< Ézéchiel 8 >
1 La sixième année, au sixième mois, le cinquième jour du mois, comme j’étais assis dans ma maison, et que les anciens de Juda étaient assis devant moi, la main du Seigneur Yahweh tomba sur moi.
Katika siku ya tano ya mwezi wa sita mwaka wa sita, baada ya kupelekwa uhamishoni nilipokuwa nimeketi katika nyumba yangu na wazee wa Yuda walikuwa wameketi mbele yangu, mkono wa Bwana Mwenyezi ulikuja juu yangu.
2 Et je vis; et voici une figure qui avait l’aspect du feu; depuis ce qui paraissait ses reins jusqu’en bas, c’était du feu; et depuis ses reins jusqu’en haut, c’était comme l’aspect d’une clarté, comme l’aspect d’un métal.
Nikatazama, nikaona umbo mfano wa mwanadamu. Kutokana na kile kilichoonekana kuwa kiuno chake kuelekea chini alifanana na moto. Kuanzia kwenye kiuno kuelekea juu sura yake kama chuma kingʼaavyo kikiwa ndani ya moto.
3 Et il étendit une forme de main, et il me saisit par les boucles de mes cheveux, et l’Esprit m’enleva entre la terre et le ciel; et il m’amena à Jérusalem, en des visions divines, à l’entrée de la porte intérieure qui regarde au septentrion, où était placée l’idole de jalousie qui provoque la jalousie.
Akanyoosha kitu kilichoonekana kama mkono, akaniinua kwa kushika nywele za kichwa changu. Roho akaniinua juu kati ya nchi na mbingu nikiwa katika maono ya Mungu akanichukua mpaka Yerusalemu, kwenye ingilio la lango la upande wa kaskazini ya ukumbi wa ndani, mahali iliposimama ile sanamu ichocheayo wivu.
4 Et voici que là était la gloire du Dieu d’Israël selon l’aspect que j’avais vu dans la plaine.
Hapo mbele yangu palikuwa na utukufu wa Mungu wa Israeli, kama utukufu ule niliouona katika maono kule ua wa ndani.
5 Il me dit: « Fils de l’homme, lève donc tes yeux dans la direction du septentrion. » Et je levai mes yeux dans la direction du septentrion, et voici qu’au nord de la porte de l’autel, il y avait cette idole de jalousie, à l’entrée.
Kisha akaniambia, “Mwanadamu, tazama kuelekea kaskazini.” Hivyo nikatazama na kwenye ingilio upande wa kaskazini wa lango la madhabahu, nikaona sanamu hii ya wivu.
6 Et il me dit: « Fils de l’homme, vois-tu ce qu’ils font, les grandes abominations que la maison d’Israël commet ici, afin que je m’ éloigne de mon sanctuaire. Et tu verras encore d’autres grandes abominations. »
Ndipo akaniambia, “Mwanadamu, je, unaona yale wanayofanya, haya mambo ya machukizo kabisa nyumba ya Israeli wanayotenda hapa, ambayo yatanifanya niende mbali na mahali pangu patakatifu? Lakini utaona vitu ambavyo vinachukiza zaidi hata kuliko hivi.”
7 Et il me conduisit à l’entrée du parvis, et je vis: et voici qu’il y avait un trou dans le mur!
Kisha akanileta mpaka ingilio la ukumbi. Nikatazama, nami nikaona tundu ukutani.
8 et il me dit: « Fils de l’homme, perce donc la muraille. » Et je perçai la muraille, et voici qu’il y avait une porte.
Akaniambia, “Mwanadamu, sasa toboa kwenye ukuta huu.” Ndipo nikatoboa ule ukuta, nikaona hapo pana mlango.
9 Et il me dit: « Viens et vois les horribles abominations qu’ils commettent ici. »
Naye akaniambia, “Ingia ndani, ukaone maovu na machukizo wanayofanya humu.”
10 Et je vins et je vis: et voici qu’il y avait toutes sortes de figures de reptiles et d’animaux immondes, et toutes les horreurs de la maison d’Israël dessinées sur la muraille tout autour.
Hivyo nikaingia ndani na kutazama, nikaona kuta zote zimechorwa kila aina ya vitu vitambaavyo na ya wanyama wachukizao wa kila aina na sanamu zote za nyumba ya Israeli.
11 Et soixante-dix hommes d’entre les anciens de la maison d’Israël, parmi lesquels était Jézonias, fils de Saphan, se tenaient debout devant elles, et chacun avait à la main son encensoir, d’où s’élevait le parfum d’un nuage d’encens.
Mbele yao walisimama wazee sabini wa nyumba ya Israeli, naye Yaazania mwana wa Shafani alikuwa amesimama miongoni mwao. Kila mmoja alikuwa na chetezo mkononi na moshi wa harufu nzuri ya uvumba ulikuwa unapanda juu.
12 Et il me dit: « As-tu vu, fils de l’homme, ce que les anciens de la maison d’Israël font dans les ténèbres, chacun dans ses appartements couverts de figures, car ils disent: Yahweh ne nous voit pas; Yahweh a abandonné le pays! »
Akaniambia, “Mwanadamu, umeona wanayoyafanya wazee wa nyumba ya Israeli gizani, kila mmoja kwenye sehemu yake mwenyewe ya kufanyia ibada za sanamu yake? Wao husema, ‘Bwana hatuoni, Bwana ameiacha nchi.’”
13 Et il me dit: « Tu verras encore d’autres grandes abominations qu’ils commettent. »
Akasema tena, “Bado utaona machukizo wanayofanya ambayo ni makubwa kuliko haya.”
14 Et il me conduisit à l’entrée de la porte de la maison de Yahweh qui regarde le septentrion; et voici que les femmes y étaient assises, pleurant le dieu Thammuz.
Ndipo akanileta mpaka ingilio la lango la kaskazini la nyumba ya Bwana, nami nikaona wanawake wameketi hapo, wakimwombolezea Tamuzi.
15 Et il me dit: « As-tu vu, fils de l’homme? Tu verras encore d’autres abominations plus grandes que celles-là. »
Akaniambia, “Unaliona hili, mwanadamu? Utaona vitu ambavyo ni machukizo kuliko hili.”
16 Et il me conduisit alors dans le parvis intérieur de la maison de Yahweh; et voici qu’à l’entrée de la maison de Yahweh, entre le portique et l’autel, il y avait environ vingt-cinq hommes, le dos tourné au temple de Yahweh, et le visage vers l’orient; et ils se prosternaient à l’orient devant le soleil.
Ndipo akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani wa nyumba ya Bwana, nako huko katika ingilio la Hekalu, kati ya baraza na madhabahu, walikuwepo wanaume wapatao ishirini na watano. Wakiwa wamelipa kisogo Hekalu la Bwana na kuelekeza nyuso zao upande wa mashariki, wakilisujudia jua huko mashariki.
17 Et il me dit: « As-tu vu, fils de l’homme? Est-ce trop peu pour la maison de Juda de commettre les abominations qu’ils commettent ici? Faut-il qu’ils remplissent encore le pays de violence, et qu’ils recommencent toujours à m’irriter? Voici qu’ils portent le rameau à leur nez.
Akaniambia, “Je, umeona hili mwanadamu? Je, ni jambo dogo sana kwa nyumba ya Yuda kufanya machukizo wanayoyafanya hapa? Je, ni lazima pia waijaze nchi dhuluma na kuendelea siku zote kunikasirisha? Watazame wanavyonibania pua kana kwamba ninanuka!
18 Et moi aussi, j’agirai avec colère; mon œil n’épargnera point, et je serai sans pitié; ils crieront à haute voix à mes oreilles, et je ne les entendrai point. »
Kwa hiyo nitashughulika nao kwa hasira, sitawaonea huruma wala kuwaachilia. Wajapopiga makelele masikioni mwangu, sitawasikiliza.”