< Genèse 11 >

1 Toute la terre avait une seule langue et les mêmes mots.
Wakati huo dunia yote ilikuwa na lugha moja na msemo mmoja.
2 Étant partis de l’Orient, les hommes trouvèrent une plaine dans le pays de Sennaar, et ils s’y établirent.
Watu walipoelekea upande wa mashariki, wakafika kwenye tambarare katika nchi ya Shinari nao wakaishi huko.
3 Ils se dirent entre eux: « Allons, faisons des briques, et cuisons-les au feu. » Et ils se servirent de briques au lieu de pierres, et de bitume au lieu de ciment.
Wakasemezana wao kwa wao, “Njooni, tufyatue matofali na tuyachome vizuri kwa moto.” Walitumia matofali badala ya mawe, na lami kwa ajili ya kushikamanishia hayo matofali.
4 Ils dirent encore: « Allons, bâtissons-nous une ville et une tour dont le sommet soit dans le ciel, et faisons-nous un monument, de peur que nous ne soyons dispersés sur la face de toute la terre. »
Ndipo wakasema, “Njooni, tujijengee mji wenye mnara ambao utafika hadi mbinguni, ili tujipatie jina tusije tukatawanyika usoni pa dunia yote.”
5 Mais Yahweh descendit pour voir la ville et la tour que bâtissaient les fils des hommes.
Lakini Bwana akashuka ili auone mji na mnara ambao wanadamu waliokuwa wanaujenga.
6 Et Yahweh dit: « Voici, ils sont un seul peuple et ils ont pour eux tous une même langue; et cet ouvrage est le commencement de leurs entreprises; maintenant rien ne les empêchera d’accomplir leurs projets.
Bwana akasema, “Ikiwa kama taifa moja wanaozungumza lugha moja wameanza kufanya hili, basi hakuna lolote watakalopanga kufanya ambalo halitawezekana kwao.
7 Allons, descendons, et là même confondons leur langage, de sorte qu’ils n’entendent plus le langage les uns des autres. »
Njooni, tushuke tuvuruge lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”
8 C’est ainsi que Yahweh les dispersa de là sur la face de toute la terre, et ils cessèrent de bâtir la ville.
Hivyo Bwana akawatawanya kutoka mahali pale kwenda katika dunia yote, nao wakaacha kuujenga huo mji.
9 C’est pourquoi on lui donna le nom de Babel, car c’est là que Yahweh confondit le langage de toute la terre, et c’est de là que Yahweh les a dispersés sur la face de toute la terre.
Ndiyo maana pakaitwa Babeli, kwa sababu hapo ndipo Bwana alipoivuruga lugha ya dunia nzima. Kutoka hapo Bwana akawatawanya katika uso wa dunia yote.
10 Voici l’histoire de Sem: Sem, âgé de cent ans, engendra Arphaxad, deux ans après le déluge.
Hivi ndivyo vizazi vya Shemu. Miaka miwili baada ya gharika, Shemu alipokuwa na miaka 100, akamzaa Arfaksadi.
11 Après qu’il eut engendré Arphaxad, Sem vécut cinq cents ans, et il engendra des fils et des filles.
Baada ya kumzaa Arfaksadi, Shemu aliishi miaka 500, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
12 Arphaxad vécut trente-cinq ans, et il engendra Salé
Wakati Arfaksadi alipokuwa na miaka thelathini na mitano, akamzaa Shela.
13 Après qu’il eut engendré Salé, Arphaxad vécut quatre cent trois ans, et il engendra des fils et des filles.
Baada ya Arfaksadi kumzaa Shela, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
14 Salé vécut trente ans, et il engendra Héber.
Shela alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Eberi.
15 Après qu’il eut engendré Héber, Salé vécut quatre cent trois ans, et il engendra des fils et des filles.
Shela baada ya kumzaa Eberi, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
16 Héber vécut trente-quatre ans, et il engendra Phaleg.
Eberi alipokuwa na miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
17 Après qu’il eut engendré Phaleg, Héber vécut quatre cent trente ans, et il engendra des fils et des filles.
Baada ya Eberi kumzaa Pelegi, aliishi miaka 430, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
18 Phaleg vécut trente ans, et il engendra Réü.
Pelegi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Reu.
19 Après qu’il eut engendré Réü, Phaleg vécut deux cent neuf ans, et il engendra des fils et des filles.
Baada ya Pelegi kumzaa Reu, aliishi miaka 209, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
20 Réü vécut trente-deux ans, et il engendra Sarug.
Reu alipokuwa na miaka thelathini na miwili, akamzaa Serugi.
21 Après qu’il eut engendré Sarug, Réü vécut deux cent sept ans, et il engendra des fils et des filles.
Baada ya Reu kumzaa Serugi, aliishi miaka 207, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
22 Sarug vécut trente ans, et il engendra Nachor.
Serugi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Nahori.
23 Après qu’il eut engendré Nachor, Sarug vécut deux cents ans, et il engendra des fils et des filles.
Baada ya Serugi kumzaa Nahori, aliishi miaka 200, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
24 Nachor vécut vingt-neuf ans, et il engendra Tharé.
Nahori alipokuwa na miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
25 Après qu’il eut engendré Tharé, Nachor vécut cent dix-neuf ans, et il engendra des fils et des filles.
Baada ya Nahori kumzaa Tera, aliishi miaka 119, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
26 Tharé vécut soixante-dix ans, et il engendra Abram, Nachor et Aran.
Tera alipokuwa na miaka sabini, akamzaa Abramu, Nahori na Harani.
27 Voici l’histoire de Tharé. Tharé engendra Abram, Nachor et Aran. Aran engendra Lot.
Hawa ndio wazao wa Tera. Tera aliwazaa Abramu, Nahori na Harani. Harani akamzaa Loti.
28 Et Aran mourut en présence de Tharé, son père, au pays de sa naissance, à Ur en Chaldée.
Tera alipokuwa bado hai, Harani akafa huko Uru ya Wakaldayo, nchi alimozaliwa.
29 Abram et Nachor prirent des femmes: le nom de la femme d’Abram était Saraï, et le nom de la femme de Nachor était Melcha, fille d’Aran, père de Melcha et père de Jesca.
Abramu na Nahori walioa. Mke wa Abramu aliitwa Sarai, na mke wa Nahori aliitwa Milka; Milka na Iska walikuwa watoto wa Harani.
30 Or Saraï fut stérile: elle n’avait point d’enfants.
Sarai alikuwa tasa, hakuwa na watoto.
31 Tharé prit Abram, son fils, et Lot, fils d’Aran, son petit-fils, et Saraï, sa belle-fille, femme d’Abram, son fils, et ils sortirent ensemble d’Ur des Chaldéens, pour aller au pays de Chanaan; mais, arrivés à Haran, ils s’y établirent.
Tera akamchukua Abramu mwanawe, Loti mwana wa Harani mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka kwa pamoja katika Uru ya Wakaldayo kwenda nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani, wakaishi huko.
32 Les jours de Tharé furent de deux cent cinq ans, et Tharé mourut à Haran.
Tera alikufa huko Harani akiwa na miaka 205.

< Genèse 11 >