< Psaumes 78 >

1 Cantique d’Asaph. Ecoute, ô mon peuple, mon enseignement; prête l’oreille aux paroles de ma bouche.
Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 Je vais ouvrir ma bouche pour dire des sentences, je publierai les mystères des temps anciens.
Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
3 Ce que nous avons entendu, ce que nous avons appris, ce que nos pères nous ont raconté,
Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
4 nous ne le cacherons pas à leurs enfants; nous dirons à la génération future les louanges de Yahweh, et sa puissance, et les prodiges qu’il a opérés.
Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
5 Il a mis une règle en Jacob, il a établi une loi en Israël, qu’il a enjoint à nos pères d’apprendre à leurs enfants,
Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
6 pour qu’elles soient connues des générations suivantes, des enfants qui naîtraient et qui se lèveraient, pour les raconter à leur tour à leurs enfants.
Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
7 Ainsi ils mettraient en Dieu leur confiance, ils n’oublieraient pas les œuvres de Dieu, et ils observeraient ses préceptes;
Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
8 ils ne seraient point, comme leurs pères, une race indocile et rebelle, une race au cœur volage, dont l’esprit n’est pas fidèle à Dieu.
Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
9 Les fils d’Ephraïm, archers habiles à tirer de l’arc, ont tourné le dos au jour du combat;
Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
10 ils n’ont pas gardé l’alliance de Dieu, ils ont refusé de marcher selon sa loi;
Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
11 ils ont mis en oubli ses grandes œuvres, et les merveilles qu’il leur avait montrées.
Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
12 Devant leurs pères, il avait fait des prodiges, au pays de l’Égypte, dans les campagnes de Tanis.
Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
13 Il ouvrit la mer pour les faire passer; Il retint les eaux dressées comme un monceau
Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
14 Il les conduisit le jour par la nuée, et toute la nuit par un feu brillant.
Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
15 Il fendit les rochers dans le désert, et il donna à boire comme des flots abondants.
Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
16 Du rocher il fit jaillir des ruisseaux, et couler l’eau par torrents.
Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
17 Mais ils continuèrent de pécher contre lui, de se révolter contre le Très-Haut dans le désert.
Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
18 Ils tentèrent Dieu dans leur cœur, en demandant de la nourriture selon leur convoitise.
Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
19 Ils parlèrent contre Dieu et dirent: « Dieu pourra-t-il dresser une table dans le désert?
Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
20 Voici qu’il a frappé le rocher, et des eaux ont coulé, et des torrents se sont répandus; pourra-t-il aussi nous donner du pain ou bien procurer de la viande à son peuple? »
Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
21 Yahweh entendit et il fut irrité, un feu s’alluma contre Jacob, et la colère s’éleva contre Israël,
Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
22 parce qu’ils n’avaient pas eu foi en Dieu et n’avaient pas espéré en son secours.
kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
23 Cependant il commanda aux nuées d’en haut, et il ouvrit les portes du ciel;
Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
24 il fit pleuvoir sur eux la manne pour les nourrir, et leur donna le froment du ciel.
Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
25 Chacun mangea le pain des forts, Il leur envoya de la nourriture à satiété.
Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
26 Il fit souffler dans le ciel le vent d’orient, il amena par sa puissance le vent du midi;
Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
27 il fit pleuvoir sur eux la viande comme de la poussière, et les oiseaux ailés comme le sable des mers.
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
28 Il les fit tomber au milieu de leur camp, autour de leurs tentes.
Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
29 Ils mangèrent et se rassasièrent à l’excès; Dieu leur donna ce qu’ils avaient désiré.
Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
30 Ils n’avaient pas encore satisfait leur convoitise, et leur nourriture était encore à leur bouche,
Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
31 quand la colère de Dieu s’éleva contre eux; il frappa de mort les mieux repus, il abattit les jeunes hommes d’Israël.
Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
32 Après tout cela, ils péchèrent encore, et n’eurent pas foi dans ses prodiges.
Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
33 Alors il dissipa leurs jours comme un souffle, et leurs années par une fin soudaine.
Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
34 Quand il les frappait de mort, ils le cherchaient, ils revenaient, empressés à retrouver Dieu,
Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
35 ils se rappelaient que Dieu était leur rocher, et le Dieu Très-Haut leur libérateur.
Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
36 Mais ils le trompaient par leurs paroles, et leur langue lui mentait;
Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
37 leur cœur n’était pas ferme avec lui, ils n’étaient pas fidèles à son alliance.
Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
38 Mais lui est miséricordieux: il pardonne le péché et ne détruit pas; souvent il retint sa colère, et ne se livra pas à toute sa fureur.
Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
39 Il se souvenait qu’ils n’étaient que chair, un souffle qui s’en va et ne revient plus.
Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
40 Que de fois ils se révoltèrent contre lui dans le désert, ils l’irritèrent dans la solitude!
Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
41 Ils ne cessèrent de tenter Dieu et de provoquer le Saint d’Israël.
Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
42 Ils ne se souvinrent plus de sa puissance, du jour où il les délivra de l’oppresseur,
Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
43 où il montra ses prodiges en Égypte, ses actions merveilleuses dans les campagnes de Tanis.
alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
44 Il changea leurs fleuves en sang, et ils ne purent boire à leurs ruisseaux.
Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
45 Il envoya contre eux le moucheron qui les dévora, et la grenouille qui les fit périr.
Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
46 Il livra leurs récoltes à la sauterelle, le produit de leur travail à ses essaims.
Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
47 Il détruisit leurs vignes par la grêle, et leurs sycomores par les grêlons.
Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
48 Il abandonna leur bétail à la grêle, et leurs troupeaux aux coups de la foudre.
Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
49 Il déchaîna contre eux le feu de son courroux, la fureur, la rage et la détresse, toute une armée d’anges de malheur.
Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
50 Il donna libre carrière à sa colère, il ne sauva pas leur âme de la mort, il livra leur vie à la destruction.
Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
51 Il frappa tous les premiers-nés en Égypte, les prémices de la force sous les tentes de Cham.
Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
52 Il fit partir son peuple comme des brebis, il les mena comme un troupeau dans le désert.
Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
53 Il les dirigea sûrement, sans qu’ils eussent rien à craindre, et la mer engloutit leurs ennemis.
Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
54 Il les fit arriver jusqu’à sa frontière sainte, jusqu’à la montagne que sa droite a conquise.
Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
55 Il chassa les nations devant eux, leur assigna par le sort leur part d’héritage, et fit habiter dans leurs tentes les tribus d’Israël.
Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
56 Cependant ils ont encore tenté et provoqué le Dieu Très-Haut, et ils n’ont pas observé ses ordonnances.
Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
57 Ils se sont détournés et ont été infidèles comme leurs pères, ils se sont détournés comme un arc trompeur.
Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
58 Ils l’ont irrité par leurs hauts lieux, ils ont excité sa jalousie par leurs idoles.
Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
59 Dieu entendit et s’indigna, il prit Israël en grande aversion.
Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
60 Il dédaigna la demeure de Silo, la tente où il habitait parmi les hommes.
Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
61 Il livra sa force à la captivité, et sa majesté aux mains de l’ennemi.
Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
62 Il abandonna son peuple au glaive, et il s’indigna contre son héritage.
Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
63 Le feu dévora ses jeunes hommes, et ses vierges n’entendirent pas le chant nuptial.
Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
64 Ses prêtres tombèrent par l’épée, et ses veuves ne se lamentèrent point.
Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
65 Le Seigneur se réveilla, comme un homme endormi, pareil au guerrier subjugué par le vin.
Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
66 Il frappa ses ennemis par derrière, il leur infligea une honte éternelle.
Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
67 Mais il prit en aversion la tente de Joseph, et il répudia la tribu d’Ephraïm.
Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
68 Il choisit la tribu de Juda, la montagne de Sion qu’il aimait.
Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
69 Et il bâtit son sanctuaire comme les hauteurs du ciel, comme la terre qu’il a fondée pour toujours.
Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
70 Il choisit David, son serviteur, et le tira des bergeries;
Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
71 Il le prit derrière les brebis mères, pour paître Jacob, son peuple, et Israël, son héritage.
Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
72 Et David les guida dans la droiture de son cœur, et il les conduisit d’une main habile.
Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.

< Psaumes 78 >