< Isaïe 29 >
1 Malheur à Ariel, à Ariel, à la cité où David a dressé sa tente! Ajoutez année à année, que les solennités parcourent leur cycle,
Ole wako, wewe Arieli, Arieli, mji alimokaa Daudi! Ongezeni mwaka kwa mwaka, na mzunguko wa sikukuu zenu uendelee.
2 et je serrerai de près Ariel, et il n’y aura que plaintes et gémissements! Mais elle sera pour moi comme Ariel
Hata hivyo nitauzunguka Arieli kwa jeshi, utalia na kuomboleza, utakuwa kwangu kama mahali pa kuwashia moto madhabahuni.
3 je camperai tout autour de toi, je t’environnerai de postes armés, et j’établirai contre toi des retranchements.
Nitapiga kambi pande zote dhidi yako, nitakuzunguka kwa minara na kupanga mazingirwa yangu dhidi yako.
4 Tu seras abaissée; c’est de la terre que s’élèvera ta voix, et de la poussière que se feront entendre tes sourds accents; ta voix sortira de terre, comme celle d’un spectre, et ta parole montera de la poussière comme un murmure. —
Utakaposhushwa, utanena kutoka ardhini, utamumunya maneno yako kutoka mavumbini. Sauti yako itatoka katika nchi kama vile ya mzimu, utanongʼona maneno yako toka mavumbini.
5 Et la multitude de tes ennemis sera comme une fine poussière, et la multitude des guerriers comme la paille qui s’envole.
Lakini adui zako wengi watakuwa kama vumbi laini, kundi la wakatili watakuwa kama makapi yapeperushwayo. Naam, ghafula, mara moja,
6 Et il arrivera que soudain, en un instant, tu seras visitée, par Yahweh des armées avec fracas, tonnerre et grand bruit, tourbillon, tempête et flamme de feu dévorant.
Bwana Mwenye Nguvu Zote atakuja na ngurumo, tetemeko la ardhi, na kwa sauti kuu, atakuja na dhoruba, tufani na miali ya moto iteketezayo.
7 Et il en sera comme d’un songe, vision de la nuit, de la multitude de toutes les nations qui combattront contre Ariel, et de tous ceux qui combattront contre elle et sa forteresse et la serreront de près.
Kisha makundi ya mataifa yote yale yapiganayo dhidi ya Arieli, yale yanayomshambulia yeye na ngome zake, na kumzunguka kwa jeshi, watakuwa kama ilivyo ndoto, kama maono wakati wa usiku:
8 Comme celui qui a faim rêve qu’il mange, et, à son réveil, son âme est vide; et comme un homme qui a soif rêve qu’il boit, et, à son réveil, il est épuisé et toujours altéré; ainsi il en sera de la multitude de toutes les nations, qui marchent contre la montagne de Sion.
kama vile mtu aliye na njaa aotavyo kuwa anakula, lakini huamka, bado njaa yake ingalipo, kama vile mtu mwenye kiu aotavyo kuwa anakunywa maji, lakini huamka akiwa anazimia, akiwa bado angali ana kiu. Hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa makundi yote ya mataifa yanayopigana dhidi ya Mlima Sayuni.
9 Étonnez-vous et soyez dans la stupeur! Aveuglez-vous et soyez aveuglés! Ils sont ivres, mais pas de vin; ils chancellent, mais pas de liqueurs fortes.
Duwaeni na kushangaa, jifanyeni vipofu wenyewe na msione, leweni, lakini si kwa mvinyo, pepesukeni lakini si kwa kileo.
10 Car Yahweh a répandu sur vous un esprit de léthargie; il a fermé vos yeux — les prophètes; il a jeté un voile sur vos têtes — les voyants.
Bwana amewaleteeni usingizi mzito: Ameziba macho yenu (ninyi manabii); amefunika vichwa vyenu (ninyi waonaji).
11 Et toute vision est devenue pour vous comme les paroles d’un livre scellé. On le présente à un homme qui sait lire, en disant: « Lis cela! » et il dit: « Je ne puis, car ce livre est scellé. »
Kwa maana kwenu ninyi, maono haya yote si kitu ila maneno yaliyotiwa lakiri katika kitabu. Kama mkimpa mtu yeyote awezaye kusoma kitabu hiki, nanyi mkamwambia, “Tafadhali kisome,” yeye atajibu, “Mimi siwezi, kwa kuwa kimetiwa lakiri.”
12 On le présente à un homme qui ne sait pas lire, en disant: « Lis cela! » et il dit: « Je ne sais pas lire. »
Au kama mkimpa mtu yeyote kitabu hiki asiyeweza kusoma na kumwambia, “Tafadhali kisome,” atajibu, “Mimi sijui kusoma.”
13 Le Seigneur dit: Puisque ce peuple s’approche en paroles et m’honore des lèvres, tandis qu’il tient son cœur éloigné de moi, et que le culte qu’il me rend est un précepte appris des hommes,
Bwana anasema: “Watu hawa hunikaribia kwa vinywa vyao na kuniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami. Ibada yao kwangu inatokana na maagizo waliyofundishwa na wanadamu.
14 à cause de cela, je continuerai à user de prodiges, avec ce peuple, de prodiges étranges. Et la sagesse de ses sages périra, et l’intelligence de ses docteurs s’obscurcira.
Kwa hiyo mara nyingine tena nitawashangaza watu hawa, kwa ajabu juu ya ajabu. Hekima ya wenye hekima itapotea, nayo akili ya wenye akili itatoweka.”
15 Malheur à ceux qui cachent profondément à Yahweh le secret de leurs desseins, dont l’œuvre s’accomplit dans les ténèbres, et qui disent: « Qui nous voit, qui nous connaît? »
Ole kwa wale wanaokwenda kwenye vilindi virefu kumficha Bwana mipango yao, wafanyao kazi zao gizani na kufikiri, “Ni nani anayetuona? Ni nani atakayejua?”
16 Quelle folie! Le potier sera-t-il donc estimé pour de l’argile, que l’œuvre dise de l’ouvrier: « Il ne m’a point faite; » et que le vase dise du potier: « Il n’y entend rien? »
Mnapindua mambo juu chini, kana kwamba mfinyanzi aweza kufikiriwa kuwa kama udongo wa mfinyanzi! Je, kile kilichofinyangwa chaweza kumwambia yule aliyekifinyanga, “Wewe hukunifinyanga mimi?” Je, chungu kinaweza kumwambia mfinyanzi, “Wewe hujui chochote?”
17 Est-ce que dans un peu de temps, le Liban ne sera pas changé en verger, et le verger ne sera pas réputé une forêt?
Kwa muda mfupi sana, je, Lebanoni haitageuzwa kuwa shamba lenye rutuba, na shamba lenye rutuba liwe kama msitu?
18 En ce jour-là, les sourds entendront les paroles du livre, et, sortant des ténèbres et de l’obscurité, les aveugles verront.
Katika siku ile viziwi watasikia maneno ya kitabu, na katika utusitusi na giza macho ya kipofu yataona.
19 Les humbles se réjouiront de plus en plus en Yahweh, et les plus pauvres tressailliront dans le Saint d’Israël.
Mara nyingine tena wanyenyekevu watafurahi katika Bwana, wahitaji watafurahi katika yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
20 Car l’oppresseur aura disparu, et le moqueur aura péri, et tous ceux qui méditent l’iniquité seront exterminés,
Wakatili watatoweka na wenye kudhihaki watatokomea, nao wote wenye jicho la uovu watakatiliwa mbali,
21 ceux qui condamnent un homme pour un mot, qui tendent des pièges à celui qui les confond à la porte, et qui perdent le juste par leurs mensonges.
wale ambao kwa neno humfanya mtu kuwa mwenye hatia, wamtegeao mtego mtetezi katika mahakama, na kwa ushuhuda wa uongo humnyima haki yeye asiye na hatia.
22 C’est pourquoi ainsi parle Yahweh à la maison de Jacob, lui qui a racheté Abraham: Jacob n’aura plus désormais à rougir, et son front désormais ne pâlira plus.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana, aliyemkomboa Abrahamu, analosema kwa nyumba ya Yakobo: “Yakobo hataaibishwa tena, wala nyuso zao hazitabadilika sura tena.
23 Car, lorsqu’il verra, lui et ses enfants, l’œuvre de mes mains au milieu d’eux, ils sanctifieront mon nom, ils sanctifieront le Saint de Jacob, et ils révéreront le Dieu d’Israël.
Wakati watakapoona watoto wao miongoni mwao, kazi ya mikono yangu, watalitakasa Jina langu takatifu; wataukubali utakatifu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Yakobo, nao watamcha Mungu wa Israeli.
24 Ceux qui avaient l’esprit égaré apprendront la sagesse, et ceux qui murmuraient recevront l’instruction.
Wale wanaopotoka rohoni watapata ufahamu, nao wale wanaolalamika watayakubali mafundisho.”