< Psaumes 73 >

1 Psaume d’Asaph. Oui, Dieu est bon pour Israël, pour ceux qui ont le cœur pur!
Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
2 Toutefois j’étais sur le point de fléchir, mon pied a presque glissé.
Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
3 Car je m’indignais contre les impies, en voyant le bonheur des méchants.
Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
4 Pour eux, pas de douleurs jusqu’à la mort; leur corps est plein de vigueur.
Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
5 Ils n’ont pas de part au labeur des mortels, ils ne sont pas frappés avec le reste des hommes.
Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
6 Aussi l’orgueil est la parure de leur cou, et la violence, la robe précieuse qui les couvre.
Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
7 L’iniquité sort de leurs entrailles, les pensées de leur cœur se font jour.
Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
8 Ils raillent, ils parlent iniquité et violence, ils profèrent des discours hautains.
Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
9 Ils dirigent leur bouche contre le ciel même, et leur langue s’exerce sur la terre.
Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
10 C’est pourquoi mon peuple se tourne de leur côté, il avale l’eau à grands traits.
Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
11 Ils disent: « Comment Dieu saurait-il? Comment le Très-Haut connaîtrait-il? »
Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
12 Tels sont les méchants: toujours heureux, ils accroissent leurs richesses.
Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
13 C’est donc en vain que j’ai gardé mon cœur pur, que j’ai lavé mes mains dans l’innocence;
Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
14 tout le jour je suis frappé, chaque matin mon châtiment est là. »
Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
15 Si j’avais dit: « Je veux parler comme eux », j’aurai trahi la race de tes enfants.
Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
16 J’ai réfléchi pour comprendre ces choses, la difficulté a été grande à mes yeux,
Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
17 jusqu’à ce que j’aie pénétré dans le sanctuaire de Dieu, et pris garde à leur sort final.
Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
18 Oui, tu les places sur des voies glissantes; tu les fais tomber, et ils ne sont plus que ruines.
Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
19 Eh quoi! En un instant les voilà détruits! Ils sont anéantis, ils disparaissent dans des catastrophes!
Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
20 Comme on fait d’un songe au réveil, Seigneur, à ton réveil, tu repousses leur image.
Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
21 Lorsque mon cœur s’aigrissait, et que je me sentais profondément ému,
Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
22 j’étais stupide et sans intelligence, j’étais comme une brute devant toi.
nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
23 Mais je serai à jamais avec toi: tu m’as saisi la main droite,
Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
24 par ton conseil tu me conduiras, et tu me recevras ensuite dans la gloire.
Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
25 Quel autre que toi ai-je au ciel? Avec toi, je ne désire rien sur la terre.
Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
26 Ma chair et mon cœur se consument: le rocher de mon cœur et mon partage, c’est Dieu à jamais.
Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
27 Voici que ceux qui s’éloignent de toi périssent; tu extermines tous ceux qui te sont infidèles.
Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 Pour moi, être uni à Dieu, c’est mon bonheur; dans le Seigneur Yahweh je mets ma confiance, afin de raconter toutes tes œuvres.
Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.

< Psaumes 73 >