< Jérémie 30 >
1 La parole qui fut adressée à Jérémie de la part de Yahweh, en ces termes:
Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
2 Ainsi parle Yahweh, Dieu d’Israël: Écris dans un livre toutes les paroles que je t’ai dites.
“Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Andika katika kitabu maneno yote niliyonena na wewe.
3 Car voici que des jours viennent, — oracle de Yahweh, — où je ramènerai les captifs de mon peuple d’Israël et de Juda, dit Yahweh, et je le ferai rentrer dans le pays que j’ai donné à leurs pères, et ils le posséderont.
Siku zinakuja,’ asema Bwana, ‘nitakapowaleta watu wangu Israeli na Yuda kutoka uhamishoni, na kuwarudisha katika nchi niliyowapa baba zao ili kuimiliki,’ asema Bwana.”
4 Voici les paroles que Yahweh a prononcées sur Israël et sur Juda:
Haya ndiyo maneno Bwana aliyoyanena kuhusu Israeli na Yuda:
5 Ainsi parle Yahweh: Nous avons entendu un cri de terreur: c’est l’épouvante, et il n’y a point de paix!
“Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Vilio vya woga vinasikika: hofu kuu, wala si amani.
6 Demandez et regardez si un mâle enfante. Pourquoi vois-je tous les hommes avec les mains sur leurs reins comme une femme qui enfante, et pourquoi tous les visages sont-ils devenus livides?
Ulizeni na mkaone: Je, mwanaume aweza kuzaa watoto? Kwa nini basi ninaona kila mwanaume mwenye nguvu ameweka mikono yake tumboni kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa, kila uso ukigeuka rangi kabisa?
7 Malheur! car grande est cette journée; elle n’a pas sa pareille. C’est un temps d’angoisse pour Jacob; mais il en sera délivré.
Tazama jinsi ile siku itakavyokuwa ya kutisha! Hakutakuwa na nyingine mfano wake. Utakuwa wakati wa dhiki kwa Yakobo, lakini ataokolewa kutoka hiyo.
8 Et il arrivera en ce jour-là, — oracle de Yahweh des armées: Je briserai son joug de dessus ton cou, et je romprai tes liens. Des étrangers ne t’asserviront plus;
“‘Katika siku ile,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nitaivunja nira kutoka shingoni mwao na kuvipasua vifungo vyao; wageni hawatawafanya tena watumwa.
9 mais ils seront assujettis à Yahweh leur Dieu, et à David leur roi, que je susciterai pour eux.
Badala yake, watamtumikia Bwana, Mungu wao na Daudi mfalme wao, nitakayemwinua kwa ajili yao.
10 Toi donc ne crains point, mon serviteur Jacob; — oracle de Yahweh, ne t’effraie point, Israël. Car voici que je vais te retirer de la terre lointaine, et ta postérité du pays de son exil; Jacob reviendra, il sera tranquille, en sécurité, sans que personne l’épouvante.
“‘Hivyo usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, usifadhaike, ee Israeli,’ asema Bwana. ‘Hakika, nitakuokoa kutoka mbali, wazao wako kutoka nchi ya uhamisho wao. Yakobo atakuwa tena na amani na usalama, wala hakuna atakayemtia hofu.
11 Car je suis avec toi, — oracle de Yahweh, — pour te sauver; je ferai une extermination dans toutes les nations où je t’ai dispersé. Pour toi, je ne t’exterminerai pas, mais je te châtierai selon la justice, et je ne te laisserai pas impuni.
Mimi niko pamoja nawe, nami nitakuokoa,’ asema Bwana. ‘Ingawa nitayaangamiza kabisa mataifa yote ambamo miongoni mwao nimewatawanya, sitawaangamiza ninyi kabisa. Nitawaadhibu, lakini kwa haki. Sitawaacha kabisa bila adhabu.’
12 Car ainsi parle Yahweh: Ta blessure est incurable, ta plaie est douloureuse;
“Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Kidonda chako hakina dawa, jeraha lako haliponyeki.
13 nul ne plaide ta cause pour qu’on panse ta plaie, il n’y a pas pour toi de remède qui guérisse.
Hakuna yeyote wa kukutetea shauri lako, hakuna dawa ya kidonda chako, wewe hutapona.
14 Tous tes amants t’ont oubliée, ils ne se soucient point de toi. Car je t’ai frappée comme on frappe un ennemi, d’un châtiment cruel, à cause de la multitude de tes iniquités, parce que tes péchés se sont accrus.
Wale walioungana nawe wote wamekusahau, hawajali chochote kukuhusu wewe. Nimekupiga kama vile adui angelifanya, na kukuadhibu kama vile mtu mkatili angelifanya, kwa sababu hatia yako ni kubwa mno na dhambi zako ni nyingi sana.
15 Pourquoi crier à cause de ta blessure, de ce que ton mal est incurable? C’est à cause de la multitude de tes iniquités, et parce que tes péchés se sont accrus, que je t’ai fait ces choses.
Kwa nini unalia kwa ajili ya jeraha lako, yale maumivu yako yasiyoponyeka? Kwa sababu ya uovu wako mkubwa na dhambi zako nyingi nimekufanyia mambo haya.
16 C’est pourquoi tous ceux qui te dévorent seront dévorés, tous tes oppresseurs iront en captivité, ceux qui te dépouillent seront dépouillés, et je livrerai au pillage tous ceux qui te pillent.
“‘Lakini watu wote wakuangamizao wataangamizwa; adui zako wote watakwenda uhamishoni. Wale wote wakutekao nyara watatekwa nyara; wote wakufanyao mateka nitawafanya mateka.
17 Car je vais te panser, de tes plaies je vais te guérir, — oracle de Yahweh. Car on t’appelle « Repoussée », « Sion dont nul ne prend souci. »
Lakini nitakurudishia afya yako na kuyaponya majeraha yako,’ asema Bwana, ‘kwa sababu umeitwa mwenye kutupwa, Sayuni ambaye hakuna yeyote anayekujali.’
18 Ainsi parle Yahweh: Voici que je vais rétablir les tentes de Jacob, et j’aurai compassion de leurs demeures; la ville sera rebâtie sur sa colline, et le palais rétabli à sa place.
“Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Nitarudisha baraka za mahema ya Yakobo, na kuhurumia maskani yake. Mji utajengwa tena juu ya magofu yake, nalo jumba la kifalme litasimama mahali pake halisi.
19 Il en sortira des chants de louange, et des cris d’allégresse. Je les multiplierai, et ils ne seront plus diminués; je les glorifierai, et ils ne seront plus méprisés.
Nyimbo za kushukuru zitatoka kwao na sauti ya furaha. Nitaiongeza idadi yao wala hawatapungua, nitawapa heshima na hawatadharauliwa.
20 Ses fils seront comme autrefois; son assemblée sera affermie devant moi, et je châtierai tous ses oppresseurs.
Watoto wao watakuwa kama walivyokuwa siku za zamani, nayo jumuiya yao itaimarishwa mbele yangu; nitawaadhibu wale wote wawaoneao.
21 Son chef sera un des siens, et son souverain sortira de son sein; je le ferai venir et il s’approchera de moi; car quel est l’homme qui disposerait son cœur de manière à s’approcher de moi? — oracle de Yahweh.
Mmoja wao atakuwa kiongozi wao; mtawala wao atainuka miongoni mwao. Nitamleta karibu nami, naye atanikaribia mimi, kwa maana ni nani yule atakayejitolea kuwa karibu nami?’ asema Bwana.
22 Et vous serez mon peuple, et je serai votre Dieu.
‘Kwa hiyo ninyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.’”
23 Voici que la tempête de Yahweh, la fureur, va éclater; l’orage se précipite, il fond sur la tête des impies.
Tazama, tufani ya Bwana italipuka kwa ghadhabu, upepo wa kisulisuli uendao kasi utashuka juu ya vichwa vya waovu.
24 Le feu de la colère de Yahweh ne retournera pas en arrière, qu’il n’ait agi et réalisé les desseins de son cœur; à la fin des temps vous le comprendrez.
Hasira kali ya Bwana haitarudi nyuma mpaka atakapotimiza makusudi yote ya moyo wake. Siku zijazo mtayaelewa haya.