< Luc 9 >
1 Ayant assemblé les Douze, Jésus leur donna puissance et autorité sur tous les démons, et le pouvoir de guérir les maladies.
Yesu kisha akawaita wale kumi na wawili pamoja, akawapa mamlaka na uwezo wa kutoa pepo wachafu wote na kuponya magonjwa yote,
2 Et il les envoya prêcher le royaume de Dieu et guérir les malades,
kisha akawatuma waende wakahubiri Ufalme wa Mungu na kuponya wagonjwa.
3 et il leur dit: « Ne prenez rien pour le voyage, ni bâton, ni sac, ni pain, ni argent, et n’ayez pas deux tuniques.
Akawaagiza akisema, “Msichukue chochote safarini: sio fimbo, wala mkoba, wala mkate, wala fedha, hata msichukue kanzu ya ziada.
4 Dans quelque maison que vous entriez, demeurez-y jusqu’à ce que vous partiez de ce lieu.
Katika nyumba yoyote mwingiayo, kaeni humo hadi mtakapoondoka katika mji huo.
5 Si l’on refuse de vous recevoir, sortez de cette ville et secouez même la poussière de vos pieds en témoignage contre eux. »
Kama watu wasipowakaribisha, mnapoondoka katika mji wao, kungʼuteni mavumbi kutoka kwenye miguu yenu ili kuwa ushuhuda dhidi yao.”
6 Les disciples étant partis allèrent de village en village, prêchant l’Evangile et opérant partout des guérisons.
Hivyo wale wanafunzi wakaondoka wakaenda kutoka kijiji hadi kijiji, wakihubiri habari njema na kuponya wagonjwa kila mahali.
7 Cependant Hérode le tétrarque entendit parler de tout ce que faisait Jésus, et il ne savait que penser;
Basi Mfalme Herode, mtawala wa Galilaya, alisikia habari za yote yaliyotendeka. Naye akafadhaika, kwa kuwa baadhi ya watu walikuwa wakisema Yohana Mbatizaji amefufuliwa kutoka kwa wafu.
8 car les uns disaient: « Jean est ressuscité des morts «; d’autres: « Élie a paru «; d’autres: « Un des anciens prophètes est ressuscité. »
Wengine wakasema Eliya amewatokea, na wengine wakasema kwamba mmoja wa manabii wa kale amefufuka.
9 Hérode dit: « Quant à Jean, je l’ai fait décapiter. Quel est donc cet homme, de qui j’entends dire de telles choses? » Et il cherchait à le voir.
Herode akasema, “Yohana nilimkata kichwa. Lakini ni nani huyu ambaye ninasikia mambo kama haya kumhusu?” Akatamani sana kumwona.
10 Les apôtres, étant de retour, racontèrent à Jésus tout ce qu’ils avaient fait. Il les prit avec lui et se retira à l’écart dans un lieu désert, près d’une ville nommée Bethsaïde.
Mitume wake waliporudi, wakamweleza Yesu yote waliyofanya. Akawachukua, akaenda nao faraghani mpaka mji uitwao Bethsaida.
11 Lorsque le peuple l’eut appris, il le suivit; Jésus les accueillit, et il leur parla du royaume de Dieu, et il rendit la santé à ceux qui en avaient besoin.
Lakini umati wa watu ukafahamu alikokwenda, ukamfuata. Akawakaribisha na kunena nao kuhusu Ufalme wa Mungu na kuwaponya wale wote waliokuwa wanahitaji uponyaji.
12 Comme le jour commençait à baisser, les Douze vinrent lui dirent: « Renvoyez le peuple, afin que, se répandant dans les villages et les hameaux d’alentour, ils y trouvent un abri et de la nourriture; car nous sommes ici dans un lieu désert. »
Ilipokaribia jioni, wale mitume kumi na wawili wakaenda kwa Yesu na kumwambia, “Waage makutano ili waende vijijini jirani na mashambani, ili wapate chakula na mahali pa kulala, kwa maana hapa tuko nyikani.”
13 Il leur répondit: « Donnez-leur vous-mêmes à manger. » Ils lui dirent: « Nous n’avons que cinq pains et deux poissons, à moins peut-être que nous n’allions nous-mêmes acheter de quoi nourrir tout ce peuple! »
Yesu akawajibu, “Ninyi wapeni chakula.” Nao wakajibu, “Hatuna zaidi ya mikate mitano na samaki wawili. Labda twende tukanunue chakula cha kuwatosha watu hawa wote.”
14 Car il y avait environ cinq mille hommes. Jésus dit à ses disciples: « Faites-les asseoir par groupes de cinquante. »
Walikuwako wanaume wapatao 5,000. Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Waketisheni katika makundi ya watu hamsini hamsini.”
15 Ils agirent ainsi et tout le monde s’assit.
Wanafunzi wakafanya hivyo, wakawaketisha wote.
16 Alors Jésus prit les cinq pains et les deux poissons, et levant les yeux au ciel, il prononça une bénédiction, les rompit et les donna à ses disciples pour les servir au peuple.
Yesu akaichukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama mbinguni, akavibariki na kuvimega. Kisha akawapa wanafunzi ili wawagawie watu.
17 Tous mangèrent et furent rassasiés, et des morceaux qui étaient de reste, on emporta douze corbeilles.
Wote wakala, wakashiba. Nao wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu kumi na viwili.
18 Un jour qu’il priait dans un lieu solitaire, ayant ses disciples avec lui, il leur fit cette question: « Qui suis-je, au dire des foules? »
Wakati mmoja, Yesu alipokuwa akiomba faraghani, nao wanafunzi wake wakiwa pamoja naye, akawauliza, “Watu husema mimi ni nani?”
19 Ils répondirent: « Les uns disent Jean Baptiste; d’autres Élie; d’autres, qu’un des anciens prophètes est ressuscité. —
Wakamjibu, “Baadhi husema wewe ni Yohana Mbatizaji, wengine husema ni Eliya, na bado wengine husema kwamba ni mmoja wa manabii wa kale amefufuka kutoka kwa wafu.”
20 Et vous, leur demanda-t-il, qui dites-vous que je suis? » Pierre répondit: « Le Christ de Dieu. »
Kisha akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu, “Wewe ndiwe Kristo wa Mungu.”
21 Mais il leur enjoignit d’un ton sévère de ne le dire à personne.
Yesu akawakataza wasimwambie mtu yeyote jambo hilo.
22 « Il faut, ajouta-t-il, que le Fils de l’homme souffre beaucoup, qu’il soit rejeté par les Anciens, par les Princes des prêtres et par les scribes, qu’il soit mis à mort et qu’il ressuscite le troisième jour. »
Yesu akasema, “Imempasa Mwana wa Adamu kupata mateso mengi na kukataliwa na wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa sheria, na itampasa auawe, lakini siku ya tatu kufufuliwa kutoka mauti.”
23 Puis, s’adressant à tous, il dit: « Si quelqu’un veut venir après moi, qu’il se renonce lui-même, qu’il porte sa croix chaque jour, et me suive.
Kisha akawaambia wote, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake kila siku, anifuate.
24 Car celui qui voudra sauver sa vie la perdra, et celui qui perdra sa vie à cause de moi, la sauvera.
Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu atayaokoa.
25 Que sert-il à un homme de gagner le monde entier, s’il se ruine ou se perd lui-même?
Je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akapoteza au kuangamiza nafsi yake?
26 Et si quelqu’un rougit de moi et de mes paroles, le Fils de l’homme rougira de lui, lorsqu’il viendra dans sa gloire et dans celle du Père et des saints anges.
Mtu yeyote akinionea aibu mimi na maneno yangu, Mwana wa Adamu naye atamwonea aibu atakapokuja katika utukufu wake na katika utukufu wa Baba, pamoja na malaika watakatifu.
27 Je vous le dis en vérité, quelques-uns de ceux qui sont ici présents ne goûteront pas la mort, qu’ils n’aient vu le royaume de Dieu. »
Amin, nawaambia, wako baadhi ya watu waliosimama hapa ambao hawataonja mauti kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu.”
28 Environ huit jours après qu’il eut dit ces paroles, Jésus prit avec lui Pierre, Jacques et Jean, et monta sur la montagne pour prier.
Yapata siku nane baada ya Yesu kusema hayo, aliwachukua Petro, Yakobo na Yohana, akaenda nao mlimani kuomba.
29 Pendant qu’il priait, l’aspect de son visage changea, et ses vêtements devinrent éblouissants de blancheur.
Alipokuwa akiomba, sura ya uso wake ikabadilika, nayo mavazi yake yakametameta kama mwanga wa umeme wa radi.
30 Et voilà que deux hommes conversaient avec lui: c’étaient Moïse et Élie,
Ghafula wakawaona watu wawili, ndio Mose na Eliya, wakizungumza naye.
31 apparaissant dans la gloire; ils s’entretenaient de sa mort qui devait s’accomplir dans Jérusalem.
Walionekana katika utukufu wakizungumza na Yesu kuhusu kifo chake ambacho kingetokea huko Yerusalemu.
32 Pierre et ses compagnons étaient accablés de sommeil; mais s’étant tenus éveillés, ils virent la gloire de Jésus, et les deux hommes qui étaient avec lui.
Petro na wenzake walikuwa wamelala usingizi mzito. Walipoamka, wakaona utukufu wa Yesu na wale watu wawili waliokuwa wamesimama pamoja naye.
33 Au moment où ceux-ci s’éloignaient de lui, Pierre dit à Jésus: « Maître, il nous est bon d’être ici; dressons trois tentes, une pour toi, une pour Moïse et une pour Elie », il ne savait ce qu’il disait.
Mose na Eliya walipokuwa wanaondoka, Petro akamwambia Yesu, “Bwana, ni vizuri tukae hapa! Tutajenga vibanda vitatu: kimoja chako, kingine cha Mose na kingine cha Eliya.” Lakini Petro alikuwa hajui asemacho.
34 Comme il parlait ainsi, une nuée vint les couvrir de son ombre et les disciples furent saisis de frayeur tandis qu’ils entraient dans la nuée.
Alipokuwa bado anazungumza, pakatokea wingu, likawafunika, nao wakaogopa walipoingia mle kwenye wingu.
35 Et de la nuée sortit une voix qui disait: « Celui-ci est mon Fils bien-aimé, écoutez-le. »
Sauti ikatoka kwenye lile wingu ikisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa, niliyemchagua. Msikieni yeye.”
36 Pendant que la voix parlait, Jésus se trouva seul. Les disciples gardèrent le silence, et ils ne racontèrent à personne, en ce temps-là, rien de ce qu’ils avaient vu.
Baada ya sauti hiyo kusema, walimkuta Yesu akiwa peke yake. Wale wanafunzi wakalihifadhi jambo hili, wala kwa wakati huo hawakumwambia mtu yeyote yale waliyokuwa wameyaona.
37 Le jour suivant, lorsqu’ils furent descendus de la montagne, une foule nombreuse vint au-devant de Jésus.
Kesho yake waliposhuka kutoka mlimani, alikutana na umati mkubwa wa watu.
38 Et un homme s’écria du milieu de la foule: « Maître, je t’en supplie, jette un regard sur mon fils, car c’est mon seul enfant.
Mtu mmoja katika ule umati wa watu akapaza sauti, akasema, “Mwalimu, naomba umwangalie mwanangu, kwani ndiye mtoto wangu wa pekee.
39 Un esprit s’empare de lui, et aussitôt il pousse des cris; l’esprit l’agite avec violence en le faisant écumer, et à peine le quitte-t-il après l’avoir tout meurtri.
Mara kwa mara pepo mchafu humpagaa na kumfanya apige kelele, kisha humwangusha na kumtia kifafa hata akatokwa na povu kinywani. Huyo pepo mchafu anamtesa sana, na hamwachi ila mara chache.
40 J’ai prié vos disciples de le chasser, et ils ne l’ont pu. —
Niliwaomba wanafunzi wako wamtoe huyo pepo mchafu, lakini hawakuweza.”
41 O race incrédule et perverse, répondit Jésus, jusques à quand serai-je avec vous et vous supporterai-je? Amène ici ton fils. »
Yesu akawajibu, “Enyi kizazi kisichoamini na kilichopotoka! Nitakaa nanyi na kuwavumilia mpaka lini? Mlete mwanao hapa.”
42 Et comme l’enfant s’approchait, le démon le jeta par terre et l’agita violemment.
Hata yule mtoto alipokuwa akija, yule pepo mchafu akamwangusha, akamtia kifafa. Lakini Yesu akamkemea yule pepo mchafu amtoke, akamponya yule mtoto, na akamrudisha kwa baba yake.
43 Mais Jésus menaça l’esprit impur, guérit l’enfant et le rendit à son père.
Watu wote wakastaajabia uweza mkuu wa Mungu. Wakati bado watu walikuwa wanastaajabia hayo yote aliyokuwa akiyafanya Yesu, yeye akawaambia wanafunzi wake:
44 Et tous furent frappés de la grandeur de Dieu. Tandis que chacun était dans l’admiration de ce que faisait Jésus, il dit à ses disciples: « Vous, écoutez bien ceci. Le Fils de l’homme doit être livré entre les mains des hommes. »
“Sikilizeni kwa makini haya nitakayowaambia sasa: Mwana wa Adamu atasalitiwa na kutiwa mikononi mwa watu.”
45 Mais ils ne comprenaient pas cette parole; elle était voilée pour eux, de sorte qu’ils n’en avaient pas l’intelligence, et ils craignaient de l’interroger à ce sujet.
Lakini wao hawakuelewa alimaanisha nini. Maana ya maneno hayo ilifichika kwao, hivyo hawakuyaelewa, nao wakaogopa kumuuliza maana yake.
46 Or, une pensée se glissa dans leur esprit, savoir lequel d’entre eux était le plus grand.
Kukazuka mabishano miongoni mwa wanafunzi kuhusu ni nani miongoni mwao atakayekuwa mkuu kuliko wote.
47 Jésus, voyant les pensées de leur cœur, prit un petit enfant, le mit près de lui,
Lakini Yesu akayatambua mawazo yao, naye akamchukua mtoto mdogo, akamsimamisha kando yake.
48 et leur dit: « Quiconque reçoit en mon nom ce petit enfant, me reçoit; et quiconque me reçoit, reçoit Celui qui m’a envoyé. Car celui d’entre vous tous qui est le plus petit, c’est celui-là qui est grand. »
Kisha akawaambia, “Yeyote amkaribishaye mtoto huyu mdogo kwa Jina langu, anikaribisha mimi, na yeyote atakayenikaribisha mimi, atakuwa amemkaribisha yeye aliyenituma. Kwa maana yeye aliye mdogo miongoni mwenu, ndiye aliye mkuu kuliko wote.”
49 Jean, prenant la parole, dit: « Maître, nous avons vu un homme qui chasse les démons en votre nom, et nous l’en avons empêché, parce qu’il ne va pas avec nous. —
Yohana akasema, “Bwana, tumemwona mtu akitoa pepo wachafu kwa jina lako, nasi tukamzuia, kwa sababu yeye si mmoja wetu.”
50 Ne l’en empêchez pas, lui répondit Jésus, car celui qui n’est pas contre vous est pour vous. »
Yesu akasema, “Msimzuie, kwa sababu yeyote ambaye si kinyume nanyi, yu upande wenu.”
51 Quand les jours où il devait être enlevé du monde furent près de s’accomplir, il prit la résolution d’aller à Jérusalem,
Wakati ulipokaribia wa yeye kuchukuliwa mbinguni, alikaza uso wake kwenda Yerusalemu.
52 Il envoya devant lui des messagers, qui se mirent en route, et entrèrent dans un bourg des Samaritains pour préparer sa réception;
Akatuma watu wamtangulie, nao wakaenda katika kijiji kimoja cha Samaria kumwandalia kila kitu;
53 mais les habitants refusèrent de le recevoir, parce qu’il se dirigeait vers Jérusalem.
lakini watu wa kijiji kile hawakumkaribisha kwa sababu alikuwa anakwenda zake Yerusalemu.
54 Ce que voyant, ses disciples Jacques et Jean dirent: « Seigneur, veux-tu que nous commandions que le feu descende du ciel et les consume? »
Wanafunzi wake, yaani Yakobo na Yohana, walipoona hayo, wakasema: “Bwana, unataka tuagize moto kutoka mbinguni ili uwaangamize?”
55 Jésus, s’étant retourné, les reprit en disant: « Vous ne savez pas de quel esprit vous êtes!
Yesu akageuka na kuwakemea,
56 Le Fils de l’homme est venu, non pour perdre les vies d’hommes, mais pour les sauver. » Et ils allèrent dans une autre bourgade.
nao wakaenda kijiji kingine.
57 Pendant qu’ils étaient en chemin, un homme lui dit: « Je te suivrai partout où tu iras. »
Walipokuwa njiani wakienda, mtu mmoja akamwambia Yesu, “Nitakufuata kokote uendako.”
58 Jésus lui répondit: « Les renards ont des tanières, et les oiseaux du ciel des nids; mais le Fils de l’homme n’a pas où reposer sa tête. »
Yesu akamjibu, “Mbweha wana mapango, nao ndege wa angani wana viota, lakini Mwana wa Adamu hana mahali pa kulaza kichwa chake.”
59 Il dit à un autre: « Suis-moi. » Celui-ci répondit: « Seigneur, permettez-moi d’aller auparavant ensevelir mon père. »
Yesu akamwambia mtu mwingine, “Nifuate.” Mtu huyo akamjibu, “Bwana, niruhusu kwanza nikamzike baba yangu.”
60 Mais Jésus lui dit: « Laisse les morts ensevelir leurs morts; pour toi, va annoncer le royaume de Dieu. »
Yesu akamwambia, “Waache wafu wawazike wafu wao, bali wewe nenda ukautangaze Ufalme wa Mungu.”
61 Un autre lui dit: « Je te suivrai, Seigneur, mais permets-moi d’aller auparavant faire mes adieux à ceux de ma maison. »
Mtu mwingine akamwambia, “Bwana, nitakufuata lakini naomba kwanza nikawaage jamaa yangu.”
62 Jésus lui répondit: « Quiconque met la main à la charrue et regarde en arrière, n’est pas propre au royaume de Dieu. »
Yesu akamwambia, “Mtu yeyote atiaye mkono wake kulima, kisha akatazama nyuma, hafai kwa Ufalme wa Mungu.”