< Luc 20 >

1 Un de ces jours-là, comme Jésus enseignait le peuple dans le temple, et qu’il annonçait la bonne nouvelle, les Princes des prêtres et les scribes survinrent avec les Anciens,
Siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuwahubiria juu ya Habari Njema, makuhani wakuu na walimu wa Sheria pamoja na wazee walifika,
2 et lui dirent: « Dites-nous par quelle autorité tu fais ces choses, ou qui t’ as donné cette autorité? »
wakasema, “Tuambie! Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani?”
3 Jésus leur répondit: « Moi aussi je vous ferai une question. Répondez-moi.
Yesu akawaambia, “Na mimi nitawaulizeni swali:
4 Le baptême de Jean était-il du ciel, ou des hommes? »
mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa Mungu au kwa watu?”
5 Mais ils faisaient entre eux cette réflexion: « Si nous répondons: Du ciel, il nous dira: Pourquoi n’avez-vous pas cru en lui?
Lakini wao wakajadiliana hivi: “Tukisema yalitoka mbinguni, yeye atatuuliza: Mbona hamkumsadiki?
6 Et si nous répondons: Des hommes, tout le peuple nous lapidera, car il est persuadé que Jean était un prophète. »
Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii.”
7 Ils lui répondirent donc qu’ils ne savaient d’où il était.
Basi, wakamwambia, “Hatujui mamlaka hayo yalitoka wapi.”
8 « Et Moi, leur dit Jésus, je ne vous dis pas non plus par quelle autorité je fais ces choses. »
Yesu akawaambia, “Hata mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”
9 Alors il se mit à dire au peuple cette parabole: « Un homme planta une vigne, et la loua à des vignerons; puis il s’en alla pour un temps assez long en pays étranger.
Yesu akaendelea kuwaambia watu mfano huu: “Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima; kisha akasafiri hadi nchi ya mbali, akakaa huko kwa muda mrefu.
10 La saison étant venue, il envoya un serviteur aux vignerons, afin qu’ils lui donnassent du produit de la vigne. Mais eux, l’ayant battu, le renvoyèrent les mains vides.
Wakati wa mavuno, mtu huyo alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima, akachukue sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga mtumishi huyo wakamrudisha mikono mitupu.
11 Il envoya encore un autre serviteur; mais, l’ayant aussi battu et traité indignement, ils le renvoyèrent les mains vides.
Yule bwana akamtuma tena mtumishi mwingine; lakini wao wakampiga huyo vilevile na kumtendea vibaya, wakamrudisha mikono mitupu.
12 Il en envoya un troisième; mais, lui aussi, les vignerons le blessèrent et le jetèrent dehors.
Akamtuma tena wa tatu; huyu naye, baada ya kumwumiza, wakamfukuza.
13 Alors le maître de la vigne se dit: Que ferai-je?’enverrai mon fils bien-aimé; peut-être qu’en le voyant ils auront pour lui du respect.
Yule mwenye shamba akafikiri: Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpenzi; labda watamjali yeye.
14 Mais lorsque les vignerons le virent, ils se dirent entre eux: Celui-ci est l’héritier, tuons-le, afin que l’héritage soit à nous.
Wale wakulima walipomwona tu, wakasemezana: Huyu ndiye mrithi. Basi, tumwue ili urithi wake uwe wetu.
15 Et l’ayant jeté hors de la vigne, ils le tuèrent. Que leur fera donc le maître de la vigne?
Basi, wakamtoa nje ya lile shamba la mizabibu, wakamwua.” Yesu akauliza, “Yule mwenye shamba atawafanya nini hao wakulima?
16 Il viendra et exterminera ces vignerons, et donnera sa vigne à d’autres. » Ce qu’ayant entendu, ils dirent: « A Dieu ne plaise! »
Atakuja kuwaangamiza wakulima hao, na atawapa wakulima wengine hilo shamba la mizabibu.” Watu waliposikia maneno hayo, walisema: “Hasha! Yasitukie hata kidogo!”
17 Mais, fixant le regard sur eux, Jésus dit: « Qu’est-ce donc que cette parole de l’Ecriture: La pierre qu’ont rejetée ceux qui bâtissaient est devenue la pierre angulaire?
Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, “Maandiko haya Matakatifu yana maana gani basi? Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi!
18 Quiconque tombera sur cette pierre sera brisé; et celui sur qui elle tombera, sera écrasé. »
Mtu yeyote akianguka juu ya jiwe hilo, atavunjika vipandevipande; na likimwangukia mtu yeyote, litamsaga kabisa.”
19 Les Princes des prêtres et les scribes cherchèrent à se saisir de lui à l’heure même; mais la crainte du peuple les retint, car ils comprenaient bien que c’était pour eux que Jésus avait dit cette parabole.
Walimu wa Sheria na makuhani wakuu walifahamu kwamba mfano huo ulikuwa unawahusu, na hivyo walitaka kumkamata palepale, ila tu waliogopa watu.
20 Ils ne le perdirent donc pas de vue, et lui envoyèrent des gens apostés qui feignaient d’être justes, pour le surprendre dans ses paroles, afin de le livrer à l’autorité et au pouvoir du gouverneur.
Basi, wakawa wanatafuta wakati wa kufaa. Wakawahonga watu fulani wajisingizie kuwa wema, wakawatuma wamnase Yesu kwa maswali, na hivyo waweze kumtia nguvuni na kumpeleka kwa wakuu wa serikali.
21 Ces gens l’interrogèrent en ces termes: « Maître, nous savons que tu parles et enseignes avec droiture, et sans faire acception de personne, mais que tu enseignes la voie de Dieu dans la vérité.
Hao wapelelezi wakamwambia, “Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli; tunajua kwamba wewe huna ubaguzi; wewe wafundisha ukweli juu ya njia ya Mungu.
22 Nous est-il permis, ou non, de payer le tribut à César? »
Basi, twambie kama ni halali, au la, kulipa kodi kwa Kaisari!”
23 Jésus, connaissant leur fourberie, leur dit: « Pourquoi me tentez-vous?
Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
24 Montrez-moi un denier. De qui porte-t-il l’effigie et le nom? » Ils lui répondirent: « De César. »
“Nionyesheni sarafu. Je, sura na chapa ni vya nani?”
25 Et il leur dit: « Rendez donc à César ce qui est à César, et à Dieu ce qui est à Dieu. »
Nao wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Yesu akawaambia, “Basi, mpeni Kaisari vilivyo vyake Kaisari, na Mungu vilivyo vyake Mungu.”
26 Ainsi ils ne purent le prendre en défaut sur aucune parole devant le peuple; et admirant sa réponse, ils gardèrent le silence.
Hawakufaulu kumnasa kwa neno lolote pale mbele ya watu na hivyo wakakaa kimya wakilistaajabia jibu lake.
27 Quelques-uns des Sadducéens, qui nient la résurrection, s’approchèrent alors et l’interrogèrent:
Kisha Masadukayo, ambao husema kwamba wafu hawafufuki, wakamjia Yesu, wakasema:
28 « Maître, lui dirent-ils, Moïse nous a donné cette loi: Si un homme, ayant une femme, meurt sans laisser d’enfants, que son frère prenne sa femme, et suscite des enfants à son frère.
“Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu ya mtu fulani akifa na kumwacha mjane wake bila watoto, ni lazima ndugu yake amchukue huyo mama mjane, amzalie watoto ndugu yake marehemu.
29 Or, il y avait sept frères; le premier prit une femme et mourut sans enfants.
Sasa, wakati mmoja kulikuwa na ndugu saba. Yule wa kwanza alioa na baadaye akafa bila kuacha mtoto.
30 Le second prit sa femme, et mourut aussi sans enfants.
Yule ndugu wa pili akamwoa yule mjane, naye pia, akafa;
31 Le troisième la prit ensuite, et de même tous les sept, et ils moururent sans laisser d’enfants.
na ndugu wa tatu vilevile. Mambo yakawa yaleyale kwa wote saba—wote walikufa bila kuacha watoto.
32 Après eux tous, la femme mourut aussi.
Mwishowe akafa pia yule mwanamke.
33 Duquel donc, au temps de la résurrection, sera-t-elle la femme, car elle l’a été de tous les sept? »
Je, siku wafu watakapofufuliwa, mwanamke huyo atakuwa mke wa nani? Alikuwa ameolewa na wote saba.”
34 Jésus leur dit: « Les enfants de ce siècle se marient et sont donnés en mariage; (aiōn g165)
Yesu akawaambia, “Watu wa nyakati hizi huoa na kuolewa; (aiōn g165)
35 mais ceux qui ont été trouvés dignes d’avoir part au siècle à venir et à la résurrection des morts, ne prennent pas de femme et n’ont pas de mari; (aiōn g165)
lakini wale ambao Mungu atawawezesha kushiriki ule wakati wa ufufuo, hawataoa wala kuolewa. (aiōn g165)
36 aussi bien ne peuvent-ils plus mourir, puisqu’ils sont en comme les anges, et qu’ils sont fils de Dieu, étant fils de la résurrection.
Ama hakika, hawawezi kufa tena, kwa sababu watakuwa kama malaika, na ni watoto wa Mungu kwa vile wamefufuliwa katika wafu.
37 Mais que les morts ressuscitent, c’est ce que Moïse lui-même a fait connaître dans le passage du Buisson, lorsqu’il nomme le Seigneur: Le Dieu d’Abraham, le Dieu d’Isaac et le Dieu de Jacob.
Lakini, kwamba kuna kufufuka kutoka wafu, hata Mose alithibitisha jambo hilo katika Maandiko Matakatifu. Katika sehemu ya Maandiko Matakatifu juu ya kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto, anamtaja Bwana kama Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.
38 Or il n’est pas Dieu des morts, mais des vivants; car tous sont vivants devant lui. »
Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa wale walio hai; maana wale aliowaita kwake, wanaishi naye.”
39 Quelques-uns des scribes, prenant la parole, lui dirent: « Maître, tu as bien parlé. »
Baadhi ya wale walimu wa Sheria wakasema, “Mwalimu, umejibu vema kabisa.”
40 Et ils n’osaient plus lui poser aucune question.
Walisema hivyo kwa sababu hawakuthubutu kumwuliza tena maswali mengine.
41 Jésus leur dit: « Comment dit-on que le Christ est fils de David?
Yesu akawauliza, “Yasemekanaje kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
42 David lui-même dit dans le livre des Psaumes: Le Seigneur a dit à mon Seigneur: Assieds-toi à ma droite,
Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia
43 jusqu’à ce que je fasse de vos ennemis l’escabeau de vos pieds. —
mpaka niwafanye adui zako kama kiti cha kuwekea miguu yako.
44 David l’appelle donc Seigneur; comment peut-il être son fils? »
Ikiwa Daudi anamwita yeye, Bwana, basi atakuwaje mwanawe?”
45 Tandis que tout le peuple l’écoutait, il dit à ses disciples:
Yesu aliwaambia wanafunzi wake mbele ya watu wote,
46 « Gardez-vous des scribes, qui se plaisent à se promener en longues robes; qui aiment à être salués dans les places publiques, à occuper les premiers sièges dans les synagogues et les premières places dans les festins:
“Jihadharini na walimu wa Sheria ambao hupenda kupitapita wamevalia kanzu. Hupenda kusalimiwa na watu kwa heshima masokoni, huketi mahali pa heshima katika masunagogi na kuchukua nafasi za heshima katika karamu.
47 ces gens qui dévorent les maisons des veuves, et font pour l’apparence de longues prières, subiront une condamnation plus sévère. »
Huwadhulumu wajane huku wakisingizia kuwa wema kwa kusali sala ndefu. Hao watapata hukumu kali zaidi!”

< Luc 20 >