< Michée 7 >
1 Hélas! je suis comme après la récolte des fruits d’été, comme après le grappillage de la vendange: pas une grappe a manger! pas une des premières figues que mon âme désire!
Taabu gani hii niliyo nayo! Nimefanana na yule akusanyaye matunda ya kiangazi, aokotaye masazo baada ya kuvunwa shamba la mizabibu; hakuna kishada chenye matunda ya kula, hakuna hata ile tini ya mwanzoni ninayoitamani.
2 L’homme pieux a disparu de la terre, et il n’y a plus un juste parmi les hommes. Tous ils se mettent en embuscade pour répandre le sang; chacun fait la chasse à son frère et lui tend le filet.
Wanaomcha Mungu wameondolewa kutoka nchi; hakuna mtu mnyofu hata mmoja aliyebaki. Watu wote wanavizia kumwaga damu, kila mmoja anamwinda ndugu yake kwa wavu.
3 Le mal, il y a des mains pour le bien faire; le prince exige, le juge fait son prix, et le grand manifeste son avidité; c’est ainsi qu’ils ourdissent ensemble leur trame.
Mikono yote miwili ni hodari katika kufanya ubaya, mtawala anadai zawadi, hakimu anapokea rushwa, wenye nguvu wanaamuru wanachotaka: wote wanafanya shauri baya pamoja.
4 Le meilleur d’entre eux est pareil à l’épine; le plus droit, pire qu’une haie de ronces. — Le jour annoncé par tes sentinelles, le jour de ton châtiment est venu; maintenant ils vont être dans la confusion! —
Aliye mwema kupita wote kati yao ni kama mchongoma, anayeonekana mnyofu zaidi miongoni mwao ni mbaya kuliko uzio wa miiba. Siku ya walinzi wako imewadia, siku atakayokutembelea Mungu. Sasa ni wakati wao wa kuchanganyikiwa.
5 Ne croyez pas à un ami, ne vous fiez pas à un intime; devant celle qui repose sur ton sein, garde les paroles de ta bouche!
Usimtumaini jirani; usiweke matumaini kwa rafiki. Hata kwa yule alalaye kifuani mwako uwe mwangalifu kwa maneno yako.
6 Car le fils traite son père de fou; la fille s’insurge contre sa mère, la belle-fille contre sa belle-mère; chacun a pour ennemis les gens de sa maison.
Kwa kuwa mwana humdharau baba yake, naye binti huinuka dhidi ya mama yake, mkwe kuwa kinyume na mama mkwe wake: adui wa mtu ni wale wa nyumbani mwake hasa.
7 Et moi je regarderai vers Yahweh, j’espérerai dans le Dieu de mon salut; mon Dieu m’écoutera.
Lakini mimi, namtazama Bwana kwa matumaini, namngoja Mungu Mwokozi wangu; Mungu wangu atanisikia mimi.
8 Ne te réjouis pas à mon sujet, ô mon ennemie; car, si je suis tombée, je me relèverai; si je suis assise dans les ténèbres, Yahweh est ma lumière.
Usifurahie msiba wangu, ee adui yangu! Ingawa nimeanguka, nitainuka. Japo ninaketi gizani, Bwana atakuwa nuru yangu.
9 Je porterai la colère de Yahweh, puisque j’ai péché contre lui, jusqu’à ce qu’il prenne en main ma cause, et qu’il établisse mon droit; il me fera sortir à la lumière, je contemplerai sa justice.
Kwa sababu nimetenda dhambi dhidi yake, nitabeba ghadhabu ya Bwana, mpaka atakaponitetea shauri langu na kuithibitisha haki yangu. Atanileta nje kwenye mwanga, nami nitaiona haki yake.
10 Que mon ennemie le voie, et que la honte la recouvre, elle qui me disait: « Où est Yahweh, ton Dieu? » Mes yeux la contempleront; maintenant elle sera foulée aux pieds, comme la boue des rues.
Kisha adui yangu ataliona naye atafunikwa na aibu, yule aliyeniambia, “Yu wapi Bwana Mungu wako?” Macho yangu yataona kuanguka kwake, hata sasa atakanyagwa chini ya mguu kama tope barabarani.
11 Le jour vient où tes murs seront rebâtis; ce jour-là le décret sera retiré.
Siku ya kujenga kuta zako itawadia, siku ya kupanua mipaka yako.
12 Ce jour-là, on viendra jusqu’à toi, de l’Assyrie et des villes d’Égypte, de l’Égypte jusqu’au fleuve, d’une mer à l’autre et d’une montagne à l’autre.
Siku hiyo watu watakuja kwako kutoka Ashuru na miji ya Misri, hata kutoka Misri hadi Frati na kutoka bahari hadi bahari na kutoka mlima hadi mlima.
13 Le pays deviendra un désert, à cause de ses habitants: c’est là le fruit de leurs actions.
Dunia itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakazi wake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.
14 Pais ton peuple avec ta houlette, le troupeau de ton héritage, qui habite solitaire dans la forêt, au milieu du Carmel; qu’elles paissent en Basan et en Galaad, comme aux jours anciens!
Wachunge watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako, ambalo linaishi peke yake msituni, katika nchi ya malisho yenye rutuba. Waache walishe katika Bashani na Gileadi kama ilivyokuwa siku za kale.
15 Comme au jour où tu sortis du pays d’Égypte, je lui ferai voir des prodiges.
“Kama siku zile mlipotoka Misri, nitawaonyesha maajabu yangu.”
16 Les nations le verront, et seront confuses de toute leur puissance; elles mettront la main sur la bouche; leurs oreilles seront assourdies.
Mataifa yataona na kuaibika, waliondolewa nguvu zao zote. Wataweka mikono yao kwenye vinywa vyao na masikio yao yatakuwa na uziwi.
17 Elles lécheront la poussière comme le serpent; comme les reptiles de la terre, elles sortiront avec effroi de leurs retraites; elles viendront en tremblant vers Yahweh, notre Dieu, et elles vous craindront.
Wataramba mavumbi kama nyoka, kama viumbe vitambaavyo juu ya ardhi. Watatoka nje ya mapango yao wakitetemeka; watamgeukia Bwana Mungu wetu kwa hofu nao watakuogopa.
18 Quel Dieu est semblable à vous, qui ôtez l’iniquité, et qui pardonnez la transgression au reste de votre héritage? Il ne fait pas à toujours prévaloir sa colère, car il prend plaisir, lui, à faire grâce.
Ni nani Mungu kama wewe, ambaye anaachilia dhambi na kusamehe makosa ya mabaki ya urithi wake? Wewe huwi na hasira milele, bali unafurahia kuonyesha rehema.
19 Il aura encore pitié de nous, il foulera encore aux pieds nos iniquités! Vous jetterez au fond de la mer tous leurs péchés;
Utatuhurumia tena, utazikanyaga dhambi zetu chini ya nyayo zako, na kutupa maovu yetu yote katika vilindi vya bahari.
20 vous ferez voir à Jacob votre fidélité, à Abraham la miséricorde, que vous avez jurée à nos pères, dès les jours anciens.
Utakuwa wa kweli kwa Yakobo, nawe utamwonyesha Abrahamu rehema, kama ulivyowaahidi kwa kiapo baba zetu siku za kale.