< Actes 11 >
1 Les apôtres et les frères qui étaient dans la Judée apprirent que les Gentils avaient aussi reçu la parole de Dieu.
Mitume na ndugu kule Yudea walisikia kwamba watu wa mataifa mengine pia walikuwa wamelipokea neno la Mungu.
2 Et lorsque Pierre fut remonté à Jérusalem, les fidèles de la circoncision lui adressèrent des reproches,
Basi, Petro aliporudi Yerusalemu, wale Wayahudi waumini waliopendelea watu wa mataifa mengine watahiriwe, walimlaumu wakisema:
3 en disant: « Tu es entré chez des incirconcis, et tu as mangé avec eux! »
“Wewe umekwenda kukaa na watu wasiotahiriwa na hata umekula pamoja nao!
4 Pierre, prenant la parole, se mit à leur exposer, d’une manière suivie, ce qui s’était passé.
Hapo Petro akawaeleza kinaganaga juu ya yale yaliyotendeka tangu mwanzo:
5 « J’étais en prière, dit-il, dans la ville de Joppé, et j’eus, en extase, une vision: un objet semblable à une grande nappe, tenue par les quatre coins, descendait du ciel et venait jusqu’à moi.
“Siku moja nikiwa nasali mjini Yopa, niliona maono; niliona kitu kama shuka kubwa likishushwa chini kutoka mbinguni likiwa limeshikwa pembe zake nne, likawekwa kando yangu.
6 Fixant les yeux sur cette nappe, je la considérai, et j’y vis les quadrupèdes de la terre, les bêtes sauvages, les reptiles et les oiseaux du ciel.
Nilichungulia ndani kwa makini nikaona wanyama wenye miguu minne, wanyama wa mwituni, wanyama watambaao na ndege wa angani.
7 J’entendis aussi une voix qui me disait: « Lève-toi, Pierre; tue et mange. —
Kisha nikasikia sauti ikiniambia: Petro amka, chinja, ule.
8 Je répondis: « Oh non, Seigneur, car jamais rien de profane et d’impur n’est entré dans ma bouche. —
Lakini mimi nikasema: La, Bwana; maana chochote kilicho najisi au kichafu hakijapata kamwe kuingia kinywani mwangu.
9 Pour la seconde fois une voix se fit entendre du ciel: Ce que Dieu a déclaré pur, ne l’appelle pas profane. —
Ile sauti ikasikika tena kutoka mbinguni: Usiviite najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa.
10 Cela arriva par trois fois; puis tout fut retiré dans le ciel.
Jambo hilo lilifanyika mara tatu, na mwishowe vyote vilirudishwa juu mbinguni.
11 Au même instant trois hommes se présentèrent devant la maison où nous étions; on les avait envoyés de Césarée vers moi.
Ghafla, watu watatu waliokuwa wametumwa kwangu kutoka Kaisarea waliwasili kwenye nyumba niliyokuwa nakaa.
12 L’Esprit me dit de partir avec eux sans hésiter. Les six frères que voici m’accompagnèrent, et nous entrâmes dans la maison de Corneille.
Roho aliniambia niende pamoja nao bila kusita. Hawa ndugu sita waliandamana nami pia kwenda Kaisarea na huko tuliingia nyumbani mwa Kornelio.
13 Cet homme nous raconta comment il avait vu dans sa maison l’ange se présenter à lui, en disant: Envoie à Joppé, et fais venir Simon, surnommé Pierre;
Yeye alitueleza jinsi alivyokuwa amemwona malaika amesimama nyumbani mwake na kumwambia: Mtume mtu Yopa akamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petro.
14 il te dira des paroles par lesquelles tu seras sauvé, toi et toute ta maison. —
Yeye atakuambia maneno ambayo kwayo wewe na jamaa yako yote mtaokolewa.
15 Lorsque j’eus commencé à leur parler, l’Esprit-Saint descendit sur eux, comme sur nous au commencement.
Na nilipoanza tu kuongea, Roho Mtakatifu aliwashukia kama alivyotushukia sisi pale awali.
16 Et je me souvins de cette parole du Seigneur: Jean a baptisé dans l’eau; mais vous, vous serez baptisés dans l’Esprit-Saint. —
Hapo nilikumbuka yale maneno Bwana aliyosema: Yohane alibatiza kwa maji, lakini ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.
17 Si donc Dieu leur a donné la même grâce qu’à nous, qui avons cru au Seigneur Jésus-Christ, qui étais-je, moi, pour pouvoir m’opposer à Dieu! »
Basi, kama Mungu amewapa pia watu wa mataifa mengine zawadi ileile aliyotupa sisi tulipomwamini Bwana Yesu Kristo, je, mimi ni nani hata nijaribu kumpinga Mungu?”
18 Ayant entendu ce discours, ils se calmèrent, et ils glorifièrent Dieu en disant: « Dieu a donc accordé aussi aux Gentils la pénitence, afin qu’ils aient la vie. »
Waliposikia hayo, waliacha ubishi, wakamtukuza Mungu wakisema, “Mungu amewapa watu wa mataifa mengine nafasi ya kutubu na kuwa na uzima!”
19 Cependant ceux qui avaient été dispersés par la persécution survenue à l’occasion d’Étienne, allèrent jusqu’en Phénicie, dans l’île de Chypre et à Antioche, n’annonçant la parole à personne si ce n’est aux seuls Juifs.
Kutokana na mateso yaliyotokea wakati Stefano alipouawa, waumini walitawanyika. Wengine walikwenda mpaka Foinike, Kupro na Antiokia wakihubiri ule ujumbe kwa Wayahudi tu.
20 Il y eut cependant parmi eux quelques hommes de Chypre et de Cyrène qui, étant venus à Antioche, s’adressèrent aussi aux Grecs, et leur annoncèrent le Seigneur Jésus.
Lakini baadhi ya waumini waliotoka Kupro na Kurene, walikwenda Antiokia wakautangaza huo ujumbe kwa watu wa mataifa mengine wakiwahubiria ile Habari Njema juu ya Bwana Yesu.
21 Et la main du Seigneur était avec eux, et un grand nombre de personnes crurent et se convertirent au Seigneur.
Bwana aliwasaidia na idadi kubwa ya watu iliamini na kumgeukia Bwana.
22 Le bruit en étant venu aux oreilles des fidèles de l’Église de Jérusalem, ils envoyèrent Barnabé jusqu’à Antioche.
Habari ya jambo hilo ikasikika kwa lile kanisa la Yerusalemu. Hivyo wakamtuma Barnaba aende Antiokia.
23 Lorsqu’il fut arrivé et qu’il eut vu la grâce de Dieu, il s’en réjouit, et il les exhorta tous à demeurer d’un cœur ferme dans le Seigneur.
Alipofika huko na kuona jinsi Mungu alivyowaneemesha wale watu, alifurahi na kuwahimiza wote wadumu katika uaminifu wao kwa Bwana.
24 Car c’était un homme de bien rempli de l’Esprit-Saint, et de foi. Et une foule assez considérable se joignit au Seigneur.
Barnaba alikuwa mtu mwema na mwenye kujaa Roho Mtakatifu na imani. Kundi kubwa la watu lilivutwa kwa Bwana.
25 Barnabé se rendit ensuite à Tarse pour chercher Saul, et l’ayant trouvé, il l’amena à Antioche.
Kisha, Barnaba alikwenda Tarso kumtafuta Saulo
26 Or, il advint que, pendant une année entière, ils tinrent des réunions dans cette église et instruisirent une multitude nombreuse. Ce fut ainsi à Antioche que, pour la première fois, les disciples reçurent le nom de Chrétiens.
Alipompata, alimleta Antiokia. Nao wote wawili walikaa na lile kanisa kwa mwaka wote mzima wakifundisha kundi kubwa la watu. Huko Antiokia, ndiko, kwa mara ya kwanza, wafuasi waliitwa Wakristo.
27 En ces jours-là, des prophètes vinrent de Jérusalem à Antioche.
Wakati huohuo, manabii kadhaa walikuja Antiokia kutoka Yerusalemu.
28 L’un d’eux, nommé Agabus, s’étant levé, annonça par l’Esprit qu’il y aurait sur toute la terre une grande famine; elle eut lieu, en effet, sous Claude.
Basi, mmoja wao aitwaye Agabo alisimama, na kwa uwezo wa Roho akabashiri kwamba kutakuwa na njaa kubwa katika nchi yote (Njaa hiyo ilitokea wakati Klaudio alipokuwa akitawala).
29 Les disciples décidèrent d’envoyer, chacun selon ses moyens, un secours aux frères qui habitaient la Judée:
Wale wanafunzi waliamua kila mmoja kwa kadiri ya uwezo wake apeleke chochote ili kuwasaidia wale ndugu waliokuwa wanaishi Yudea.
30 ce qu’ils firent. Ce secours fut envoyé aux Anciens par les mains de Barnabé et de Saul.
Basi, wakafanya hivyo na kupeleka mchango wao kwa wazee wa kanisa kwa mikono ya Barnaba na Saulo.