< 1 Corinthiens 12 >

1 Pour ce qui concerne les dons spirituels, je ne veux pas, mes frères, que vous soyez dans l’ignorance.
Ndugu, kuhusu vipaji vya kiroho, napenda mfahamu vizuri mambo haya:
2 Vous savez que, lorsque vous étiez païens, vous vous laissiez entraîner vers les idoles muettes, selon que vous y étiez conduits.
Mnajua kwamba, kabla ya kuongoka kwenu, mlitawaliwa na kupotoshwa na sanamu tupu.
3 Je vous déclare donc que personne, s’il parle par l’Esprit de Dieu, ne dit: Jésus est anathème; et personne ne peut dire: « Jésus est le Seigneur, « si ce n’est par l’Esprit-Saint.
Basi, jueni kwamba mtu yeyote anayeongozwa na Roho wa Mungu hawezi kusema: “Yesu alaaniwe!” Hali kadhalika, mtu yeyote hawezi kusema: “Yesu ni Bwana,” asipoongozwa na Roho Mtakatifu.
4 Il y a pourtant diversité de dons, mais c’est le même Esprit;
Vipaji vya kiroho ni vya namna nyingi, lakini Roho avitoaye ni mmoja.
5 diversité de ministères, mais c’est le même Seigneur;
Kuna namna nyingi za kutumikia, lakini Bwana anayetumikiwa ni mmoja.
6 diversité d’opérations, mais c’est le même Dieu qui opère tout en tous.
Kuna namna mbalimbali za kufanya kazi ya huduma, lakini Mungu ni mmoja, anayewezesha kazi zote katika wote.
7 À chacun la manifestation de l’Esprit est donnée pour l’utilité commune.
Kila mtu hupewa mwangaza wa Roho kwa faida ya wote.
8 En effet, à l’un est donnée par l’Esprit une parole de sagesse, à l’autre une parole de connaissance, selon le même Esprit;
Roho humpa mmoja ujumbe wa hekima, na mwingine ujumbe wa elimu apendavyo Roho huyohuyo.
9 à un autre, la foi, par le même Esprit; à un autre, le don des guérisons, par ce seul et même Esprit;
Roho huyohuyo humpa mmoja imani, na humpa mwingine kipaji cha kuponya;
10 à un autre, la puissance d’opérer des miracles; à un autre la prophétie; à un autre, le discernement des esprits; à un autre la diversité des langues; à un autre le don de les interpréter.
humpa mmoja kipaji cha kufanya miujiza, mwingine kipaji cha kusema ujumbe wa Mungu, mwingine kipaji cha kubainisha vipaji vitokavyo kwa Roho na visivyo vya Roho; humpa mmoja kipaji cha kusema lugha ngeni, na mwingine kipaji cha kuzifafanua.
11 Mais c’est le seul et même Esprit qui produit tous ces dons, les distribuant à chacun en particulier, comme il lui plaît.
Hizo zote ni kazi za Roho huyohuyo mmoja, ambaye humpa kila mtu kipaji tofauti, kama apendavyo mwenyewe.
12 Car, comme le corps est un et a plusieurs membres, et comme tous les membres du corps, malgré leur nombre, ne forment qu’un seul corps, ainsi en est-il du Christ.
Kama vile mwili ulivyo mmoja wenye viungo vingi, na viungo hivyo vyote—ingawaje ni vingi—hufanya mwili mmoja, ndivyo ilivyo pia kwa Kristo.
13 Tous, en effet, nous avons été baptisés dans un seul esprit pour former un seul corps, soit Juifs, soit Grecs, soit esclaves, soit libres, et nous avons tous été abreuvés d’un seul Esprit.
Maana sisi, tukiwa Wayahudi au watu wa mataifa mengine, watumwa au watu huru, sote tumebatizwa kwa Roho mmoja katika mwili huo mmoja; na sote tukanyweshwa Roho huyo mmoja.
14 Ainsi le corps n’est pas un seul membre, mais il est formé de plusieurs.
Mwili hauna kiungo kimoja tu, bali una viungo vingi.
15 Si le pied disait: « Puisque je ne suis pas main, je ne suis pas du corps », en serait-il moins du corps pour cela?
Kama mguu ungejisemea: “Kwa kuwa mimi si mkono, basi mimi si mali ya mwili”, je, ungekoma kuwa sehemu ya mwili? La hasha!
16 Et si l’oreille disait: « Puisque je ne suis pas œil, je ne suis pas du corps », en serait-elle moins du corps pour cela?
Kama sikio lingejisemea: “Kwa vile mimi si jicho, basi mimi si mali ya mwili”, je, kwa hoja hiyo lingekoma kuwa sehemu ya mwili? La!
17 Si tout le corps était œil, où serait l’ouïe? S’il était tout entier ouïe, où serait l’odorat?
Kama mwili wote ungekuwa jicho, sikio lingekuwa wapi? Na kama mwili wote ungekuwa sikio, mtu angewezaje kunusa?
18 Mais Dieu a placé chacun des membres dans le corps, comme il l’a voulu.
Lakini kama ilivyo, Mungu alizipanga sehemu hizo tofauti katika mwili kama alivyopenda.
19 Si tous étaient un seul et même membre, où serait le corps?
Kama sehemu zote zingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
20 Il y a donc plusieurs membres et un seul corps.
Ukweli ni kwamba, sehemu za mwili ni nyingi, lakini mwili ni mmoja.
21 L’œil ne peut pas dire à la main: « Je n’ai pas besoin de toi »; ni la tête dire aux pieds: « Je n’ai pas besoin de vous. »
Basi, jicho haliwezi kuuambia mkono: “Sikuhitaji wewe”, wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu: “Siwahitaji ninyi.”
22 Au contraire, les membres du corps qui paraissent les plus faibles sont plus nécessaires;
Zaidi ya hayo, inaonekana kwamba sehemu zile za mwili zinazoonekana kuwa ni dhaifu ndizo zilizo muhimu zaidi.
23 et ceux que nous tenons pour les moins honorables du corps, sont ceux que nous entourons de plus d’honneur. Ainsi nos membres les moins honnêtes, nous les traitons avec plus de décence,
Tena, viungo vile tunavyovifikiria kuwa havistahili heshima kubwa, ndivyo tunavyovitunza kwa uangalifu zaidi; viungo vya mwili ambavyo havionekani kuwa vizuri sana, huhifadhiwa zaidi,
24 tandis que nos parties honnêtes n’en ont pas besoin. Dieu a disposé le corps de manière à donner plus de respect à ce qui est moins digne,
ambapo viungo vingine havihitaji kushughulikiwa. Mungu mwenyewe ameuweka mwili katika mpango, akakipa heshima zaidi kiungo kile kilichopungukiwa heshima,
25 afin qu’il n’y ait pas de division dans le corps, mais que les membres aient également soin les uns des autres.
ili kusiweko na utengano katika mwili bali viungo vyote vishughulikiane.
26 Et si un membre souffre, tous les membres souffrent avec lui; si un membre est honoré, tous les membres s’en réjouissent avec lui.
Kama kiungo kimoja kinaumia viungo vyote huumia pamoja nacho. Kiungo kimoja kikisifiwa viungo vingine vyote hufurahi pamoja nacho.
27 Vous êtes le corps du Christ, et vous êtes ses membres, chacun pour sa part.
Basi, ninyi nyote ni mwili wa Kristo; kila mmoja wenu ni kiungo cha mwili huo.
28 Dieu a établi dans l’Église premièrement des apôtres, secondement des prophètes, troisièmement des docteurs, ensuite ceux qui ont les dons de guérir, d’assister, de gouverner, de parler diverses langues.
Mungu ameweka katika kanisa: kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu; kisha ameweka wale wenye kipaji cha kufanya miujiza, kuponya, kusaidia; viongozi na wenye kusema lugha ngeni.
29 Tous sont-ils apôtres? Tous prophètes? Tous docteurs?
Je, wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni walimu? Wote ni wenye kipaji cha kufanya miujiza?
30 Tous thaumaturges? Tous ont-ils les grâces de guérison? Tous parlent-ils des langues? Tous interprètent-ils?
Je, wote ni wenye kipaji cha kuponya? Wote ni wenye kipaji cha kusema lugha ngeni? Je, wote hufafanua lugha?
31 Aspirez aux dons supérieurs. Aussi bien je vais vous montrer une voie excellente entre toutes.
Muwe basi, na tamaa ya kupata vipaji muhimu zaidi. Nami sasa nitawaonyesheni njia bora zaidi kuliko hizi zote.

< 1 Corinthiens 12 >