< Matthieu 15 >

1 Alors des scribes et des Pharisiens venus de Jérusalem s’approchèrent de Jésus, et lui dirent:
Ndipo baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria wakamjia Yesu kutoka Yerusalemu na kumuuliza,
2 « Pourquoi tes disciples transgressent-ils la tradition des anciens? Car ils ne se lavent pas les mains lorsqu’ils prennent leur repas. »
“Mbona wanafunzi wako wanakiuka mapokeo ya wazee? Kwa maana wao hawanawi mikono yao kabla ya kula!”
3 Il leur répondit: « Et vous, pourquoi transgressez-vous le commandement de Dieu par votre tradition?
Yesu akawajibu, “Mbona ninyi mnavunja amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu?
4 Car Dieu a dit: Honore ton père et ta mère; et: Quiconque maudira son père ou sa mère, qu’il soit puni de mort.
Kwa maana Mungu alisema, ‘Waheshimu baba yako na mama yako,’ na, ‘Yeyote amtukanaye baba yake au mama yake, na auawe.’
5 Mais vous, vous dites: Quiconque dit à son père ou à sa mère: Ce dont j’aurais pu vous assister, j’en ait fait offrande, —
Lakini ninyi mwafundisha kwamba mtu akimwambia baba yake au mama yake, ‘Kile ambacho ningeweza kukusaidia kimewekwa wakfu kwa Mungu,’
6 n’a pas besoin d’honorer autrement son père ou sa mère. Et vous mettez ainsi à néant le commandement de Dieu par votre tradition.
basi hana tena sababu ya kumheshimu baba yake nacho. Basi kwa ajili ya mafundisho yenu mnavunja amri ya Mungu.
7 Hypocrites, Isaïe a bien prophétisé de vous quand il a dit:
Ninyi wanafiki! Isaya alikuwa sawa alipotabiri juu yenu kwamba:
8 Ce peuple m’honore des lèvres, mais son cœur est loin de moi.
“‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami.
9 C’est en vain qu’ils m’honorent, en donnant des préceptes qui ne sont que des commandements venant des hommes. »
Huniabudu bure; nayo mafundisho yao ni maagizo ya wanadamu tu.’”
10 Puis, ayant fait approcher la foule, il leur dit: « Écoutez et comprenez.
Yesu akaita ule umati wa watu, akawaambia, “Sikilizeni na mwelewe:
11 Ce n’est pas ce qui entre dans la bouche qui souille l’homme; mais ce qui sort de la bouche, voilà ce qui souille l’homme. »
kinachomfanya mtu kuwa najisi mbele za Mungu si kile kiingiacho kinywani mwake, bali ni kile kitokacho kinywani mwake.”
12 Alors ses disciples venant à lui, lui dirent: « Sais-tu que les Pharisiens, en entendant cette parole, se sont scandalisés? »
Kisha wanafunzi wake wakamjia na kumuuliza, “Je, unajua kwamba Mafarisayo walichukizwa sana waliposikia yale uliyosema?”
13 Il répondit: « Toute plante que n’a pas plantée mon Père céleste, sera arrachée.
Akawajibu, “Kila pando ambalo Baba yangu wa mbinguni hakulipanda, litangʼolewa.
14 Laissez-les; ce sont des aveugles qui conduisent des aveugles. Or, si un aveugle conduit un aveugle, ils tomberont tous deux dans la fosse. »
Waacheni; wao ni viongozi vipofu, wanaoongoza vipofu. Kama kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili watatumbukia shimoni.”
15 Pierre, prenant la parole, lui dit: « Explique-nous cette parabole. »
Petro akasema, “Tueleze maana ya huu mfano.”
16 Jésus répondit: « Êtes-vous encore, vous aussi, sans intelligence?
Yesu akawauliza, “Je, bado ninyi hamfahamu?
17 Ne comprenez-vous pas que tout ce qui entre dans la bouche va au ventre, et est rejeté au lieu secret?
Je, hamwelewi kwamba chochote kiingiacho kinywani huenda tumboni, na hatimaye hutolewa nje kikiwa uchafu?
18 Mais ce qui sort de la bouche vient du cœur, et c’est là ce qui souille l’homme.
Lakini kitokacho kinywani hutoka moyoni, na hiki ndicho kimtiacho mtu unajisi.
19 Car c’est du cœur que viennent les mauvaises pensées, les meurtres, les adultères, les impudicités, les vols, les faux témoignages, les paroles injurieuses.
Kwa maana ndani ya moyo hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushahidi wa uongo na masingizio.
20 Voilà ce qui souille l’homme; mais manger sans s’être lavé les mains, cela ne souille pas l’homme. »
Haya ndiyo yamtiayo mtu unajisi; lakini kula bila kunawa mikono hakumtii mtu unajisi.”
21 Jésus étant parti de là, se retira du côté de Tyr et de Sidon.
Yesu aliondoka mahali pale, akaenda sehemu za Tiro na Sidoni.
22 Et voilà qu’une femme cananéenne, de ce pays-là, sortit en criant à haute voix: « Aie pitié de moi, Seigneur, fils de David; ma fille est cruellement tourmentée par le démon. »
Mwanamke mmoja Mkanaani aliyeishi sehemu jirani na hizo akaja kwake akilia, akasema, “Nihurumie, Ee Bwana, Mwana wa Daudi! Binti yangu amepagawa na pepo mchafu, na anateseka sana.”
23 Jésus ne lui répondit pas un mot. Alors ses disciples, s’étant approchés, le prièrent en disant: « Renvoye-la, car elle nous poursuit de ses cris. »
Lakini Yesu hakumjibu neno. Hivyo wanafunzi wake wakamwendea na kumsihi sana, wakisema, “Mwambie aende zake, kwa maana anaendelea kutupigia kelele.”
24 Il répondit: « Je n’ai été envoyé qu’aux brebis perdues de la maison d’Israël. »
Yesu akajibu, “Nimetumwa tu kwa ajili ya kondoo wa Israeli waliopotea.”
25 Mais cette femme vint se prosterner devant lui, en disant: « Seigneur, secoure-moi. »
Lakini yule mwanamke akaja, akapiga magoti mbele ya Yesu, akasema, “Bwana, nisaidie!”
26 Il répondit: « Il n’est pas bien de prendre le pain des enfants pour le jeter aux petits chiens. »
Yesu akajibu, “Si haki kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.”
27 « Il est vrai, Seigneur, dit-elle; mais les petits chiens mangent au moins les miettes qui tombent de la table de leur maître. »
Yule mwanamke akajibu, “Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yanayoanguka kutoka kwenye meza za bwana zao.”
28 Alors Jésus lui dit: « O femme, ta foi est grande: qu’il te soit fait selon ton désir. » Et sa fille fut guérie à l’heure même.
Ndipo Yesu akamwambia, “Mwanamke, imani yako ni kubwa! Iwe kwako kama unavyotaka.” Naye binti yake akapona tangu saa ile.
29 Jésus quitta ces lieux et vint près de la mer de Galilée. Étant monté sur la montagne, il s’y assit.
Yesu akaondoka na kwenda kando ya Bahari ya Galilaya. Kisha akapanda mlimani, akaketi huko.
30 Et de grandes troupes de gens s’approchèrent de lui, ayant avec eux des boiteux, des aveugles, des sourds-muets, des estropiés et beaucoup d’autres malades. Ils les mirent à ses pieds, et il les guérit;
Umati mkubwa wa watu ukamjia, wakiwaleta vilema, vipofu, viwete, bubu na wengine wengi, wakawaweka miguuni pake; naye akawaponya.
31 de sorte que la multitude était dans l’admiration, en voyant les muets parler, les estropiés guéris, les boiteux marcher, les aveugles voir, et elle glorifiait le Dieu d’Israël.
Hao watu wakashangaa walipoona bubu wakisema, vilema wakipona, viwete wakitembea na vipofu wakiona, wakamtukuza Mungu wa Israeli.
32 Cependant Jésus, ayant appelé ses disciples, leur dit: « J’ai compassion de cette foule; car voilà déjà trois jours qu’ils restent près de moi, et ils n’ont rien à manger. Je ne veux pas les renvoyer à jeun, de peur que les forces ne leur manquent en chemin. »
Kisha Yesu akawaita wanafunzi wake, akawaambia, “Ninauhurumia huu umati wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa pamoja nami kwa muda wa siku tatu, na hawana chakula chochote. Nami sipendi kuwaaga wakiwa na njaa, wasije wakazimia njiani.”
33 Les disciples lui dirent: « Où trouver dans un désert assez de pains pour rassasier une si grande foule? »
Wanafunzi wake wakasema, “Tutapata wapi mikate ya kutosha kuwalisha umati huu wa watu mkubwa namna hii, nasi tuko nyikani?”
34 Jésus leur demanda: « Combien avez-vous de pains? » « Sept, lui dirent-ils, et quelques petits poissons. »
Yesu akawauliza, “Mnayo mikate mingapi?” Wakamjibu, “Tunayo mikate saba na visamaki vichache.”
35 Alors il fit asseoir la foule par terre,
Yesu akawaambia ule umati wa watu waketi chini.
36 prit les sept pains et les poissons, et, ayant rendu grâces, il les rompit et les donna à ses disciples, et ceux-ci au peuple.
Kisha akachukua ile mikate saba na wale samaki, naye akiisha kumshukuru Mungu, akavimega na kuwapa wanafunzi wake, nao wakawapa ule umati wa watu.
37 Tous mangèrent et furent rassasiés, et des morceaux qui restaient, on emporta sept corbeilles pleines.
Wote wakala na kushiba. Baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu saba.
38 Or le nombre de ceux qui avaient mangé s’élevait à quatre mille, sans compter les femmes et les enfants.
Idadi ya watu walikuwa wanaume 4,000, bila kuhesabu wanawake na watoto.
39 Après avoir renvoyé le peuple, Jésus monta dans la barque et vint dans le pays de Magédan.
Baada ya kuaga ule umati wa watu, Yesu aliingia katika mashua, akaenda sehemu za Magadani.

< Matthieu 15 >