< Isaïe 13 >
1 Oracle sur Babylone, révélé à Isaïe, fils d’Amots.
Tamko kuhusu Babeli, ambalo Isaya mtoto wa Amozi alipokea:
2 Sur une montagne nue levez un étendard; appelez-les à haute voix, faites des signes de la main, et qu’ils franchissent les portes des princes.
Kwenye mlima wa wazi imewekwa bendera ya ishara, lia kwa sauti kwao, wapungie mikono waende kwenye lango la wenye vyeo.
3 Moi, j’ai donné ordre à mes consacrés; j’ai appelé mes héros pour servir ma colère, ceux qui acclament avec joie ma majesté.
Nimewamuru watakatifu wangu, ndio, nimewaita watu wangu wenye nguvu kutekeleza asira yangu, na hata watu wangu wanojigmba na kujiinua wenyewe.
4 On entend sur les montagnes une rumeur: on dirait le bruit d’un peuple nombreux; on entend un tumulte de royaumes, de nations rassemblées: C’est Yahweh des armées qui passe en revue ses troupes de guerre.
Kelele za umati wa watu kwenye milima, za watu wengi! Kelele za ghasiaza ufalme kama mataifa mengi yamekusanyika pamoja! Yahwe wa majeshi anapanga jeshi kwa vita.
5 Ils viennent d’un pays lointain, de l’extrémité du ciel, Yahweh et les instruments de son courroux, pour ravager toute la terre.
Wametoka katika nchi ya mbali, kutoka juu ya upeo wa macho. Ni Yahwe na silaha zake za hukumu, kuhiharibu nchi yetu.
6 Poussez des hurlements, car le jour de Yahweh est proche: il vient comme une dévastation du Tout-puissant.
Omboleza maana siku ya Yahwe imekaribia; itakuja na uharibifu kutoka kwa Mwenyenzi.
7 C’est pourquoi toute main sera défaillante, et tout cœur d’homme se fondra.
Hivyo basi mikono ining'inizwe kama kiwete, na kila moyo ulioyeyuka.
8 Ils trembleront, les transes et les douleurs les saisiront; ils se tordront comme une femme qui enfante; ils se regarderont les uns les autres avec stupeur; leurs visages seront comme la flamme.
Itawatisha; maumivu na uchungu atawapa wao, kama mwanamke ambaye anajifungua. Watangalia kwa kushangaa kwa kila mmoja mmoja; nyuso zao zitakuwa kama moto.
9 Voici que le jour de Yahweh est venu, jour cruel, de fureur et d’ardente colère, pour réduire la terre en désert, et en exterminer les pécheurs.
Tazama, siku za Yahwe zinakuja na laana kali wingi wa hasira, kuifanya nchi yenye ukiwa na kuharibu wenye dhambi katika nchi.
10 Car les étoiles du ciel et leurs constellations ne font point briller leur lumière; le soleil s’est obscurci à son lever, et la lune ne répand plus sa clarté.
Nyota ya mbinguni na matangamano havitatoa nuru yake. Jua litakuwa giza na hata mwenzi hautaangaza.
11 Je punirai le monde pour sa malice, et les méchants pour leur iniquité; je ferai cesser l’arrogance des superbes, et j’abaisserai l’orgueil des tyrans.
Nitaihadhibu nchi kwa maovu yake na makosa ya uovu wao. Nitamaliza kiburi cha majivuno na nitawashusha wenye kiburi wasiwe makali.
12 Je rendrai les hommes plus rares que l’or fin, plus rares que l’or d’Ophir.
Nitawafanya watu kuwa nadra zaidi ya dhahabu nzuri na watu kuwa vigumu kupatikana zaidi ya dhahabu safi ya Ofiri.
13 C’est pourquoi je ferai trembler les cieux, et la terre sera ébranlée de sa place, par la fureur de Yahweh des armées, au jour où s’allumera sa colère.
Hivyo basi nitazifanya mbingu kutingishika, na dunia itayumba kutoka sehemu iliyoko, Kwa hasira ya Yahwe wa majeshi, na siku ya hasira yake.
14 Alors, comme une gazelle que l’on poursuit, comme un troupeau que personne ne rassemble, chacun se tournera vers son peuple, et s’enfuira dans son pays.
Kama Paa anayewindwa au kama kondoo wasio na mchungaji, kila mtu atageukia watu wake na kukimbia kwenye nchi yake.
15 Tous ceux qu’on trouvera seront transpercés, tous ceux qu’on saisira tomberont par l’épée.
Kwa yeyote atakayeonekana atauliwa, na yeyote atakayekamatwa atauliwa kwa upanga.
16 Leurs petits enfants seront écrasés sous leurs yeux, leurs maisons pillées et leurs femmes violées.
Watoto wao watakatwa vipandevipande mbele ya macho yao. Nyumba zao zitavamiwa na wake zao watabakwa.
17 Voici que je fais lever contre eux les Mèdes, qui ne font point cas de l’argent, et ne convoitent pas l’or.
Tazama, ninakaribia kuwakoroga Wamede ili wawavamie wao, ambao hawaoni maana ya fedha wala furaha ya dhahabu.
18 Leurs arcs écraseront les jeunes gens; ils ne feront point grâce au fruit des entrailles; leur œil n’aura pas pitié des enfants.
Mishale yao itawachoma vijana wadogo. Hakutakuwa na shimo kwa watoto wao na hawatawacha watoto wao.
19 Et Babylone, l’ornement des royaumes, la parure des fiers Chaldéens, sera comme Sodome et Gomorrhe que Dieu a détruites.
Na Babali ufalme unaovutia zaidi, fahari ya mapambo ya wakaldyo, itaangamizwa na Mungu kama Sodoma na Gomora.
20 Elle ne sera jamais plus peuplée, elle ne sera plus habitée dans le cours des âges; l’Arabe n’y dressera pas sa tente, et le berger n’y parquera pas ses troupeaux.
Hapatakuwa na wenyeji wala wakazi kutoka kizazi kimoja hadi kizazi kingine. Mwarabu atapiga hema lake uko wala wachungaji hawatalaza mifugo yao pale.
21 Les animaux du désert y feront leur gîte; les hiboux rempliront ses maisons; là habiteront les autruches, et le satyre y bondira.
Lakini wanyama pori wa jangwani watalala pale. Nyumba zao zitajaa bundi; na mbuni watakaa huko na mbuzi pori wataruka pale.
22 Les chacals hurleront dans ses palais déserts, et les chiens sauvages dans ses maisons de plaisir. Son temps est proche, et ses jours ne seront pas prolongés.
Fisi watalia kwenye ngome yao, na mbeha katika maeneo yao mazuri. Mda wao umekaribia, na siku zao hazitachelewa.