< 1 Samuel 23 >
1 On vint dire à David: « Voici que les Philistins attaquent Céïla et pillent les aires. »
Daudi alipoambiwa kuwa, “Tazama, Wafilisti wanapigana dhidi ya Keila nao wanapokonya nafaka katika sakafu za kupuria,”
2 David consulta Yahweh, en disant: « Irai-je et battrai-je ces Philistins? » Et Yahweh répondit à David: « Va, tu battras les Philistins et tu délivreras Céïla. »
akauliza kwa Bwana, akisema, “Je, niende na kuwashambulia hawa Wafilisti?” Bwana akamjibu, “Nenda, washambulie Wafilisti na uuokoe Keila.”
3 Mais les hommes de David lui dirent: « Voici que, en Juda, nous sommes dans la crainte; combien plus si nous allons à Céïla contre les troupes des Philistins? »
Lakini watu wa Daudi wakamwambia, “Hapa Yuda kwenyewe tunaogopa. Si zaidi sana, kama tukienda Keila dhidi ya majeshi ya Wafilisti!”
4 David consulta de nouveau Yahweh, et Yahweh lui répondit en ces termes: « Lève-toi, descends à Céïla, car je livre les Philistins entre tes mains. »
Daudi akauliza kwa Bwana tena, naye Bwana akamjibu akamwambia, “Shuka uende Keila, kwa kuwa nitawatia Wafilisti mkononi mwako.”
5 David alla donc avec ses hommes à Céïla, et attaqua les Philistins; il emmena leur bétail et leur fit éprouver une grande défaite. C’est ainsi que David délivra les habitants de Céïla.
Basi Daudi na watu wake wakaenda Keila, wakapigana na Wafilisti na kutwaa wanyama wao wa kutosha. Daudi akawatia hasara kubwa Wafilisti na kuwaokoa watu wa Keila.
6 Or quand Abiathar, fils d’Achimélech, s’enfuit vers David à Céïla, il descendit ayant en main l’éphod.
(Basi Abiathari mwana wa Ahimeleki alikuwa ameleta kisibau alipokimbilia kwa Daudi huko Keila.)
7 On annonça à Saül que David était allé à Céïla, et Saül dit: « Dieu le livre entre mes mains, car il s’est enfermé en venant dans une ville qui a des portes et des barres. »
Sauli akaambiwa kwamba Daudi alikuwa amekwenda Keila, naye akasema, “Mungu amemtia mkononi mwangu, kwa kuwa Daudi amejifunga mwenyewe kwa kuingia kwenye mji wenye malango na makomeo.”
8 Et Saül convoqua tout le peuple à la guerre, afin de descendre à Céïla et d’assiéger David et ses hommes.
Naye Sauli akayaita majeshi yake yote yaende vitani, kuishukia Keila ili kumzingira Daudi na watu wake kwa jeshi.
9 Mais David, ayant su que Saül préparait le mal contre lui, dit au prêtre Abiathar: « Apporte l’éphod. »
Daudi alipojua kuwa Sauli alikuwa ana hila dhidi yake, akamwambia Abiathari kuhani, “Leta kile kisibau.”
10 Et David dit: « Yahweh, Dieu d’Israël, votre serviteur a appris que Saül cherche à venir à Céïla, pour détruire la ville à cause de moi.
Daudi akasema, “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mtumishi wako amesikia kwa hakika kwamba Sauli anapanga kuja Keila na kuangamiza mji kwa ajili yangu.
11 Les habitants de Céïla me livreront-ils entre ses mains? Saül descendra-t-il, comme votre serviteur l’a entendu dire? Yahweh, Dieu d’Israël, daignez le révéler à votre serviteur. » Yahweh répondit: « Il descendra. »
Je, watu wa Keila watanisalimisha kwake? Je, Sauli atateremka, kama mtumishi wako alivyosikia? Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mwambie mtumishi wako.” Naye Bwana akasema, “Ndiyo, atashuka.”
12 Et David dit: « Les habitants de Céïla me livreront-ils, moi et mes hommes, entre les mains de Saül? » Yahweh répondit: « Ils te livreront. »
Daudi akauliza tena, “Je watu wa Keila watanisalimisha mimi pamoja na watu wangu kwa Sauli?” Naye Bwana akasema, “Ndiyo, watafanya hivyo.”
13 Alors David se leva avec ses gens au nombre d’ environ six cents hommes; ils sortirent de Céïla, et ils allaient et venaient à l’aventure. Informé que David s’était enfui de Céïla, Saül suspendit sa marche.
Basi Daudi na watu wake, wapatao 600, wakaondoka Keila wakawa wanakwenda sehemu moja hadi nyingine. Sauli alipoambiwa Daudi ametoroka kutoka Keila, hakwenda huko.
14 David demeura au désert, dans les lieux forts, et il resta dans la montagne au désert de Ziph. Saül le cherchait tous les jours, mais Dieu ne le livra pas entre ses mains.
Daudi akakaa katika ngome za jangwani na katika vilima vya Jangwa la Zifu. Siku baada ya siku Sauli aliendelea kumsaka, lakini Mungu hakumtia Daudi mikononi mwake.
15 David sut que Saül s’était mis en campagne pour lui ôter la vie: David se tenait au désert de Ziph, dans la forêt;
Daudi alipokuwa huko Horeshi katika Jangwa la Zifu, akajua kuwa Sauli alikuwa amekuja ili amuue.
16 et Jonathas, fils de Saül, se leva et alla vers David dans la forêt. Il fortifia sa main en Dieu et lui dit:
Naye Yonathani mwana wa Sauli akamwendea Daudi huko Horeshi na kumtia moyo kusimama imara katika imani yake kwa Mungu.
17 « Ne crains rien, car la main de Saül, mon père, ne t’atteindra pas. Toi, tu régneras sur Israël, et moi, je serai le second après toi; Saül, mon père, le sait bien aussi. »
Akamwambia, “Usiogope, Daudi; baba yangu Sauli hatakutia mkononi mwake. Utakuwa mfalme juu ya Israeli, nami nitakuwa wa pili wako. Hata baba yangu Sauli anajua hili.”
18 Ils firent tous deux alliance devant Yahweh; et David resta dans la forêt, et Jonathas retourna chez lui.
Wote wawili wakaweka agano mbele za Bwana. Kisha Yonathani akaenda zake nyumbani, lakini Daudi akabaki Horeshi.
19 Les Ziphiens montèrent vers Saül à Gabaa, et dirent: « David est caché parmi nous dans des lieux forts, dans la forêt, sur la colline de Hachila, qui est au midi de la lande.
Basi Wazifu wakakwea kwa Sauli huko Gibea na kusema, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu katika ngome huko Horeshi, katika kilima cha Hakila, kusini mwa Yeshimoni?
20 Descends donc, ô roi, comme toute ton âme le désire; c’est à nous de le livrer entre les mains du roi. »
Sasa, ee mfalme, uteremke wakati wowote unapoona vyema kufanya hivyo, sisi tutawajibika kumkabidhi kwa mfalme.”
21 Saül dit: « Soyez bénis de Yahweh, de ce que vous avez eu pitié de moi!
Sauli akajibu, “Bwana awabariki kwa kunifikiria.
22 Allez, je vous prie, assurez-vous encore, sachez et voyez en quel lieu il porte ses pas et qui l’a vu là; car il est, m’a-t-on dit, fort rusé.
Nendeni mkafanye maandalizi zaidi. Mkajue mahali ambapo Daudi huenda mara kwa mara na nani amepata kumwona huko. Wananiambia yeye ni mwerevu sana.
23 Voyez et sachez toutes les retraites où il se cache; puis revenez vers moi avec des renseignements certains, et j’irai avec vous. S’il est dans le pays, je le chercherai parmi tous les milliers de Juda. »
Jueni kila mahali anapojificha mrudi na kunipa taarifa kamili. Kisha nitakwenda pamoja nanyi; kama atakuwa katika eneo hilo, nitamsaka miongoni mwa koo zote za Yuda.”
24 Ils se levèrent donc et allèrent à Ziph, avant Saül. Mais David et ses hommes s’étaient retirés au désert de Maon, dans la plaine, au midi de la lande.
Basi wakaondoka na kwenda mpaka Zifu wakimtangulia Sauli. Naye Daudi na watu wake walikuwa katika Jangwa la Maoni, katika Araba kusini mwa Yeshimoni.
25 Saül partit avec ses hommes à la recherche de David. David, l’ayant appris, descendit au rocher et resta dans le désert de Maon. Saül en fut informé et poursuivit David dans le désert de Maon;
Sauli na watu wake wakaanza msako, naye Daudi alipoelezwa hili, akateremka mpaka mwambani na kukaa katika Jangwa la Maoni. Sauli aliposikia hili, akaenda katika Jangwa la Maoni akimfuata Daudi.
26 Saül marchait d’un côté de la montagne, et David avec ses hommes de l’autre côté de la montagne; David se hâtait pour échapper à Saül, tandis que Saül et ses hommes cernaient David et ses hommes pour s’emparer d’eux.
Sauli alikuwa akienda upande mmoja wa mlima, naye Daudi na watu wake walikuwa upande mwingine wa mlima, wakiharakisha kumkimbia Sauli. Wakati Sauli na majeshi yake walipokaribia kumkamata Daudi na watu wake,
27 Un messager vint vers Saül en disant: « Hâte-toi de venir, car les Philistins ont fait invasion dans le pays. »
mjumbe alikuja kwa Sauli, akisema, “Njoo haraka! Wafilisti wanaishambulia nchi.”
28 Saül cessa de poursuivre David, et s’en alla à la rencontre des Philistins. C’est pourquoi on appela ce lieu Séla-Hammachleqoth.
Ndipo Sauli akarudi akaacha kumfuata Daudi na kwenda kukabiliana na Wafilisti. Ndiyo sababu wanaiita sehemu hii Sela-Hamalekothi.
29 David monta de là et s’établit dans les lieux forts d’Engaddi.
Naye Daudi akakwea kutoka huko na kuishi katika ngome za En-Gedi.