< Michée 4 >
1 Il arrivera à la fin des jours, que la Montagne de la maison de Yahweh sera établie au sommet des montagnes, et élevée au-dessus des collines. Et sur elle les nations afflueront.
Lakini katika siku za mwisho itakuja kuhusu kwamba mlima wa nyumba ya Yahwe utawekwa imare juu ya milima mingine. Utainuliwa juu ya milima, na watu watautakabisha.
2 Et des peuples nombreux viendront et diront: « Venez, montons à la montagne de Yahweh, et à la maison du Dieu de Jacob; il nous instruira de ses voies, et nous marcherons dans ses sentiers. » Car de Sion sortira la loi, et de Jérusalem la parole de Yahweh.
Mataifa mengi yataenda na kusema, “Njoni, twendeni juu kwenye mlima wa Yahwe, kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo. Atatufundisha njia zake, na tutembea katika njia zake.” Kwa kuwa kutoka Sayuni sheria itatoka, na neno la Yahwe kutoka Yerusalemu.
3 Il sera l’arbitre de nations nombreuses, et le juge de peuples puissants, jusqu’au loin. Ils forgeront leurs épées en socs de charrue, et leurs lances en faucilles; une nation ne lèvera plus l’épée contre l’autre, et l’on n’apprendra plus la guerre.
Atahukumu miongoni mwa watu na kuamua kuhusiana na mataifa mengi ya mbali. Watapoga mapanga yao kuwa plau na mikuki yao kuwa miuundu ya kupogolea. Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa, wala kutawala kwa vita tena.
4 Ils resteront assis chacun sous sa vigne, et sous son figuier, sans qu’il y ait personne pour les troubler; car la bouche de Yahweh des armées a parlé.
Badala yake, wataketi kila mtu chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake. Hakuna mtu atakayewafanya waogope, kwa kuwa mdomo wa Yahwe wa majeshi umesema.
5 Car tous les peuples marchent chacun au nom de son dieu; et nous, nous marchons au nom de Yahweh notre Dieu, toujours et à jamais.
Kwa kuwa watu wote wataenenda, kila mmoja, katika jina la mungu wake. Lakini sisi tutaenenda katika jina la Yahwe Mungu wetu milele na milele.
6 En ce jour-là, — oracle de Yahweh, je recueillerai celles qui boitent, je rassemblerai celles qui étaient dispersées, et auxquelles j’avais fait du mal.
“Katika siku hiyo,” aseme Yahwe, “Nitamkusanya achechemeaye na kumkusanya aliyefukuzwa, wale ambao nimewatesa.
7 Et je ferai de celles qui boitent un reste, et de celles qui sont éloignées une nation puissante. Et Yahweh régnera sur eux, sur la montagne de Sion, dès lors et à jamais.
Nitamrudisha aliyechechemea kwenye mabaki, na yeye aliyetupwa kwenye taifa imara, na mimi, Yahwe, nitatawala juu yao katika Milima Sayuni, sasa na milele.
8 Et toi, tour du troupeau, colline de la fille de Sion, elle viendra jusqu’à toi, elle te reviendra, l’ancienne domination, la royauté qui appartient à la fille de Jérusalem.
Kama kwako, mnara wa saa kwa ajili ya kundi, mlima wa binti wa Sayuni-utakuja kwenu, utawala wenu wa zamani utarudishwa, ufalme ambao unaomilikiwa na binti wa Yerusalemu.
9 Pourquoi maintenant pousses-tu des cris? N’y a-t-il plus, de roi en toi, et ton conseiller a-t-il péri, pour que la douleur t’ait saisie comme une femme qui enfante?
Sasa, kwa nini unapiga kelele kwa sauti kuu? Je hakuna mfalme miongoni mwenu? Je mshauri wako amekufa? Kwa nini uchungu umekushika kama yule mwanamke akiwa anazaa?
10 Sois dans les douleurs et les efforts, fille de Sion, comme celle qui enfante! Car maintenant tu vas sortir de la ville; et demeurer dans les champs, et tu iras jusqu’à Babylone; là tu seras délivrée; là Yahweh te rachètera, de la main de tes ennemis.
Kuwa katika uchungu wa kuzaa ili uzae, binti Sayuni, kama mwanamke mwenye uchungu. Kwa sasa utatoka nje ya mji, kuishi kwenye shamba, na kwenda Babeli. Huko utaokolewa. Huko Yahwe atakuokoa kutoka kwenye mikono ya maadui.
11 Et maintenant, contre toi se sont rassemblées des nations nombreuses; elles disent: « Qu’elle soit profanée, et que nos yeux contemplent Sion! »
Sasa mataifa mengi yamekusanyika juu yako; wakisema; 'Atiwe unajisi; macho yenu yaangalie Sayuni.”'
12 Mais elles ne connaissent pas les pensées de Yahweh, et elles ne comprennent pas ses desseins: savoir qu’il les a rassemblées comme des gerbes sur l’aire.
Nabii asema, “Hawayajui mawazo ya Yahwe, wala hawaelewi mpango wake, kwa kuwa wamewakusanaya kama miganda kupura sakafuni.”
13 Lève-toi et foule, fille de Sion! Car je ferai que ta corne soit de fer, et je ferai que tes sabots soient d’airain; et tu broieras des peuples nombreux; et je consacrerai leurs gains à Yahweh, et leurs richesses au Seigneur de toute la terre.
Yahwe asema, “siamama na upure, binti Sayuni, kwa kuwa nitaifanya pembe yako kuwa chuma, na nitazifanya kwato zako kuwa shaba. Utaponda watu wengi. Nitaweka wakfu udhalimu wao kwangu mwenyewe, Yahwe, miliki zao kwangu, Bwana wa dunia nzima.”