< Psaumes 109 >

1 Au maître de chant. Psaume de David. Dieu de ma louange, ne garde pas le silence!
Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
2 Car la bouche du méchant, la bouche du perfide, s’ouvre contre moi. Ils parlent contre moi avec une langue de mensonge,
Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
3 ils m’assiègent de paroles haineuses, et ils me font la guerre sans motif.
Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
4 En retour de mon affection, ils me combattent, et moi, je ne fais que prier.
Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
5 Ils me rendent le mal pour le bien, et la haine pour l’amour.
Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
6 Mets-le au pouvoir d’un méchant, et que l’accusateur se tienne à sa droite!
Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
7 Quand on le jugera, qu’il sorte coupable, et que sa prière soit réputée péché!
Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
8 Que ses jours soient abrégés, et qu’un autre prenne sa charge!
Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
9 Que ses enfants deviennent orphelins, que son épouse soit veuve!
Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
10 Que ses enfants soient vagabonds et mendiants, cherchant leur pain loin de leurs maisons en ruines!
Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
11 Que le créancier s’empare de tout ce qui est à lui, et que les étrangers pillent ce qu’il a gagné par son travail!
Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
12 Qu’il n’ait personne qui lui garde son affection, que nul n’ait pitié de ses orphelins!
Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
13 Que ses descendants soient voués à la ruine, et que leur nom soit effacé à la seconde génération!
Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
14 Que l’iniquité de ses pères reste en souvenir devant Yahweh, et que la faute de leur mère ne soit pas effacée!
Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
15 Qu’elles soient toujours devant Yahweh, et qu’il retranche de la terre leur mémoire!
Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
16 Parce qu’il ne s’est pas souvenu d’exercer la miséricorde, parce qu’il a persécuté le malheureux et l’indigent, et l’homme au cœur brisé pour le faire mourir.
Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
17 Il aimait la malédiction: elle tombe sur lui; il dédaignait la bénédiction: elle s’éloigne de lui.
Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
18 Il s’est revêtu de la malédiction comme d’un vêtement; comme l’eau elle entre au-dedans de lui, et comme l’huile elle pénètre dans ses os.
Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
19 Qu’elle soit pour lui le vêtement qui l’enveloppe, la ceinture qui ne cesse de l’entourer!
Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
20 Tel soit, de la part de Yahweh le salaire de mes adversaires, et de ceux qui parlent méchamment contre moi.
Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
21 Et toi, Seigneur Yahweh, prends ma défense à cause de ton nom; dans ta grande bonté, délivre-moi.
Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
22 Car je suis malheureux et indigent, et mon cœur est blessé au-dedans de moi.
Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
23 Je m’en vais comme l’ombre à son déclin, je suis emporté comme la sauterelle.
Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
24 A force de jeûne mes genoux chancellent, et mon corps est épuisé de maigreur.
Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
25 Je suis pour eux un objet d’opprobre; ils me regardent et branlent de la tête.
Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
26 Secours-moi, Yahweh, mon Dieu! Sauve-moi dans ta bonté!
Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
27 Qu’ils sachent que c’est ta main, que c’est toi, Yahweh, qui l’a fait!
Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
28 Eux, ils maudissent; mais toi, tu béniras; ils se lèvent, mais ils seront confondus, et ton serviteur sera dans la joie.
Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
29 Mes adversaires seront revêtus d’ignominie, ils seront enveloppés de leur honte comme d’un manteau.
Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
30 Mes lèvres loueront hautement Yahweh; je le célébrerai au milieu de la multitude;
Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
31 car il se tient à la droite du pauvre, pour le sauver de ceux qui le condamnent.
Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.

< Psaumes 109 >