< Juges 18 >
1 En ce temps-là, il n’y avait pas de roi en Israël; en ce temps-là la tribu des Danites se cherchait une possession pour s’établir, car jusqu’à ce jour il ne lui était pas échu d’héritage au milieu des tribus d’Israël.
Katika siku hizo Israeli walikuwa hawana mfalme. Katika siku hizo kabila la Wadani walikuwa wanatafuta mahali pao wenyewe pa kuishi, kwa sababu walikuwa hawajafika kwenye urithi wao miongoni mwa makabila ya Israeli.
2 Les fils de Dan, ayant pris d’entre eux tous cinq hommes de leur famille, hommes vaillants, les envoyèrent de Saraa et d’Esthaol pour explorer le pays et le reconnaître. Ils leur dirent: « Allez, reconnaissez le pays. » Les cinq hommes arrivèrent dans la montagne d’Ephraïm jusqu’à la maison de Michas, et ils y passèrent la nuit.
Hivyo Wadani wakatuma mashujaa watano kutoka Sora na Eshtaoli ili kupeleleza nchi na kuichunguza. Hawa watu waliwakilisha koo zao zote. Waliwaambia, “Nendeni mkaichunguze hiyo nchi.” Watu hao wakaingia katika nchi ya vilima ya Efraimu, nao wakafika nyumba ya Mika, ambako walilala usiku huo.
3 Comme ils étaient prés de la maison de Michas, reconnaissant la voix du jeune Lévite, ils s’approchèrent et lui dirent: « Qui t’a amené ici? Que fais-tu dans ce lieu et qu’as-tu ici? »
Walipofika karibu na nyumba ya Mika, waliitambua sauti ya yule kijana Mlawi; hivyo wakaingia humo na kumuuliza, “Ni nani aliyekuleta hapa? Unafanya nini mahali hapa? Kwa nini uko hapa?”
4 Il leur répondit: « Michas a fait pour moi telle et telle chose, il me donne un salaire, et je lui sers de prêtre. »
Akawaeleza yale Mika aliyomtendea, naye akasema, “Ameniajiri nami ni kuhani wake.”
5 Ils lui dirent: « Eh bien, consulte Dieu, afin que nous sachions si notre voyage aura du succès. »
Kisha wakamwambia, “Tafadhali tuulizie kwa Mungu kama safari yetu itafanikiwa.”
6 Et le prêtre leur répondit: « Allez en paix; le voyage que vous faites est sous le regard de Yahweh. »
Yule kuhani akawajibu, “Enendeni kwa amani. Safari yenu ina kibali cha Bwana.”
7 S’étant mis en route, les cinq hommes arrivèrent à Laïs. Ils virent le peuple qui était dans cette ville, vivant en sécurité à la manière des Sidoniens, paisible et tranquille, et il n’y avait personne dans le pays qui, investi de l’autorité, les molestât en aucune manière; ils étaient éloignés des Sidoniens, et n’avaient affaire avec personne.
Basi hao watu watano wakaondoka na kufika Laishi, mahali ambapo waliwakuta watu wanaishi salama, kama Wasidoni, kwa utulivu na bila mashaka. Nchi yao haikupungukiwa na kitu chochote, hivyo wakawa tajiri. Pia walikaa mbali sana na Wasidoni, wala hawakushughulika na mtu yeyote.
8 Ils revinrent vers leurs frères à Saraa et Esthaol, et leurs frères leur dirent: « Que dites -vous? »
Waliporudi kwa ndugu zao huko Sora na Eshtaoli, ndugu zao wakawauliza, “Mlionaje mambo huko?”
9 Ils répondirent: « Debout, et montons contre ceux; car nous avons vu le pays et voici, qu’il est très bon. Et vous restez là sans mot dire? Ne soyez point paresseux à vous mettre en marche pour aller prendre possession de ce pays.
Wakajibu, “Twendeni, tukapigane nao! Tumeona kuwa nchi ni nzuri sana. Je, hamtafanya chochote? Msisite kupanda ili kuimiliki.
10 En y entrant, vous arriverez chez un peuple en sécurité. Le pays est vaste, et Dieu l’a livré entre vos mains; c’est un lieu où rien ne manque de tout ce qu’il y a sur la terre. »
Mtakapokwenda huko mtakuta watu waliotulia walio salama, nayo nchi hiyo ni kubwa na Mungu ameitia mikononi mwenu, nayo ni nchi ambayo haikupungukiwa na kitu chochote kilicho duniani.”
11 Six cents hommes de la famille de Dan partirent de Saraa et d’Esthaol, munis de leurs armes de guerre.
Ndipo watu 600 toka ukoo wa Wadani, waliojifunga silaha za vita, wakaondoka Sora na Eshtaoli.
12 Ils montèrent et campèrent à Cariathiarim en Juda; c’est pourquoi ce lieu a été appelé jusqu’à ce jour Machanêh-Dan; voici qu’il est à l’occident de Cariathiarim.
Walipokuwa wakisafiri wakapiga kambi huko Kiriath-Yearimu katika Yuda. Hii ndiyo sababu sehemu ya magharibi ya Kiriath-Yearimu inaitwa Mahane-Dani mpaka leo.
13 Ils passèrent de là dans la montagne d’Ephraïm, et ils arrivèrent jusqu’à la maison de Michas.
Kutoka hapo wakaendelea mbele mpaka nchi ya vilima ya Efraimu na kufika katika nyumba ya Mika.
14 Les cinq hommes qui avaient été explorer le pays de Laïs prirent la parole et dirent à leurs frères: « Savez-vous qu’il y a dans ces maisons un éphod, des théraphim, une image taillée et un objet en fonte? Voyez maintenant ce que vous avez à faire. »
Ndipo wale watu watano waliopeleleza nchi ya Laishi wakawaambia ndugu zao, “Je, mwajua kuwa mojawapo ya nyumba hizi kuna naivera, sanamu ndogo za nyumbani, sanamu ya kuchonga na sanamu ya kusubu? Sasa basi fikirini mtakalofanya.”
15 Ils se dirigèrent de ce côte-là et, entrant dans la maison du jeune Lévite, la maison de Michas, ils lui demandèrent comment il se portait.
Basi wakaingia humo na kwenda kwenye nyumba ya yule kijana Mlawi katika nyumba ya Mika na kumsalimu.
16 Les six cents hommes d’entre les fils de Dan, munis de leurs armes de guerre, se tenaient à l’entrée de la porte.
Wale Wadani 600, waliovaa silaha za vita, wakasimama penye ingilio la lango.
17 Et les cinq hommes qui avaient été explorer le pays montèrent et, étant entrés dans le sanctuaire, ils prirent l’image taillée, l’éphod, les théraphim et l’objet en fonte, pendant que le prêtre était à l’entrée de la porte avec les six cents hommes munis de leurs armes de guerre.
Wale watu watano waliokwenda kupeleleza nchi wakaingia ndani na kuchukua ile sanamu ya kuchonga, ile naivera, na zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani pamoja na ile sanamu ya kusubu, wakati yule kuhani akiwa amesimama pale penye ingilio la lango pamoja na wale watu 600 waliokuwa wamejifunga silaha za vita.
18 Lorsqu’ils furent entrés dans la maison de Michas et qu’ils eurent pris l’image taillée, l’éphod, les théraphim et l’objet en fonte, le prêtre leur dit: « Que faites-vous? »
Hao watu walipoingia katika nyumba ya Mika na kuchukua ile sanamu ya kuchonga, ile naivera, na zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani, pamoja na ile sanamu ya kusubu, yule kuhani akawauliza, “Mnafanya nini?”
19 Ils lui répondirent: « Tais-toi, mets ta main sur ta bouche et viens avec nous, et tu seras pour nous un père et un prêtre. Vaut-il mieux que tu sois prêtre pour la maison d’un seul homme, ou que tu sois prêtre pour une tribu et pour une famille en Israël? »
Wakamjibu, “Nyamaza kimya! Weka mkono wako juu ya kinywa chako na ufuatane nasi, uwe baba yetu na kuhani wetu. Si ni afadhali utumikie kabila na ukoo katika Israeli kama kuhani kuliko kumtumikia mtu mmoja na watu wa nyumbani mwake?”
20 Le cœur du prêtre devint joyeux; il prit l’éphod, les théraphim et l’image taillée, et il vint au milieu de la troupe.
Yule kuhani akafurahi. Akachukua ile naivera, zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani, na sanamu ya kuchonga, naye akaenda pamoja na wale watu.
21 Ils se remirent en route et partirent, ayant placé devant eux les enfants, le bétail et toutes les choses de prix.
Ndipo wakageuka na kuondoka wakiwatanguliza mbele watoto wao wadogo, wanyama wao wa kufugwa na mali zao.
22 Ils étaient déjà loin de la maison de Michas, lorsque les gens qui habitaient les maisons voisines de la maison de Michas se rassemblèrent et poursuivirent les fils de Dan.
Walipokuwa wamesafiri umbali kidogo toka nyumbani kwa Mika, watu walioishi karibu na Mika wakaitwa wakakusanyika pamoja, nao wakawafikia Wadani.
23 Ils crièrent après les fils de Dan, et ceux-ci, se retournant, dirent à Michas: « Que te faut-il, que tu aies attroupé ces hommes? »
Walipofuatilia wakipiga kelele Wadani wakawageukia na kumwambia Mika, “Una nini wewe hata ukaja na kundi la watu namna hii ili kupigana?”
24 Il répondit: « Mes dieux que j’ai faits, vous les avez enlevés, avec le prêtre, et vous êtes partis: que me reste-t-il? Comment donc pouvez-vous me dire: Que te faut-il? »
Akawajibu, “Mmechukua miungu yote niliyoitengeneza, mkachukua na kuhani wangu, nanyi mkaondoka. Nimebaki na nini kingine? Mnawezaje kuniuliza, ‘Una nini wewe?’”
25 Les fils de Dan lui dirent: « Ne nous fais pas entendre ta voix, de peur que des hommes irrités se jettent sur vous et que tu perdes ta vie et celle des gens de ta maison. »
Wadani wakamjibu, “Usibishane na sisi, la sivyo watu wenye hasira kali watakushambulia, nawe na watu wa nyumbani mwako mtapoteza maisha.”
26 Et les fils de Dan continuèrent leur route. Voyant qu’ils étaient plus forts que lui, Michas s’en retourna et revint dans sa maison.
Basi Wadani wakaenda zao, naye Mika alipoona kuwa wana nguvu kumliko yeye, akageuka na kurudi nyumbani kwake.
27 C’est ainsi que les Danites enlevèrent ce qu’avait fait Michas, et le prêtre qui était à son service; et ils marchèrent contre Laïs, contre un peuple tranquille et en sécurité; ils le passèrent au fil de l’épée et brûlèrent la ville.
Kisha wakachukua vile Mika alivyokuwa ametengeneza, na kuhani wake, wakaendelea hadi Laishi, dhidi ya watu walio na amani, wasiokuwa na wasiwasi. Wakawashambulia kwa upanga na kuuteketeza mji wao kwa moto.
28 Il n’y eut personne pour la délivrer, car elle était éloignée de Sidon, et ses habitants n’avaient point affaire avec d’autres hommes: elle était dans la vallée qui s’étend vers Beth-Rohob. Les fils de Dan rebâtirent la ville et y habitèrent;
Hapakuwa na yeyote wa kuwaokoa, kwa kuwa kulikuwa mbali sana na Sidoni na hawakuwa na ushirikiano na mtu mwingine yeyote. Mji ulikuwa kwenye bonde karibu na Beth-Rehobu. Wadani wakaujenga upya huo mji na kuishi humo.
29 ils l’appelèrent Dan, d’après le nom de Dan, leur père, qui était né d’Israël; mais la ville s’appelait primitivement Laïs.
Wakauita ule mji Dani kwa kufuata jina la baba yao aliyezaliwa na Israeli, ingawa mji huo ulikuwa ukiitwa Laishi hapo kwanza.
30 Les fils de Dan dressèrent pour eux l’image taillée, et Jonathan, fils de Gersam, fils de Moïse, lui et ses fils, furent prêtres de la tribu des Danites, jusqu’au jour de la captivité du pays.
Kisha Wadani wakajisimamishia sanamu ile ya kuchonga, naye Yonathani mwana wa Gershomu, mwana wa Mose pamoja na wanawe walikuwa makuhani wa kabila la Wadani mpaka nchi hiyo ilipotekwa.
31 Ils dressèrent pour eux l’image taillée qu’avait faite Michas, pendant tout le temps que la maison de Dieu fut à Silo.
Wakaisimamisha na kuiabudu hiyo sanamu ya kuchonga ya Mika aliyokuwa ameitengeneza, wakati wote ule nyumba ya Mungu ilipokuwa huko Shilo.