< Luc 22 >

1 La fête des Azymes, qu’on appelle la Pâque, approchait;
Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
2 et les Princes des prêtres et les scribes cherchaient comment ils feraient mourir Jésus; car ils craignaient le peuple.
Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
3 Or, Satan entra dans Judas, surnommé Iscariote, du nombre des Douze;
Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
4 et celui-ci alla s’entendre avec les Princes des prêtres et les magistrats, sur la manière de le leur livrer.
Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
5 Eux, pleins de joie, promirent de lui donner de l’argent.
Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
6 Il s’engagea de son côté, et il cherchait une occasion favorable de leur livrer Jésus à l’insu de la foule.
Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
7 Arriva le jour des Azymes, où l’on devait immoler la Pâque.
Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
8 Jésus envoya Pierre et Jean: « Allez, leur dit-il, nous préparer le repas pascal. »
Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, “Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka.”
9 Ils lui dirent: « Où veux-tu que nous le préparions? »
Nao wakamwuliza, “Unataka tuiandae wapi?”
10 Il leur répondit: « En entrant dans la ville, t rencontrerez un homme portant une cruche d’eau; suivez-le dans la maison où il entrera,
Akawaambia, “Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
11 et vous direz au maître de cette maison: Le Maître te fait dire: Où est la salle où je mangerai la Pâque avec mes disciples?
Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
12 Et il vous montrera un grand cénacle meublé: préparez-y ce qu’il faut. »
Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo.”
13 Ils partirent, et trouvèrent les choses comme il le leur avait dit; et ils préparèrent la Pâque.
Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
14 L’heure étant venue, Jésus se mit à table, et les douze Apôtres avec lui;
Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
15 et il leur dit: « J’ai désiré d’un grand désir de manger cette Pâque avec vous avant de souffrir.
Akawaambia, “Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
16 Car, je vous le dis, je ne la mangerai plus jusqu’à la Pâque parfaite, célébrée dans le royaume de Dieu. »
Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu.”
17 Et prenant une coupe, il rendit grâces et dit: « Prenez et partagez entre vous.
Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, “Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
18 Car, je vous le dis, je ne boirai plus du fruit de la vigne, jusqu’à ce que le royaume de Dieu soit venu. »
Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
19 Puis il prit du pain, et ayant rendu grâces, il le rompit et le leur donna, en disant: « Ceci est mon corps, qui est donné pour vous: faites ceci en mémoire de moi. »
Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, “Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka.”
20 Il fit de même pour la coupe, après le souper, disant: « Cette coupe est la nouvelle alliance en mon sang, lequel est versé pour vous.
Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
21 Cependant voici que la main de celui qui me trahit est avec moi à cette table.
“Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
22 Quant au Fils de l’homme, il va selon ce qui a été décrété; mais malheur à l’homme par qui il est trahi! »
Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti.”
23 Et les disciples se mirent à se demander les uns aux autres quel était celui d’entre eux qui devait faire cela.
Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
24 Il s’éleva aussi parmi eux une dispute, pour savoir lequel d’entre eux devait être estimé le plus grand.
Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
25 Jésus leur dit: « Les rois des nations dominent sur elles, et ceux qui leur commandent sont appelés Bienfaiteurs.
Yesu akawaambia, “Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
26 Pour vous, ne faites pas ainsi; mais que le plus grand parmi vous soit comme le dernier, et celui qui gouverne comme celui qui sert.
Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
27 Car quel est le plus grand, de celui qui est à table, ou de celui qui sert? N’est-ce pas celui qui est à table? Et moi, cependant, je suis au milieu de vous comme celui qui sert.
Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
28 Vous, vous êtes demeurés avec moi dans mes épreuves;
“Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
29 et moi, je vous prépare un royaume, comme mon Père me l’a préparé,
na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
30 afin que vous mangiez et bu viez à ma table dans mon royaume, et que vous soyez assis sur des trônes, pour juger les douze tribus d’Israël. »
Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
31 Et le Seigneur dit: « Simon, Simon, voici que Satan t’a réclamés pour te cribler comme le froment;
“Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
32 mais j’ai prié pour toi, afin que ta foi ne défaille pas; et toi, quand tu seras converti, affermis tes frères. —
Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako.”
33 Seigneur, lui dit Pierre, je suis prêt à aller avec toi et en prison et à la mort. »
Naye Petro akamjibu, “Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa.”
34 Jésus lui répondit: « Je te le dis, Pierre, le coq ne chantera pas aujourd’hui, que tu n’aies nié trois fois de me connaître. »
Yesu akamjibu, “Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu.”
35 Il dit encore à ses disciples: « Quand je vous ai envoyés sans bourse, ni sac, ni chaussures, avez-vous manqué de quelque chose? —
Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, “Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?” Wakajibu, “La.”
36 De rien, » lui dirent-ils. Il ajouta: « Mais maintenant, que celui qui a une bourse la prenne, et de même celui qui a un sac; et que celui qui n’a pas d’épée vende son manteau, et en achète une.
Naye akawaambia, “Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
37 Car, je vous le dis, il faut encore que cette parole de l’Écriture s’accomplisse en moi: Il a été mis au rang des malfaiteurs. En effet, ce qui me concerne touche à sa fin. »
Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake.”
38 Ils lui dirent: « Seigneur, il y a ici deux épées. » Il leur répondit: « C’est assez. »
Nao wakasema, “Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili.” Naye akasema, “Basi!”
39 Etant sorti, il s’en alla, selon sa coutume, vers le mont des Oliviers, et ses disciples le suivirent.
Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
40 Lorsqu’il fut arrivé dans ce lieu, il leur dit: « Priez, afin de ne pas tomber en tentation. »
Alipofika huko akawaambia, “Salini, msije mkaingia katika kishawishi.”
41 Puis il s’éloigna d’eux à la distance d’un jet de pierre; et s’étant mis à genoux, il priait,
Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
42 disant: « Père, si tu veux, éloignes de moi ce calice! Cependant que ce ne soit pas ma volonté, mais la vôtre qui se fasse. »
“Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu.”
43 Alors lui apparut du ciel un ange qui le fortifiait.
Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
44 Et se trouvant en agonie, il priait plus instamment, et sa sueur devint comme des gouttes de sang découlant jusqu’à terre.
Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
45 Après avoir prié, il se leva et vint vers les disciples, qu’il trouva endormis de tristesse.
Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
46 Et il leur dit: « Pourquoi dormez-vous? Levez-vous et priez, afin de ne pas entrer en tentation. »
Akawaambia, “Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi.”
47 Comme il parlait encore, voici qu’une troupe de gens parut; celui qu’on appelait Judas, l’un des Douze, marchait en tête. Il s’approcha de Jésus pour le baiser.
Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
48 Et Jésus lui dit: « Judas, tu livres le Fils de l’homme par un baiser! »
Lakini Yesu akamwambia, “Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?”
49 Ceux qui étaient avec Jésus, voyant ce qui allait arriver, lui dirent: « Seigneur, si nous frappions de l’épée? »
Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, “Bwana, tutumie panga zetu?”
50 Et l’un d’eux frappa le serviteur du grand prêtre, et lui emporta l’oreille droite.
Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
51 Mais Jésus dit: « Restez-en là. » Et, ayant touché l’oreille de cet homme, il le guérit.
Hapo, Yesu akasema, “Acha! Hii inatosha.” Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
52 Puis, s’adressant aux Princes des prêtres, aux officiers du temple et aux Anciens qui étaient venus pour le prendre, il leur dit: « Vous êtes venus comme après un brigand, avec des épées et des bâtons.
Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: “Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
53 J’étais tous les jours avec vous dans le temple, et vous n’avez mis pas la main sur moi. Mais voici votre heure et la puissance des ténèbres. »
Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza.”
54 S’étant saisis de lui, ils l’emmenèrent et le conduisirent dans la maison du grand prêtre; Pierre suivait de loin.
Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
55 Ayant allumé du feu au milieu de la cour, ils s’assirent autour, et Pierre s’assit parmi eux.
Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
56 Une servante, qui le vit assis devant le feu, l’ayant regardé fixement, dit: « Cet homme était aussi avec lui. »
Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, “Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu.”
57 Mais Pierre renia Jésus, en disant: « Femme, je ne le connais point. »
Lakini Petro akakana akisema, “Wee! simjui mimi.”
58 Peu après, un autre l’ayant vu, dit: « Tu es aussi de ces gens-là. » Pierre répondit: « Mon ami, je n’en suis point. »
Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, “Wewe ni mmoja wao.” Lakini Petro akajibu “Bwana we; si mimi!”
59 Une heure s’était écoulée, lorsqu’un autre se mit à dire avec assurance: « Certainement cet homme était aussi avec lui, car il est de la Galilée. »
Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, “Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati.”
60 Pierre répondit: « Mon ami, je ne sais ce que tu veux dire. » Et aussitôt, comme il parlait encore, le coq chanta.
Lakini Petro akasema, “Bwana wee; sijui hata unachosema!” Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
61 Et le Seigneur, s’étant retourné, regarda Pierre, et Pierre se souvint de la parole que le Seigneur lui avait dite: « Avant que le coq chante, tu me renieras trois fois. »
Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: “Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
62 Et étant sorti de la maison, Pierre pleura amèrement.
Hapo akatoka nje, akalia sana.
63 Or, ceux qui tenaient Jésus se moquaient de lui et le frappaient.
Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
64 Ils lui bandèrent les yeux, et, le frappant au visage, ils l’interrogeaient, disant: « Devine qui t’a frappé. »
Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, “Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!”
65 Et ils proféraient contre lui beaucoup d’autres injures.
Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
66 Dès qu’il fit jour, les Anciens du peuple, les Princes des prêtres et les scribes se réunirent, et amenèrent Jésus dans leur assemblée. Ils dirent: « Si tu es le Christ, dis-le-nous. »
Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
67 Il leur répondit: « Si je vous le dis, vous ne le croirez pas;
Nao wakamwambia, “Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?” Lakini Yesu akawaambia, “Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
68 et si je vous interroge, vous ne me répondrez pas et ne me relâcherez pas.
na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
69 Désormais le Fils de l’homme sera assis à la droite de la puissance de Dieu. »
Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi.”
70 Alors ils dirent tous: « Tu es donc le Fils de Dieu? » Il leur répondit: « Vous le dites, je le suis. »
Hapo wote wakasema, “Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?” Naye akasema, “Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye.”
71 Et ils dirent: « Qu’avons-nous encore besoin de témoignage? Nous l’avons nous-mêmes entendu de sa bouche. »
Nao wakasema, “Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe.”

< Luc 22 >