Bwana kutokana na dhambi zenu zote.
31 Ce sera pour vous un sabbat, un jour de repos, et vous affligerez vos âmes. C’est une loi perpétuelle.
Ni Sabato ya mapumziko, na lazima mfunge; ni agizo la kudumu.
32 L’expiation sera faite, dans l’avenir, par le grand prêtre qui aura reçu l’onction et qui aura été installé pour remplir les fonctions sacerdotales à la place de son père. Il revêtira des vêtements de lin, des vêtements sacrés.
Kuhani ambaye ametiwa mafuta na kuwekwa wakfu ili kuingia mahali pa baba yake kama kuhani mkuu atafanya upatanisho. Atavaa mavazi matakatifu ya kitani,
33 Il fera l’expiation pour le sanctuaire de sainteté, il fera l’expiation pour la tente de réunion et pour l’autel des holocaustes; il fera l’expiation pour les prêtres et pour tout le peuple de l’assemblée.
na kufanya upatanisho kwa ajili ya Patakatifu pa Patakatifu, Hema la Kukutania na madhabahu, na pia kwa ajili ya makuhani, pamoja na jumuiya yote ya watu.
34 Ce sera pour vous une loi perpétuelle: l’expiation se fera une fois chaque année pour les enfants d’Israël, à cause de leurs péchés. » On fit ce que Yahweh avait ordonné à Moïse.
“Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu: Upatanisho utafanywa mara moja tu kwa mwaka kwa ajili ya dhambi zote za Waisraeli.” Ndivyo ilivyofanyika, kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.

< Lévitique 16 >