< Isaïe 7 >

1 Il arriva du temps d’Achaz, fils de Joatham, fils d’Ozias, roi de Juda, que Rasin, roi de Syrie, avec Phacée, fils de Romélie, roi d’Israël, monta contre Jérusalem pour l’attaquer; mais il ne put s’en emparer.
Wakati Ahazi mwana wa Yothamu, mwana wa Uzia, alipokuwa mfalme wa Yuda, Mfalme Resini wa Aramu, na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli walipanda kupigana dhidi ya Yerusalemu, lakini hawakuweza kuushinda.
2 On annonça à la maison de David cette nouvelle: « La Syrie est campée en Éphraïm. » Alors le cœur du roi et le cœur de son peuple furent agités comme les arbres de la forêt sont agités par le vent.
Wakati huu nyumba ya Daudi iliambiwa, “Aramu wameungana na Efraimu.” Kwa hiyo mioyo ya Ahazi na watu wake ilitikiswa, kama miti ya msituni inavyotikiswa na upepo.
3 Et Yahweh dit à Isaïe: « Sors à la rencontre d’Achaz, toi et Schéar-Jasub, ton fils, vers l’extrémité du canal de l’étang supérieur, sur le chemin du champ du foulon.
Ndipo Bwana akamwambia Isaya, “Toka uende, wewe na mwanao Shear-Yashubu, mkutane na Ahazi huko mwisho wa mfereji wa Bwawa la Juu, kwenye barabara iendayo Shamba la Dobi.
4 Et tu lui diras: Prends garde, tiens-toi tranquille, ne crains point, et que ton cœur ne défaille point devant ces deux bouts de tisons fumants, à cause de la fureur de Rasin et de la Syrie, et du fils de Romélie.
Mwambie, ‘Uwe mwangalifu, utulie na usiogope. Usife moyo kwa ajili ya watu hawa wawili walio kama visiki vya kuni vifukavyo moshi, kwa ajili ya hasira kali ya Resini na Aramu na ya mwana wa Remalia.
5 Parce que la Syrie a médité le mal contre toi ainsi qu’Éphraïm et le fils de Romélie, en disant:
Aramu, Efraimu na mwana wa Remalia wamepanga shauri baya ili wakuangamize, wakisema,
6 « Montons contre Juda, jetons-le dans l’épouvante, envahissons-le, et établissons-y pour roi le fils de Tabéel;
“Tuishambulie Yuda, naam, tuirarue vipande vipande na kuigawa miongoni mwetu, na kumtawaza mwana wa Tabeeli awe mfalme juu yake.”
7 ainsi parle le Seigneur Yahweh: Cela n’aura pas d’effet, cela ne sera pas!
Lakini Bwana Mwenyezi asema hivi: “‘Jambo hili halitatendeka, halitatokea,
8 Car la tête de la Syrie, c’est Damas, et la tête de Damas, c’est Rasin; et encore soixante-cinq ans, et Éphraïm aura cessé d’être un peuple.
kwa kuwa kichwa cha Aramu ni Dameski, na kichwa cha Dameski ni Resini peke yake. Katika muda wa miaka sitini na mitano, Efraimu atakuwa ameharibiwa kiasi kwamba hataweza tena kuwa taifa.
9 Et la tête d’Éphraïm, c’est Samarie, et la tête de Samarie, c’est le fils de Romélie. Si vous ne croyez pas, vous ne subsisterez pas! »
Kichwa cha Efraimu ni Samaria, na kichwa cha Samaria ni mwana wa Remalia peke yake. Kama hamtasimama thabiti katika imani yenu, hamtaimarika kamwe.’”
10 Yahweh parla encore à Achaz, en disant:
Bwana akasema na Ahazi tena,
11 « Demande un signe à Yahweh, ton Dieu, demande-le dans les profondeurs du schéol ou dans les hauteurs du ciel. » (Sheol h7585)
“Mwombe Bwana Mungu wako ishara, iwe kwenye vina virefu sana, au kwenye vimo virefu sana.” (Sheol h7585)
12 Mais Achaz dit: « Je ne le demanderai pas, je ne tenterai pas Yahweh. »
Lakini Ahazi akasema, “Sitaomba; sitamjaribu Bwana.”
13 Et Isaïe dit: « Écoutez, maison de David: Est-ce trop peu pour vous de fatiguer les hommes, que vous fatiguiez aussi mon Dieu?
Ndipo Isaya akasema, “Sikia sasa, ewe nyumba ya Daudi! Je, haitoshi kujaribu uvumilivu wa wanadamu? Je, mtaujaribu uvumilivu wa Mungu wangu pia?
14 C’est pourquoi le Seigneur lui-même vous donnera un signe: Voici que la Vierge a conçu, et elle enfante un fils, et elle lui donne le nom d’Emmanuel.
Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara: Bikira atachukua mimba, naye atamzaa mwana, na ataitwa Imanueli.
15 Il mangera de la crème et du miel, jusqu’à ce qu’il sache rejeter le mal et choisir le bien.
Atakula jibini na asali atakapokuwa ameweza kukataa mabaya na kuchagua mema.
16 Car avant que l’enfant sache rejeter le mal et choisir le bien, le pays dont tu redoutes les deux rois sera dévasté.
Lakini kabla mtoto hajajua kukataa mabaya na kuchagua mema, nchi ya wafalme hao wawili unaowaogopa itafanywa ukiwa.
17 Yahweh fera venir sur toi et sur ton peuple, et sur la maison de ton père, des jours tels qu’il n’en est pas venu depuis le jour où Éphraïm s’est séparé de Juda, — le roi d’Assyrie. »
Bwana ataleta juu yako, juu ya watu wako, na juu ya nyumba ya baba yako wakati ambao haujawahi kuwako tangu Efraimu alipojitenga na Yuda: yeye atawaleteeni mfalme wa Ashuru.”
18 En ce jour-là, Yahweh sifflera la mouche qui est à l’extrémité des fleuves d’Égypte, et l’abeille qui est au pays d’Assyrie.
Katika siku ile Bwana atawapigia filimbi mainzi kutoka vijito vya mbali vya Misri, na nyuki kutoka nchi ya Ashuru.
19 Elles viendront et se poseront toutes dans les vallées escarpées et dans les fentes des rochers, sur tous les buissons et sur tous les pâturages.
Wote watakuja na kukaa kwenye mabonde yenye miteremko, na kwenye nyufa za miamba, kwenye vichaka vyote vyenye miiba, na kwenye mashimo yote ya maji.
20 En ce jour-là, le Seigneur rasera avec un rasoir qu’il aura loué au delà du Fleuve — avec le roi d’Assyrie, — la tête et le poil des pieds, et il enlèvera aussi la barbe.
Katika siku ile Bwana atatumia wembe ulioajiriwa kutoka ngʼambo ya Mto, yaani mfalme wa Ashuru, kunyoa nywele za kichwa chako na malaika ya miguu yako, na kuziondoa ndevu zako pia.
21 En ce jour-là, un homme nourrira une vache et deux brebis,
Katika siku ile, mtu atahifadhi hai ndama mmoja na kondoo wawili.
22 et, à cause de l’abondance du lait qu’elles donneront, on ne mangera plus que de la crème; car c’est de la crème et du miel que mangeront tous ceux qui seront restés dans le pays.
Kwa ajili ya wingi wa maziwa watakayotoa, atapata jibini ya kula. Wote watakaobakia katika nchi watakula jibini na asali.
23 En ce jour-là, tout endroit où il y avait mille ceps de vigne, valant mille pièces d’argent, sera couvert de ronces et d’épines.
Katika siku ile, kila mahali palipokuwa na mizabibu elfu moja yenye thamani ya shekeli 1,000 za fedha, patakuwa na michongoma na miiba tu.
24 On y entrera avec des flèches et avec l’arc, car tout le pays ne sera que ronces et épines.
Watu watakwenda huko wakiwa na upinde na mshale, kwa maana nchi itafunikwa na michongoma na miiba.
25 Et sur toutes les montagnes que l’on cultivait avec le sarcloir, tu n’iras plus, par crainte des ronces et des épines, elles seront un pâturage de bœufs, et une terre foulée par les brebis.
Kuhusu vilima vyote vilivyokuwa vikilimwa kwa jembe, hamtakwenda huko tena kwa ajili ya hofu ya michongoma na miiba. Patakuwa mahali ambapo ngʼombe wataachiwa huru, na kondoo kukimbia kimbia.

< Isaïe 7 >