< Marc 1 >
1 Commencement de l’Évangile de Jésus-Christ, Fils de Dieu.
Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
2 Selon ce qui est écrit dans le prophète Isaïe: « Voici que j’envoie mon messager devant toi, pour te frayer ton chemin.
Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie; yeye atakutayarishia njia yako.
3 Une voix crie dans le désert: Préparez le chemin du Seigneur, aplanissez ses sentiers. »
Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni mapito yake.”
4 Jean parut, baptisant dans le désert, et prêchant le baptême de pénitence pour la rémission des péchés.
Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba ni lazima watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
5 Et tout le pays de Judée et tous les habitants de Jérusalem venaient à lui, et, confessant leurs péchés, ils recevaient de lui le baptême dans le fleuve du Jourdain.
Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
6 Or, Jean était vêtu de poils de chameau; et avait autour de ses reins une ceinture de cuir, et se nourrissait de sauterelles et de miel sauvage.
Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
7 Et il prêchait en disant: « Il vient après moi, celui qui est plus puissant que moi, et je ne suis pas digne de délier, en me baissant, les cordons de sa chaussure.
Naye alihubiri akisema, “Baada yangu anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.
8 Moi, je vous ai baptisés dans l’eau, mais lui vous baptisera dans le Saint-Esprit. »
Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
9 Or, il arriva en ces jours-là que Jésus vint de Nazareth, [ville] de Galilée, et il fut baptisé par Jean dans le Jourdain.
Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani.
10 Et aussitôt, [comme] il sortait de l’eau, il vit les cieux se déchirer et l’Esprit descendre sur lui comme une colombe.
Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa.
11 Et du ciel vint une voix [qui se fit entendre]: « Tu es mon Fils bien-aimé, en toi je me complais. »
Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
12 Et aussitôt l’Esprit le poussa au désert.
Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani,
13 Et il était dans le désert quarante jours, tenté par Satan; et il était parmi les bêtes sauvages, et les anges le servaient.
akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamtumikia.
14 Après que Jean eut été mis en prison, Jésus vint en Galilée, prêchant l’Évangile du royaume de Dieu.
Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema,
15 Et il disait: « Le temps est accompli, et le royaume de Dieu est proche; repentez-vous et croyez à l’Évangile. »
“Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!”
16 Alors qu’il passait le long de la mer de Galilée, il vit Simon et André son frère qui jetaient leurs filets dans la mer, car ils étaient pêcheurs.
Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu.
17 Et Jésus leur dit: « Venez à ma suite, et je vous ferai devenir pêcheurs d’hommes. »
Yesu akawaambia, “Nifuateni nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu.”
18 Et aussitôt, laissant leurs filets, ils le suivirent.
Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
19 Et avançant un peu, il vit Jacques, [fils] de Zébédée, et Jean son frère, qui étaient, eux aussi, dans une barque, réparant leurs filets.
Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
20 Et il les appela aussitôt; et, laissant leur père Zébédée dans la barque avec les employés, ils partirent à sa suite.
Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
21 Et ils entrèrent à Capharnaüm, et dès le [jour du] sabbat, entrant dans la synagogue, il se mit à enseigner.
Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika Sunagogi, akaanza kufundisha.
22 Et ils étaient frappés de sa doctrine, car il les enseignait comme ayant autorité, et non comme les scribes.
Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama walimu wao wa Sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.
23 Et aussitôt il se trouva dans leur synagogue un homme possédé d’un esprit impur, qui s’écria
Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu,
24 en disant: « Qu’avons-nous à faire avec toi, Jésus de Nazareth? Tu es venu pour nous perdre! Je sais qui tu es, le Saint de Dieu. »
akapaaza sauti, “Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: wewe ni Mtakatifu wa Mungu!”
25 Mais Jésus, le menaçant: « Tais-toi, dit-il, et sors de cet homme. »
Yesu akamkemea, “Nyamaza! Mtoke mtu huyu.”
26 Et l’esprit impur, l’agitant violemment, sortit de lui en jetant un grand cri.
Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.
27 Et tous furent saisis d’étonnement, de sorte qu’ils se demandaient entre eux en disant: « Qu’est-ce que ceci? Quelle est cette doctrine nouvelle? Car il commande avec autorité, même aux esprits impurs, et ils lui obéissent. »
Watu wote wakashangaa, wakaulizana, “Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
28 Et sa renommée se répandit aussitôt partout, dans tout le pays qui avoisine la Galilée.
Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika wilaya ya Galilaya.
29 Et aussitôt, sortant de la synagogue, ils allèrent dans la maison de Simon et d’André, avec Jacques et Jean.
Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.
30 Or, la belle-mère de Simon était au lit, ayant la fièvre; et aussitôt ils lui parlèrent à son sujet.
Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.
31 Et s’approchant, il la fit lever, [en] la prenant par la main; et aussitôt la fièvre la quitta, et elle se mit à les servir.
Yesu akamwendea huyo mama, akamshika mkono, akamwinua. Na ile homa ikamwacha, akaanza kuwatumikia.
32 Sur le soir, lorsque le soleil fut couché, on se mit à lui amener tous ceux [qui] étaient malades et les démoniaques,
Jioni, jua lilipokwisha tua, wakamletea Yesu wagonjwa wote na watu waliopagawa na pepo.
33 et toute la ville était rassemblée devant la porte.
Watu wote wa mji ule wakakusanyika nje ya mlango.
34 Et il guérit beaucoup de malades affligés de diverses infirmités, et il chassa beaucoup de démons; et il ne leur permettait pas de parler, parce qu’ils le connaissaient.
Naye Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa mbalimbali; aliwafukuza pepo wengi, lakini hakuwaruhusu kusema kitu maana walikuwa wanamjua yeye ni nani.
35 Et au petit matin, [alors qu’il faisait encore] grandement nuit, il se leva, sortit, et s’en alla dans un lieu solitaire, [et] il y pria.
Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
36 Et Simon et ceux [qui étaient] avec lui le recherchèrent;
Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
37 et l’ayant trouvé, ils lui dirent: « Tout [le monde] te cherche. »
Walipomwona wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta.”
38 Il leur répondit: « Allons ailleurs dans les bourgades voisines, afin que j’y prêche aussi; car c’est pour cela que je suis sorti. »
Yesu akawaambia, “Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo.”
39 Et il prêchait dans leurs synagogues, parcourant la Galilée entière, et chassait les démons.
Basi, akaenda kila mahali Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
40 Un lépreux vint à lui, et se jetant à genoux, il lui dit [d’un ton] suppliant: « Si tu [le] veux, tu peux me purifier. »
Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba, “Ukitaka, waweza kunitakasa!”
41 Ému de compassion, Jésus étendit la main, le toucha, en disant: « Je [le] veux, sois purifié. »
Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, “Nataka, takasika!”
42 Et aussitôt [qu’il eut parlé], la lèpre le quitta, et il fut purifié.
Mara ukoma ukamwacha mtu huyo, akatakasika.
43 [Jésus] en le sermonnant le renvoya aussitôt,
Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwonya vikali,
44 et lui dit: « Garde-toi d’en parler à personne; mais va te montrer au prêtre, et offre pour ta purification ce que Moïse a ordonné pour leur servir de témoignage. »
“Usimwambie mtu yeyote jambo hili, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani; kisha utoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona.”
45 Mais cet homme étant parti, se mit à raconter et à publier partout ce qui s’était passé: de sorte que Jésus ne pouvait plus entrer publiquement dans une ville; il se tenait dehors, dans des lieux solitaires, et l’on venait à lui de tous côtés.
Lakini huyo mtu akaenda, akaanza kueneza habari hiyo kila mahali na kusema mambo mengi hata Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote waziwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande.