< 2 Corinthiens 9 >
1 Pour ce qui est de l’assistance destinée aux saints, il est superflu de vous en écrire;
Si lazima kuandika zaidi kuhusu huduma hiyo yenu kwa ajili ya watu wa Mungu.
2 car je connais votre bonne volonté, et je m’en fais gloire pour vous auprès des Macédoniens, leur disant que, dès l’année passée, l’Achaïe est prête. Ce zèle dont vous donnez l’exemple en a stimulé un grand nombre.
Ninajua jinsi mlivyo na moyo wa kusaidia, na nilijivuna juu yenu kuhusu jambo hilo mbele ya watu wa Makedonia. Niliwaambia: “Ndugu zetu wa Akaya wako tayari tangu mwaka jana.” Hivyo, moto wenu umekwisha wahimiza watu wengi zaidi.
3 Toutefois, je vous ai envoyé les frères, afin que l’éloge que j’ai fait de vous ne soit pas démenti sur ce point, et que vous soyez prêts, comme j’ai affirmé que vous le seriez.
Basi, nimewatuma ndugu zetu hao, ili fahari yetu juu yenu ionekane kwamba si maneno matupu, na kwamba mko tayari kabisa na msaada wenu kama nilivyosema.
4 Prenez-y garde: si des Macédoniens venaient avec moi et ne vous trouvaient pas prêts, quelle confusion pour moi, — pour ne pas dire pour vous, — dans une telle assurance!
Isije ikawa kwamba watu wa Makedonia watakapokuja pamoja nami tukawakuta hamko tayari, hapo sisi tutaaibika—bila kutaja aibu mtakayopata ninyi wenyewe—kwa sababu tutakuwa tumewatumainia kupita kiasi.
5 J’ai donc jugé nécessaire de prier nos frères de nous devancer chez vous, et d’organiser à temps votre libéralité déjà promise, afin qu’elle soit prête, mais comme une libéralité, et non comme une lésinerie.
Kwa hiyo, nimeona ni lazima kuwaomba hawa ndugu watutangulie kuja kwenu, wapate kuweka tayari zawadi yenu kubwa mliyoahidi; nayo ionyeshe kweli kwamba ni zawadi iliyotolewa kwa hiari na si kwa kulazimishwa.
6 Je vous le dis, celui qui sème peu moissonnera peu, et celui qui sème abondamment moissonnera abondamment.
Kumbukeni: “Apandaye kidogo huvuna kidogo; apandaye kwa wingi huvuna kwa wingi.”
7 Que chacun donne, comme il l’a résolu en son cœur, non avec regret ni par contrainte; car “Dieu aime celui qui donne avec joie.”
Kila mmoja, basi, na atoe kadiri alivyoamua, kwa moyo na wala si kwa huzuni au kwa kulazimishwa, maana Mungu humpenda yule mwenye kutoa kwa furaha.
8 Il est puissant pour vous combler de toutes sortes de grâces, afin que, ayant toujours en toutes choses de quoi satisfaire à tous vos besoins, il vous en reste encore abondamment pour toute espèce de bonnes œuvres,
Mungu anaweza kuwapeni ninyi zaidi ya yale mnayoyahitaji, mpate daima kuwa na kila kitu mnachohitaji, na hivyo mzidi kusaidia katika kila kazi njema.
9 selon qu’il est écrit: “Avec largesse, il a donné aux pauvres; sa justice subsiste à jamais.” (aiōn )
Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Yeye hutoa kwa ukarimu, huwapa maskini, wema wahudumu milele.” (aiōn )
10 Celui qui fournit la semence au semeur et du pain pour sa nourriture, vous fournira la semence à vous aussi, et la multipliera, et il fera croître les fruits de votre justice;
Na Mungu ampaye mkulima mbegu na mkate kwa chakula, atawapa ninyi pia mbegu mnazohitaji, na atazifanya ziote, ziwe na kuwapa mavuno mengi ya ukarimu wenu.
11 et vous serez ainsi enrichis à tous égards, pour donner d’un cœur simple ce qui, recueilli par nous, fera offrir à Dieu des actions de grâces.
Yeye atawatajirisha ninyi daima kwa kila kitu, ili watu wapate kumshukuru Mungu kwa ajili ya zawadi zenu wanazozipokea kwa mikono yetu.
12 Car la dispensation de cette libéralité ne pourvoit pas seulement en abondance aux besoins des saints, mais elle est encore une riche source de nombreuses actions de grâces envers Dieu.
Maana huduma hii takatifu mnayoifanya si tu kwamba itasaidia mahitaji ya watu wa Mungu, bali pia itasababisha watu wengi wamshukuru Mungu.
13 À cause de la vertu éprouvée que cette offrande montre en vous, ils glorifient Dieu de votre obéissance dans la profession de l’Évangile du Christ, et de la simplicité avec laquelle vous faites part de vos dons à eux et à tous.
Kutokana na uthibitisho unaoonyeshwa kwa huduma hii yetu, watu watamtukuza Mungu kwa sababu ya uaminifu wenu kwa Habari Njema ya Kristo mnayoiungama, na pia kwa sababu ya ukarimu mnaowapa wao na watu wote.
14 Ils prient aussi pour vous, vous aimant d’un tendre amour, à cause de la grâce éminente que Dieu a mise en vous.
Kwa hiyo watawaombea ninyi kwa moyo kwa sababu ya neema ya pekee aliyowajalieni Mungu.
15 Grâces soient rendues à Dieu pour son don ineffable!
Tumshukuru Mungu kwa ajili ya zawadi yake isiyo na kifani!