< Nombres 12 >
1 Marie, avec Aaron, parla contre Moïse au sujet de la femme couschite qu’il avait prise; car il avait pris une femme couschite.
Miriamu na Aroni walianza kuzungumza dhidi ya Mose kwa sababu ya mke wake Mkushi, kwa kuwa alikuwa ameoa Mkushi.
2 Ils dirent: « Est-ce seulement par Moïse que Yahweh a parlé? N’a-t-il pas parlé aussi par nous? » Et Yahweh l’entendit.
Waliuliza, “Je, Bwana amesema kupitia Mose peke yake? Je, hajasema kutupitia sisi pia?” Naye Bwana akasikia hili.
3 Mais Moïse était un homme fort doux, plus qu’aucun homme qui fût sur la face de la terre.
(Basi Mose alikuwa mtu mnyenyekevu sana, mnyenyekevu kuliko mtu mwingine yeyote katika uso wa dunia.)
4 Soudain Yahweh dit à Moïse, à Aaron et à Marie: « Sortez, vous trois, vers la tente de réunion. » Et ils sortirent tous les trois;
Ghafula Bwana akawaambia Mose, Aroni na Miriamu, “Njooni katika Hema la Kukutania, ninyi nyote watatu.” Kwa hiyo wote watatu wakaenda.
5 et Yahweh descendit dans la colonne de nuée et se tint à l’entrée de la tente. Il appela Aaron et Marie, qui s’avancèrent tous deux;
Kisha Bwana akashuka katika nguzo ya wingu, akasimama kwenye ingilio la Hema, akawaita Aroni na Miriamu. Wakati wote wawili waliposogea mbele,
6 et il dit: « Ecoutez bien mes paroles: si vous avez quelque prophète de Yahweh, c’est en vision que je me révèle à lui, c’est en songe que je lui parle.
Bwana akasema, “Sikilizeni maneno yangu: “Akiwapo nabii wa Bwana miongoni mwenu, nitajifunua kwake kwa maono, nitanena naye katika ndoto.
7 Tel n’est pas mon serviteur Moïse; il est reconnu fidèle dans toute ma maison.
Lakini sivyo kwa mtumishi wangu Mose; yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote.
8 Je lui parle bouche à bouche, en me faisant voir, et non par énigmes, et il contemple la figure de Yahweh. Pourquoi donc n’avez-vous pas craint de parler contre mon serviteur, contre Moïse? »
Kwake nitanena naye uso kwa uso, waziwazi wala si kwa mafumbo; yeye ataona umbo la Bwana. Kwa nini basi ninyi hamkuogopa kuzungumza kinyume cha mtumishi wangu Mose?”
9 Et la colère de Yahweh s’enflamma contre eux; et il s’en alla;
Hasira ya Bwana ikawaka dhidi yao, akawaacha.
10 la nuée se retira de dessus la tente. Et voici, Marie devint lépreuse, blanche comme la neige. Aaron se tourna vers Marie, et voici, elle était lépreuse.
Wakati hilo wingu liliinuka kutoka juu ya Hema, Miriamu akawa tayari ana ukoma, mweupe kama theluji. Aroni akamgeukia, akaona ana ukoma.
11 Et Aaron dit à Moïse: « De grâce, mon seigneur, ne mets pas sur nous ce péché que nous avons follement commis, et dont nous sommes coupables.
Kisha Aroni akamwambia Mose, “Tafadhali, bwana wangu, usituhesabie dhambi hii ambayo tumeifanya kwa upumbavu.
12 Ah! Qu’elle ne soit pas comme l’enfant mort-né qui, en sortant du sein de sa mère, a la chair à demi-consumée! »
Usimwache awe kama mtoto mchanga aliyezaliwa akiwa mfu, ambaye nusu ya mwili wake imeharibika hapo atokapo katika tumbo la mama yake.”
13 Moïse cria à Yahweh, en disant: « O Dieu, je vous prie, guérissez-là! »
Hivyo Mose akamlilia Bwana akisema, “Ee Mungu, nakuomba umponye!”
14 Yahweh dit à Moïse: « Si son père lui avait craché au visage, ne serait-elle pas pendant sept jours couverte de honte? Qu’elle soit séquestrée sept jours hors du camp; après quoi, elle y sera reçue. »
Bwana akamjibu Mose, “Je, kama baba yake angemtemea usoni, asingeona aibu kwa siku saba? Mfungie nje ya kambi kwa siku saba; baada ya hapo anaweza kurudishwa kambini.”
15 Marie fut donc séquestrée sept jours hors du camp, et le peuple ne partit point, jusqu’à ce que Marie eût été reçue.
Kwa hiyo Miriamu akafungiwa nje ya kambi kwa siku saba, nao watu hawakuendelea na safari mpaka aliporudishwa kambini.
16 Après cela, le peuple partit de Haséroth, et ils campèrent dans le désert de Pharan.
Baada ya hayo, watu waliondoka Haserothi, wakapiga kambi katika Jangwa la Parani.