< Psaumes 57 >
1 Au maître de chant. « Ne détruis pas. » Hymne de David, lorsque, poursuivi par Saül, il se réfugia dans la caverne. Aie pitié de moi, ô Dieu, aie pitié de moi, car en toi mon âme cherche un refuge; je m’abriterai à l’ombre de tes ailes, jusqu’à ce que la calamité soit passée.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni. Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie, kwa maana nafsi yangu inakukimbilia. Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia mpaka maafa yapite.
2 Je crie vers le Dieu Très-Haut, le Dieu qui fait tout pour moi.
Namlilia Mungu Aliye Juu Sana, Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.
3 Il m’enverra du ciel le salut: — mon persécuteur m’accable d’outrages! — Séla. Dieu enverra sa bonté et sa vérité.
Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa, akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali; Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.
4 Je couche au milieu des lions, des hommes qui vomissent la flamme, qui ont pour dents la lance et les flèches, et dont la langue est un glaive tranchant.
Niko katikati ya simba, nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu: watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, ambao ndimi zao ni panga kali.
5 Elève-toi au-dessus des cieux, ô Dieu, que ta gloire brille par toute la terre!
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
6 Ils avaient tendu un piège devant mes pas, déjà mon âme se courbait; ils avaient creusé une fosse devant moi: ils y sont tombés! — Séla.
Waliitegea miguu yangu nyavu, nikainamishwa chini na dhiki. Wamechimba shimo katika njia yangu, lakini wametumbukia humo wao wenyewe.
7 Mon cœur est affermi, ô Dieu, mon cœur est affermi; je chanterai et ferai retentir de joyeux instruments.
Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
8 Eveille-toi, ma gloire! Eveillez-vous, ma lyre et ma harpe! Que j’éveille l’aurore!
Amka, nafsi yangu! Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
9 Je te louerai parmi les peuples, Seigneur, je te chanterai parmi les nations.
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
10 Car ta fidélité atteint jusqu’aux cieux, et ta vérité jusqu’aux nues.
Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni, uaminifu wako unazifikia anga.
11 Elève-toi au-dessus des cieux, ô Dieu, que ta gloire brille sur toute la terre!
Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni, utukufu wako na uwe duniani pote.