< Jérémie 21 >
1 La parole qui fut adressée à Jérémie de la part de Yahweh, lorsque le roi Sédécias envoya vers lui Phassur, fils de Melchias, et le prêtre Sophonias, fils de Maasias, pour lui dire:
Neno lilimjia Yeremia kutoka kwa Bwana wakati Mfalme Sedekia alipowatuma Pashuri mwana wa Malkiya, na kuhani Sefania mwana wa Maaseya kwake, kusema:
2 « Consulte, je t’en prie, Yahweh pour nous; car Nabuchodonosor, roi de Babylone, nous fait la guerre; peut-être Yahweh renouvellera-t-il en notre faveur tous ses grands miracles, afin qu’il s’éloigne de nous. »
“Tuulizie sasa kwa Bwana, kwa sababu Nebukadneza mfalme wa Babeli anatushambulia. Labda Bwana atatenda maajabu kwa ajili yetu kama nyakati zilizopita, ili Nebukadneza atuondokee.”
3 Jérémie leur répondit: Voici ce que vous direz à Sédécias:
Lakini Yeremia akawajibu, “Mwambieni Sedekia,
4 Ainsi parle Yahweh, Dieu d’Israël: Voici que je vais faire retourner en arrière les armes de guerre qui sont dans vos mains, avec lesquelles vous combattez hors des murs le roi de Babylone et les Chaldéens qui vous assiègent, et je les rassemblerai au milieu de la ville;
‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: Ninakaribia kuwageuzia silaha za vita zilizo mikononi mwenu, ambazo mnatumia kupigana na mfalme wa Babeli na Wakaldayo ambao wako nje ya ukuta wakiwazunguka kwa jeshi. Nami nitawakusanya ndani ya mji huu.
5 et moi, je combattrai contre vous la main étendue et d’un bras puissant, avec colère, fureur et grande indignation.
Mimi mwenyewe nitapigana dhidi yenu kwa mkono wangu ulionyooshwa na mkono wa nguvu, kwa hasira na ghadhabu kali na ukali mwingi.
6 Je frapperai les habitants de cette ville, les hommes et les bêtes, et ils mourront d’une grande peste.
Nitawaangamiza waishio katika mji huu, watu na wanyama, nao watauawa kwa tauni ya kutisha.
7 Après cela, — oracle de Yahweh, je livrerai Sédécias, roi, de Juda, ses serviteurs, le peuple, et ceux qui, dans cette ville auront échappé à la peste, à l’épée et à la famine, je les livrerai aux mains de Nabuchodonosor, roi de Babylone, aux mains de leurs ennemis et de ceux qui en veulent à leur vie; et il les passera au fil de l’épée; il ne les épargnera pas, il n’aura ni pitié ni compassion.
Baada ya hayo, nitamtia Sedekia mfalme wa Yuda, maafisa wake na watu wa mji huu ambao walinusurika tauni, upanga na njaa, mkononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, na kwa adui zao wale wanaotafuta uhai wao. Atawaua kwa upanga; hatakuwa na rehema juu yao au huruma wala kuwasikitikia,’ asema Bwana.
8 Et tu diras à ce peuple: Ainsi parle Yahweh: Voici que je mets devant vous le chemin de la vie et le chemin de la mort.
“Zaidi ya hayo, waambie watu hawa, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Tazama, naweka mbele yenu njia ya uzima, na njia ya mauti.
9 Celui qui restera dans cette ville mourra par l’épée, par la famine où par la peste; celui qui en sortira pour se rendre aux Chaldéens qui vous assiègent vivra et aura sa vie pour butin.
Yeyote atakayekaa katika mji huu atakufa kwa upanga, njaa au tauni. Lakini yeyote atakayetoka na kujisalimisha kwa Wakaldayo ambao wameuzunguka mji huu kwa jeshi, atanusurika, naye ataishi.
10 Car j’ai tourné ma face vers cette ville pour lui faire du mal, et non pas du bien, — oracle de Yahweh; elle sera livrée aux mains du roi de Babylone, et il la consumera par le feu.
Nimekusudia kuufanyia mji huu jambo baya, wala si jema. Utatiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli, naye atauteketeza kwa moto, asema Bwana.’
11 Et à la maison du roi de Juda tu diras: Écoutez la parole de Yahweh,
“Zaidi ya hayo, ambia nyumba ya mfalme ya Yuda, ‘Sikia neno la Bwana,
12 maison de David: Ainsi parle Yahweh: Rendez la justice dès le matin; arrachez l’opprimé des mains de l’oppresseur, de peur que ma colère n’éclate comme un feu et ne brûle sans qu’on puisse l’éteindre, à cause de la méchanceté de vos actions.
Ewe nyumba ya Daudi, hili ndilo Bwana asemalo: “‘Hukumuni kwa haki kila asubuhi, mwokoeni mikononi mwa mdhalimu yeye aliyetekwa nyara, la sivyo ghadhabu yangu italipuka na kuwaka kama moto kwa sababu ya uovu mlioufanya: itawaka na hakuna wa kuizima.
13 Voici que j’en viens à toi, habitante de la vallée, rocher de la plaine, — oracle Yahweh, vous qui dites: « Qui descendra sur nous, et qui entrera dans nos retraites? »
Niko kinyume nawe, ee Yerusalemu, wewe uishiye juu ya bonde hili kwenye uwanda wa juu wa miamba, asema Bwana, wewe usemaye, “Ni nani awezaye kuja kinyume chetu? Nani ataingia mahali pa kimbilio letu?”
14 Je vous châtierai selon le fruit de vos œuvres, — oracle de Yahweh; je mettrai le feu à sa forêt, et il en dévorera tous les alentours.
Nitawaadhibu kama istahilivyo matendo yenu, asema Bwana. Nitawasha moto katika misitu yenu ambao utateketeza kila kitu kinachowazunguka.’”