< Néhémie 3 >

1 Eliasib, le grand prêtre, et ses frères les prêtres se mirent à bâtir la porte des Brebis; ils la consacrèrent et en posèrent les battants; ils réparèrent la muraille et la consacrèrent jusqu’à la tour de Méa et jusqu’à la tour de Hananéel.
Eliashibu kuhani mkuu na makuhani wenzake walikwenda kufanya kazi na kulijenga upya Lango la Kondoo. Waliliweka wakfu na kuweka milango mahali pake, wakajenga hadi kufikia Mnara wa Mia, ambao waliuweka wakfu hadi Mnara wa Hananeli.
2 A côté bâtissaient les hommes de Jéricho; et à côté bâtissait Zachur, fils d’Amri.
Watu wa Yeriko wakajenga sehemu zilizopakana nao, naye Zakuri mwana wa Imri akajenga karibu nao.
3 Les fils d’Asnaa bâtirent la porte des Poissons; ils y mirent des poutres et en posèrent les battants, les verrous et les barres;
Lango la Samaki lilijengwa upya na wana wa Hasenaa. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango yake na makomeo na nondo.
4 et à côté, réparait Marimuth, fils d’Urie, fils d’Accus; et à côté réparait Mosollam, fils de Barachie, fils de Mésézébel; et à côté réparait Sadoc, fils de Baana;
Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu iliyofuatia. Baada yake Meshulamu mwana wa Berekia, mwana wa Meshezabeli, alifanya ukarabati na aliyemfuatia ni Sadoki mwana wa Baana.
5 et à côté réparaient les Thécuites: mais leurs chefs n’apportèrent pas leur concours à la besogne de leur Seigneur.
Sehemu iliyofuatia ilikarabatiwa na watu kutoka Tekoa, lakini wakuu wao walikataa kufanya kazi chini ya wasimamizi wao.
6 Joïada, fils de Phaséa, et Mosollam, fils de Besodias, réparèrent la Vieille Porte; ils y mirent des poutres et en posèrent les battants, les verrous et les barres.
Lango la Yeshana lilikarabatiwa na Yoyada mwana wa Pasea, na Meshulamu mwana wa Besodeya. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango, makomeo na nondo.
7 Et à côté réparaient Meltias le Gabaonite, Jadon le Méronathite, et les hommes de Gabaon et de Maspha, près du tribunal du gouverneur d’au delà du fleuve;
Karibu nao ukarabati ulifanywa na watu kutoka Gibeoni na Mispa, yaani Melati Mgibeoni, na Yadoni Mmeronothi, sehemu hizi zikiwa chini ya mamlaka ya mtawala wa Ngʼambo ya Frati.
8 et à côté réparait Eziel, fils d’Araïas, chef des orfèvres; et à côté réparait Ananie, de la corporation des parfumeurs. Ils laissèrent Jérusalem jusqu’à la muraille large.
Uzieli mwana wa Harhaya, mmoja wa masonara, alikarabati sehemu iliyofuatia, naye Hanania mmoja wa watengenezaji marashi akakarabati sehemu iliyofuatia. Walitengeneza Yerusalemu mpaka kufikia Ukuta Mpana.
9 A côté d’eux réparait Raphaïas, fils de Hur, chef de la moitié du district de Jérusalem.
Refaya mwana wa Huri, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia.
10 A côté réparait, vis-à-vis de sa maison, Jédaïas, fils de Haromaph; et à côté réparait Hattus, fils de Hasebonias.
Kupakana na sehemu hii, Yedaya mwana wa Harumafu alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba yake, naye Hatushi mwana wa Hashabnea akakarabati sehemu iliyofuatia.
11 Melchias, fils de Herem, et Hasub, fils de Phahath-Moab, réparèrent une autre partie de la muraille et la tour des Fourneaux.
Malkiya mwana wa Harimu, na Hashubu mwana wa Pahath-Moabu walikarabati sehemu nyingine pamoja na Mnara wa Matanuru.
12 A côté réparait, avec ses filles, Sellum, fils d’Alohès, chef de l’autre moitié du district de Jérusalem.
Shalumu mwana wa Haloheshi, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia akisaidiwa na binti zake.
13 Hanun et les habitants de Zanoé réparèrent la porte de la Vallée; ils la bâtirent et en posèrent les battants, les verrous et les barres; ils firent en outre mille coudées de mur jusqu’à la porte du Fumier.
Lango la Bondeni lilikarabatiwa na Hanuni na wakazi wa Zanoa. Walilijenga upya, na kuweka milango yake na makomeo na nondo mahali pake. Pia walikarabati ukuta wenye urefu wa mita 450 hadi Lango la Samadi.
14 Melchias, fils de Réchab, chef du district de Bethacharam, répara la porte du Fumier; il la bâtit et en posa les battants, les verrous et les barres.
Lango la Samadi lilikarabatiwa na Malkiya mwana wa Rekabu, mtawala wa wilaya ya Beth-Hakeremu. Alilijenga upya, na kuweka milango yake, na makomeo na nondo.
15 Sellun, fils de Cholhoza, chef du district de Maspha, répara la porte de la Source; il la bâtit, la couvrit et en posa les battants, les verrous et les barres; il fit en outre les murs de l’étang de Siloé, près du jardin du Roi, jusqu’aux degrés qui descendent de la cité de David.
Lango la Chemchemi lilikarabatiwa na Shalumu mwana wa Kolhoze, mtawala wa wilaya ya Mispa. Alilijenga upya, akaliezeka na kuweka milango yake, na makomeo na nondo mahali pake. Pia alikarabati ukuta wa Bwawa la Siloamu karibu na Bustani ya Mfalme, hadi kwenye ngazi zinazoshuka kutoka Mji wa Daudi.
16 Après lui, Néhémie, fils d’Azboc, chef de la moitié du district de Bethsur, répara jusque vis-à-vis des sépulcres de David, jusqu’au réservoir qui avait été construit, et jusqu’à la maison des Héros.
Baada yake, Nehemia mwana wa Azbuki, mtawala wa nusu ya wilaya ya Beth-Suri, alikarabati kufikia mkabala na makaburi ya Daudi, mpaka kwenye bwawa lililotengenezwa, na kufikia Nyumba ya Mashujaa.
17 Après lui réparaient les lévites, sous la conduite de Réhum, fils de Benni; à côté de lui réparait, pour son district, Hasébias, chef de la moitié du district de Céïla.
Baada yake, ukarabati ulifanywa na Walawi chini ya uongozi wa Rehumu mwana wa Bani. Aliyefuatia ni Hashabia, mtawala wa nusu ya wilaya ya Keila, aliyekarabati sehemu ya wilaya yake.
18 Après lui réparaient leurs frères, sous la conduite de Bavaï, fils de Enadad, chef de l’autre moitié du district de Céïla.
Baada yake, ukarabati ulifanywa na ndugu zao chini ya usimamizi wa Binui mwana wa Henadadi, mtawala wa nusu hiyo ingine ya wilaya ya Keila.
19 A côté, Azer, fils de Josué, chef de Maspha, répara une autre portion de la muraille, vis-à-vis de la montée de l’arsenal, à l’angle.
Baada yao, Ezeri mwana wa Yeshua, mtawala wa Mispa, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia ile sehemu inayotazamana na mwinuko wa kuelekea kwenye ghala la kuhifadhia silaha, mpaka kwenye pembe ya ukuta.
20 Après lui, Baruch, fils de Zachaï, réparait avec ardeur une autre portion, depuis l’angle jusqu’à la porte de la maison d’Eliasib, le grand prêtre.
Baada yake, Baruku mwana wa Zakai alikarabati kwa bidii sehemu nyingine kuanzia ile pembe, mpaka kwenye lango la nyumba ya Eliashibu kuhani mkuu.
21 Après lui, Mérimuth, fils d’Urie, fils de Haccus, réparait une autre portion, depuis la porte de la maison d’Eliasib, jusqu’à l’extrémité de la maison d’Eliasib.
Kupakana naye, Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia penye lango la nyumba ya Eliashibu mpaka mwisho wake.
22 Après lui réparaient les prêtres, les hommes de la plaine du Jourdain.
Baada yake, ukarabati ulifanywa na makuhani waliotoka eneo lililouzunguka mji.
23 Après eux Benjamin et Hasub réparaient vis-à-vis de leur maison. Après eux, Azarias, fils de Maasias, fils d’Ananie, réparait à côté de sa maison.
Baada yao Benyamini na Hashubu walikarabati mbele ya nyumba zao, na baada yao Azaria mwana wa Maaseya, mwana wa Anania alifanya ukarabati kando ya nyumba yake.
24 Après lui, Bennui, fils de Hénadad réparait une autre portion, depuis la maison d’Azarias jusqu’à l’angle et jusqu’au tournant.
Baada yake, Binui mwana wa Henadadi alikarabati sehemu nyingine, kuanzia kwenye nyumba ya Azaria mpaka kwenye pembe ya ukuta.
25 Phalel, fils d’Ozi, réparait vis-à-vis de l’angle et de la haute tour qui fait saillie en avant de la maison du roi, près de la cour de la prison. Après lui réparait Phadaïas, fils de Pharos.
Naye Palali, mwana wa Uzai alijenga sehemu iliyokuwa mkabala na pembe ya ukuta, mpaka kwenye mnara wa juu ambao unajitokeza kuanzia kwenye jumba la kifalme, kando ya ua wa walinzi. Baada yake, Pedaya mwana wa Paroshi,
26 Les Nathinéens demeuraient sur Ophel, jusque vis-à-vis de la porte de l’Eau, à l’orient, et de la tour en saillie.
na watumishi wa Hekalu walioishi juu ya kilima cha Ofeli walikarabati hadi kufikia mkabala na Lango la Maji, kuelekea mashariki na ule mnara uliojitokeza.
27 Après lui, les Thécuites réparèrent une autre portion, vis-à-vis de la grande tour en saillie, jusqu’au mur d’Ophel.
Baada yao, watu wa Tekoa walikarabati sehemu nyingine, kuanzia mnara mkubwa utokezao hadi ukuta wa Ofeli.
28 Au-dessus de la porte des Chevaux, réparaient les prêtres, chacun devant sa maison.
Makuhani walifanya ukarabati juu ya Lango la Farasi, kila mmoja mbele ya nyumba yake.
29 Après lui, Sadoc, fils d’Emmer, réparait devant sa maison; après lui, réparait Sémaïas, fils de Séchénias, gardien de la porte orientale du temple.
Baada yao, Sadoki mwana wa Imeri alifanya ukarabati mkabala na nyumba yake. Baada yake, Shemaya mwana wa Shekania, mlinzi wa Lango la Mashariki, alifanya ukarabati.
30 Après lui, Hananias, fils de Sélémias, et Hanun, le sixième fils de Séleph, réparaient une autre portion de la muraille. Après lui, réparait Mosollam, fils de Barachie, devant sa demeure.
Baada yake, Hanania mwana wa Shelemia, na Hanuni mwana wa sita wa Salafu walikarabati sehemu nyingine. Baada yao, Meshulamu mwana wa Berekia alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba zake za kuishi.
31 Après lui, réparait Melchias, de la corporation des orfèvres, jusqu’à l’habitation des Nathinéens et des marchands, devant la porte de Miphcad, et jusqu’à la chambre haute du tournant.
Baada yake Malkiya, mmoja wa masonara, alifanya ukarabati mpaka kwenye nyumba za watumishi wa Hekalu na wafanyabiashara, mkabala na Lango la Ukaguzi, hadi kufikia chumba kilicho juu ya pembe.
32 Et, entre la chambre haute du tournant et la porte des Brebis, réparaient les orfèvres et les marchands.
Masonara na wafanyabiashara walifanya ukarabati kutoka chumba kilichoko juu ya pembe hadi Lango la Kondoo.

< Néhémie 3 >