< Genèse 37 >
1 Jacob s’établit dans le pays où son père avait séjourné dans le pays de Chanaan.
Yakobo akaishi Kanaani katika nchi ambayo baba yake alikuwa ameishi.
2 Voici l’histoire de Jacob. Joseph, âgé de dix-sept ans, faisait paître les brebis avec ses frères; comme il était encore jeune, il se trouvait avec les fils de Bala et avec les fils de Zelpha, femmes de son père; et Joseph rapporta à leur père de mauvais bruits qui couraient sur leur compte.
Zifuatazo ni habari za Yakobo. Yosefu, kijana wa miaka kumi na saba, alikuwa akichunga makundi ya kondoo na mbuzi pamoja na ndugu zake wa mama wengine, yaani wana wa Bilha na wana wa Zilpa wake za baba yake, naye akawa akimletea baba yake taarifa mbaya kuhusu hao ndugu zake.
3 Or Israël aimait Joseph plus que tous ses autres fils, parce que c’était un fils de sa vieillesse; et il lui fit une robe longue.
Basi, Israeli akampenda Yosefu kuliko yeyote miongoni mwa kaka zake, kwani ni mwanawe wa uzeeni, akamshonea joho lililorembwa vizuri sana.
4 Ses frères, voyant que leur père l’aimait plus qu’eux tous, le prirent en haine, et ils ne pouvaient plus lui parler amicalement.
Ndugu zake walipoona kwamba baba yao anampenda Yosefu kuliko yeyote mwingine miongoni mwao, walimchukia na hawakusema naye neno lolote jema.
5 Joseph eut un songe, et il le raconta à ses frères, qui le haïrent encore davantage.
Yosefu akaota ndoto, naye alipowaeleza ndugu zake, wakamchukia zaidi.
6 Il leur dit: « Écoutez, je vous prie, le songe que j’ai eu:
Akawaambia, “Sikilizeni ndoto niliyoota:
7 Nous étions à lie des gerbes au milieu des champs; et voici, ma gerbe s’est levée et s’est tenue debout, et vos gerbes l’ont entourée et se sont prosternées devant elle. »
Tulikuwa tukifunga miganda ya nafaka shambani, ghafula mganda wangu ukasimama wima, wakati miganda yenu ikiuzunguka na kuuinamia.”
8 Ses frères lui dirent: « Est-ce que tu régneras sur nous? est-ce que tu nous domineras? » Et ils le haïrent encore davantage pour ses songes et pour ses paroles.
Ndugu zake wakamwambia, “Wewe unakusudia kututawala? Hivi kweli wewe utatutawala sisi?” Wakaongeza kumchukia zaidi kwa sababu ya ndoto yake pamoja na yale aliyowaambia.
9 Il eut encore un autre songe, qu’il raconta à ses frères. Il dit: « J’ai eu encore un songe: le soleil, la lune et onze étoiles se prosternaient devant moi. »
Kisha akaota ndoto nyingine, akawaambia ndugu zake akisema, “Sikilizeni, nimeota ndoto nyingine, wakati huu jua, mwezi na nyota kumi na moja zilikuwa zinanisujudia.”
10 Il le raconta à son père et à ses frères, et son père le réprimanda, en disant: « Que signifie ce songe que tu as eu? Faudra-t-il que nous venions, moi, ta mère et tes frères, nous prosterner à terre devant toi? »
Alipomwambia baba yake pamoja na ndugu zake, baba yake akamkemea akisema, “Ni ndoto gani hii uliyoota? Hivi kweli mama yako na mimi na ndugu zako tutakuja kukusujudia wewe hadi nchi?”
11 Et ses frères furent jaloux de lui, mais son père conservait la chose dans son cœur.
Ndugu zake wakamwonea wivu, lakini baba yake akaliweka jambo hilo moyoni.
12 Les frères de Joseph allèrent paître les troupeaux de leur père à Sichem.
Basi, ndugu zake walikuwa wamekwenda kuchunga makundi ya baba yao karibu na Shekemu,
13 Et Israël dit à Joseph: « Tes frères ne paissent-ils pas le troupeau à Sichem? Viens, que je t’envoie vers eux. » Il répondit: « Me voici. »
naye Israeli akamwambia Yosefu, “Kama ujuavyo, ndugu zako wanachunga makundi huko karibu na Shekemu. Njoo, nitakutuma kwao.” Yosefu akajibu, “Vema sana, niko tayari.”
14 Et Israël lui dit: « Va donc, et vois si tes frères vont bien et si le troupeau est en bon état, et tu m’en apporteras des nouvelles. » Et il l’envoya de la vallée d’Hébron, et Joseph alla à Sichem.
Kwa hiyo akamwambia, “Nenda uone kama mambo yote ni salama kwa ndugu zako na makundi, kisha uniletee habari.” Ndipo akamtuma Yosefu kutoka Bonde la Hebroni. Yosefu alipofika Shekemu,
15 Un homme, l’ayant rencontré errant dans la campagne, le questionna, en disant: « Que cherches-tu? »
mtu mmoja akamkuta akizungukazunguka mashambani na akamuuliza, “Unatafuta nini?”
16 Il répondit: « Je cherche mes frères; indique-moi, je te prie, où ils font paître leur troupeau. »
Akajibu, “Ninawatafuta ndugu zangu. Unaweza kuniambia wanachunga wapi makundi yao?”
17 Et l’homme dit: « Ils sont partis d’ici; car je les ai entendus dire: Allons à Dothaïn. » Joseph alla après ses frères, et il les trouva à Dothaïn.
Yule mtu akajibu, “Wamehama hapa. Nilisikia wakisema, ‘Twende Dothani.’” Kwa hiyo Yosefu akawafuatilia ndugu zake na kuwakuta karibu na Dothani.
18 Ils l’aperçurent de loin et, avant qu’il fût près d’eux, ils complotèrent de le faire mourir.
Ndugu zake walipomwona akiwa mbali, kabla hajawafikia, wakapanga shauri baya la kumuua.
19 Ils se dirent l’un à l’autre: « Voici l’homme aux songes; c’est bien lui qui arrive.
Wakaambiana, “Yule mwota ndoto anakuja!
20 Venez donc, tuons-le et jetons-le dans une des citernes, et nous dirons qu’une bête féroce l’a dévoré; nous verrons ce qui en sera de ses songes! »
Njooni sasa, tumuue na kumtupa katika shimo mojawapo na tuseme kwamba mnyama mkali amemrarua. Kisha tutaona matokeo ya ndoto zake.”
21 Ruben entendit et il le délivra de leurs mains. Il dit: « Ne le frappons pas à mort. »
Reubeni aliposikia jambo hili, akajaribu kumwokoa kutoka mikononi mwao akasema, “Tusiutoe uhai wake.
22 Ruben leur dit: « Ne versez pas le sang; jetez-le dans cette citerne qui est dans le désert, et ne portez pas la main sur lui. » — Son dessein était de le délivrer de leurs mains, pour le faire retourner vers son père. —
Tusimwage damu yoyote. Mtupeni katika shimo lililoko hapa jangwani, lakini msimguse.” Reubeni alisema hivyo ili amwokoe kutoka mikononi mwao, kisha amrudishe nyumbani kwa baba yake.
23 Lorsque Joseph arriva auprès de ses frères, ils le dépouillèrent de sa robe, de la robe longue qu’il portait;
Kwa hiyo Yosefu alipowafikia ndugu zake, walimvua lile joho lake, lile joho lililorembwa vizuri alilokuwa amevaa.
24 et, l’ayant pris, ils le jetèrent dans la citerne. Cette citerne était vide: il n’y avait pas d’eau.
Kisha wakamchukua wakamtupa katika shimo. Wakati huo shimo lilikuwa tupu, halikuwa na maji ndani yake.
25 Puis ils s’assirent pour manger. Levant les yeux, ils virent, et voici qu’une caravane d’Ismaélites venait de Galaad; leurs chameaux étaient chargés d’astragale, de baume et de ladanum, qu’ils transportaient en Égypte.
Walipokaa ili wale chakula chao, wakainua macho wakaona msafara wa Waishmaeli ukija kutoka Gileadi. Ngamia wao walikuwa wamepakizwa mizigo ya vikolezo, uvumba na manemane, nao walikuwa njiani kuvipeleka Misri.
26 Alors Juda dit à ses frères: « Que gagnerons-nous à tuer notre frère et à cacher son sang?
Yuda akawaambia ndugu zake, “Tutafaidi nini ikiwa tutamuua ndugu yetu na kuificha damu yake?
27 Allons le vendre aux Ismaélites et ne portons pas la main sur lui; car il est notre frère, notre chair. » Ses frères l’écoutèrent
Njooni, tumuuze kwa hawa Waishmaeli. Tusimguse, kwa kuwa hata hivyo yeye ni ndugu yetu, nyama yetu na damu yetu wenyewe.” Ndugu zake wakakubali.
28 et, quand les marchands madianites passèrent, ils tirèrent Joseph et le firent remonter de la citerne; et ils le vendirent pour vingt pièces d’argent aux Ismaélites, qui l’emmenèrent en Égypte.
Kwa hiyo wale wafanyabiashara Wamidiani walipofika pale, ndugu zake wakamtoa Yosefu kutoka kwenye lile shimo, na kumuuza kwa shekeli ishirini za fedha kwa wale Waishmaeli, ambao walimpeleka Misri.
29 Ruben revint à la citerne, et voici que Joseph n’était plus dans la citerne.
Reubeni aliporudi kutazama kwenye lile shimo na kuona kwamba Yosefu hayupo, alirarua nguo zake.
30 Il déchira ses vêtements et, étant retourné vers ses frères, il dit: « L’enfant n’y est plus, et moi, où irai-je? »
Akawarudia ndugu zake na kusema, “Kijana hayuko mle! Nielekee wapi sasa?”
31 Ils prirent alors la robe de Joseph et, ayant tué un bouc, ils plongèrent la robe dans le sang.
Kisha wakalichukua lile joho la Yosefu, wakachinja mbuzi na kulichovya katika damu.
32 Et ils envoyèrent à leur père la longue robe, en lui faisant dire: « Voilà ce que nous avons trouvé; reconnais si c’est la robe de ton fils, ou non. »
Wakalichukua lile joho lililorembwa vizuri na kulipeleka kwa baba yao na kusema, “Tumeliokota hili joho. Uchunguze uone kama ni la mwanao.”
33 Jacob la reconnut et dit: « C’est la robe de mon fils! Une bête féroce l’a dévoré! Joseph a été mis en pièces! »
Baba yao akalitambua akasema, “Hili ni joho la mwanangu! Mnyama mkali amemrarua. Hakika Yosefu ameraruliwa vipande vipande.”
34 Et il déchira ses vêtements, mit un sac sur ses reins et fit le deuil de son fils pendant longtemps.
Kisha Yakobo akararua nguo zake, akavaa nguo ya gunia na kumwombolezea mwanawe kwa siku nyingi.
35 Tous ses fils et toutes ses filles vinrent pour le consoler; mais il refusa d’être consolé; il disait: « Je descendrai dans le deuil vers mon fils au séjour des morts. » Et son père le pleura. (Sheol )
Wanawe wote na binti zake wakaja kumfariji, lakini hakukubali kufarijiwa. Akasema, “Hapana, nitamwombolezea mwanangu mpaka nimfikie kaburini.” Kwa hiyo baba yake akaendelea kumlilia. (Sheol )
36 Les Madianites le vendirent en Égypte à Putiphar, officier de Pharaon, chef des gardes.
Wakati ule ule, Wamidiani wakamuuza Yosefu huko Misri kwa Potifa, mmojawapo wa maafisa wa Farao, aliyekuwa mkuu wa ulinzi.