< 1 Thessaloniciens 4 >
1 Au reste, frères, nous vous en prions et supplions par le Seigneur Jésus; vous avez appris de nous comment il faut se conduire pour plaire à Dieu, (et ainsi vous le faites); marchez donc de progrès en progrès.
Hatimaye, ndugu zangu, mmejifunza kutoka kwetu namna mnavyopaswa kuishi ili kumpendeza Mungu. Na kweli mmekuwa mnaishi hivyo. Sasa tunawaombeni na kuwasihi kwa jina la Bwana Yesu mfanye vema zaidi.
2 Vous connaissez en effet les préceptes que nous vous avons donnés de la part du Seigneur Jésus.
Maana mnayajua yale maagizo tuliyowapeni kwa mamlaka ya Bwana Yesu.
3 Car ce que Dieu veut, c’est votre sanctification: c’est que vous évitiez l’impudicité,
Mungu anataka ninyi muwe watakatifu na mjiepushe kabisa na maisha ya zinaa.
4 et que chacun de vous sache garder son corps dans la sainteté et l’honnêteté,
Kila mwanamume anapaswa kujua namna ya kuishi na mkewe kwa utakatifu na heshima,
5 sans l’abandonner aux emportements de la passion, comme font les païens qui ne connaissent pas Dieu;
na si kwa tamaa mbaya kama watu wa mataifa mengine wasiomjua Mungu.
6 c’est que personne en cette matière n’use de violence ou de fraude à l’égard de son frère, parce que le Seigneur fait justice de tous ces désordres, comme nous vous l’avons déjà dit et attesté.
Basi, mtu yeyote asimkosee au kumpunja mwenzake kuhusu jambo hili. Tulikwisha waambieni hayo na kuwaonya kwamba Bwana atawaadhibu wanaofanya mambo hayo.
7 Car Dieu ne nous a pas appelés à l’impureté, mais à la sainteté.
Mungu hakutuita tuishi maisha ya zinaa, bali tuishi katika utakatifu.
8 Celui donc qui méprise ces préceptes, ce n’est pas un homme qu’il méprise, mais Dieu, qui a aussi donné son Esprit-Saint pour habiter en vous.
Kwa hiyo basi, anayedharau mafundisho hayo hamdharau mtu, bali amdharau Mungu mwenyewe anayewapeni Roho wake Mtakatifu.
9 Pour ce qui est de la charité fraternelle, il n’est pas besoin de vous en écrire; car vous-mêmes avez appris de Dieu à vous aimer les uns les autres;
Hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya kuwapenda ndugu zenu waumini. Ninyi wenyewe mmefundishwa na Mungu namna mnavyopaswa kupendana.
10 aussi bien le pratiquez-vous envers tous les frères par toute la Macédoine. Mais nous vous exhortons, frères, à le pratiquer toujours mieux.
Na mmekuwa mkiwatendea hivyo ndugu zenu wote kila mahali katika Makedonia. Basi, ndugu tunawaombeni mfanye hata zaidi.
11 Appliquez-vous à vivre en repos, à vous occuper de vos propres affaires et à travailler de vos mains, comme nous vous l’avons recommandé,
Muwe na nia ya kuishi maisha ya utulivu, kila mmoja ashughulikie mambo yake mwenyewe na afanye kazi kwa mikono yake mwenyewe kama tulivyowaagiza pale awali.
12 de telle sorte que vous teniez une conduite honnête aux yeux de ceux du dehors, sans avoir besoin de personne.
Kwa namna hiyo mtajipatia sifa nzuri kutoka kwa wale wasio Wakristo, na hamtakuwa na lazima ya kuwategemea wengine kwa mahitaji yenu.
13 Mais nous ne voulons pas, frères, que vous soyez dans l’ignorance au sujet de ceux qui se sont endormis, afin que vous ne vous affligiez pas, comme les autres hommes qui n’ont pas d’espérance.
Ndugu, twataka mjue ukweli kuhusu wale ambao wamekwisha fariki dunia, ili msipatwe na huzuni kama watu wengine wasio na matumaini.
14 Car si nous croyons que Jésus est mort et qu’il est ressuscité, croyons aussi que Dieu amènera avec Jésus ceux qui se sont endormis en lui.
Sisi tunaamini kwamba Yesu alikufa, akafufuka; na hivyo sisi tunaamini kwamba Mungu atawaleta pamoja na Yesu wale wote waliofariki wakiwa wanamwamini.
15 Voici, en effet, ce que nous vous déclarons d’après la parole du Seigneur: Nous, les vivants, laissés pour l’avènement du Seigneur, nous ne devancerons pas ceux qui se sont endormis.
Hili tunalowaambieni ni fundisho la Bwana; sisi tulio hai, ambao tutakuwa tumebaki, wakati Bwana atakapokuja, hakika hatutawatangulia wale waliokwisha fariki dunia.
16 Car, au signal donné, à la voix de l’archange, au son de la trompette divine, le Seigneur lui-même descendra du ciel, et ceux qui sont morts dans le Christ ressusciteront d’abord.
Maana patatolewa amri, sauti ya malaika mkuu, sauti ya tarumbeta ya Mungu, naye Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni. Ndipo wale waliokufa wakiwa wanamwamini Kristo watafufuliwa kwanza.
17 Puis nous, qui vivons, qui sommes restés, nous serons emportés avec eux sur les nuées à la rencontre du Seigneur dans les airs, et ainsi nous serons pour toujours avec le Seigneur.
Kisha sisi tulio hai wakati huo tutakusanywa pamoja nao katika mawingu kumlaki Bwana hewani. Na hivyo tutakuwa daima pamoja na Bwana.
Basi, farijianeni kwa maneno haya.