< Psaumes 113 >

1 Alleluia! Louez, serviteurs de Yahweh, louez le nom de Yahweh,
Msifuni Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe; lisifuni jina la Yahwe.
2 Que le nom de Yahweh soit béni, dès maintenant et à jamais!
Litukuzwe jina la Yahwe, tangu sasa na hata milele.
3 Du lever du soleil jusqu’à son couchant, loué soit le nom de Yahweh!
Toka maawio ya jua hata machweo yake, Jina la Yahwe lazima lisifiwe.
4 Yahweh est élevé au-dessus de toutes les nations, sa gloire est au-dessus des cieux.
Yahwe ameinuliwa juu ya mataifa yote, na utukufu wake wafika juu mbinguni.
5 Qui est semblable à Yahweh, notre Dieu? Il siège dans les hauteurs,
Ni nani aliye kama Yahwe Mungu wetu, aliye na kiti chake juu,
6 et il regarde en bas, dans les cieux et sur la terre.
atazamaye chini angani na duniani?
7 Il relève le malheureux de la poussière, il retire le pauvre du fumier,
Humwinua maskini toka mavumbini na kumpandisha muhitaji kutoka jaani,
8 pour les faire asseoir avec les princes, avec les princes de son peuple.
ili amketishe pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
9 Il donne une demeure à la stérile de la maison, il en fait une mère joyeuse au milieu de ses enfants. Alleluia!
Humpa watoto wanamke aliye tasa, humfanya yeye kuwa mama wa watoto mwenye furaha. Msifuni Yahwe!

< Psaumes 113 >