< Lévitique 7 >
1 Voici la loi du sacrifice de réparation; c’est une chose très sainte.
“‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya hatia, ambayo ni takatifu sana:
2 C’est dans le lieu où l’on égorge l’holocauste que sera égorgée la victime de réparation. On en répandra le sang sur l’autel tout autour.
Sadaka ya hatia itachinjiwa mahali pale ambapo sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa, nayo damu yake itanyunyizwa pande zote za madhabahu.
3 On en offrira toute la graisse, la queue, la graisse qui enveloppe les entrailles,
Mafuta yake yote yatatolewa sadaka: mafuta ya mkia na mafuta yale yanayofunika sehemu za ndani,
4 les deux rognons avec la graisse qui les recouvre et qui tient à la région lombaire, et la taie du foie, qu’on détachera près des rognons.
figo zote mbili pamoja na mafuta yanayozizunguka yaliyo karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo yataondolewa pamoja na hizo figo.
5 Le prêtre les fera fumer sur l’autel en sacrifice par le feu à Yahweh. C’est un sacrifice de réparation.
Kuhani atayateketeza juu ya madhabahu kuwa sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto. Hii ni sadaka ya hatia.
6 Tout mâle parmi les prêtres en mangera la chair; il la mangera en lieu saint: c’est une chose très sainte.
Mwanaume yeyote katika jamaa ya kuhani aweza kuila, lakini lazima iliwe mahali patakatifu; ni takatifu sana.
7 Il en est du sacrifice de réparation comme du sacrifice pour le péché; la loi est la même pour les deux: la victime appartiendra au prêtre qui fera l’expiation.
“‘Sheria hii ya sadaka ya hatia ni sawasawa na ile ya sadaka ya dhambi: Nyama ya yule mnyama aliyetolewa sadaka ni ya yule kuhani anayesimamia ibada ya upatanisho.
8 Le prêtre qui offrira l’holocauste de quelqu’un aura pour lui la peau de l’holocauste qu’il a offert.
Kuhani anayetoa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya mtu yeyote anaweza kuichukua ngozi ya mnyama yule aliyetolewa iwe yake.
9 Toute oblation cuite au four, et celle qui est préparée dans la casserole ou à la poêle appartiendra au prêtre qui l’aura offerte.
Kila sadaka ya nafaka iliyookwa jikoni au kupikwa katika sufuria au katika kikaangio itakuwa ya kuhani anayeitoa.
10 Toute oblation pétrie à l’huile ou sèche sera pour tous les fils d’Aaron, qui en auront une part égale.
Nayo kila sadaka ya nafaka, iwe imechanganywa na mafuta au iko kavu, itakuwa ya wana wa Aroni, nayo itagawanywa sawa kati yao.
11 Voici la loi du sacrifice pacifique qu’on offrira à Yahweh.
“‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya amani ambayo mtu aweza kuileta kwa Bwana:
12 Si on l’offre par reconnaissance, on offrira, avec la victime de reconnaissance, des gâteaux sans levain pétris à l’huile, des galettes sans levain arrosées d’huile, de la farine frite en gâteaux pétris à l’huile.
“‘Ikiwa mtu atatoa sadaka ya amani kwa ajili ya kuonyesha shukrani, pamoja na sadaka hii ya shukrani, atatoa maandazi yasiyotiwa chachu yaliyochanganywa na mafuta, mikate myembamba isiyotiwa chachu iliyopakwa mafuta, maandazi ya unga laini uliokandwa vizuri na kuchanganywa na mafuta.
13 On ajoutera des gâteaux levés à l’offrande qu’on présentera avec la victime de reconnaissance de son sacrifice pacifique.
Pamoja na sadaka hii ya amani ya shukrani ataleta sadaka ya maandazi yaliyotengenezwa kwa chachu.
14 On présentera une pièce de chacune de ces offrandes prélevées pour Yahweh; elle sera pour le prêtre qui aura fait l’aspersion du sang de la victime pacifique.
Ataleta moja ya kila aina ya andazi kama sadaka, matoleo kwa Bwana; hii ni ya kuhani anayenyunyiza damu ya sadaka ya amani.
15 La chair de la victime de reconnaissance du sacrifice pacifique sera mangée le jour où on l’aura offerte; on n’en laissera rien jusqu’au matin.
Nyama ya sadaka ya amani kwa ajili ya shukrani lazima iliwe siku iyo hiyo inapotolewa; hutabakiza kitu chochote mpaka asubuhi.
16 Si la victime est offerte par suite d’un vœu ou comme offrande volontaire, la victime sera mangée le jour où on l’aura offerte, et ce qui en restera sera mangé le lendemain.
“‘Lakini kama sadaka yake ni kwa ajili ya nadhiri au ni sadaka ya hiari, sadaka hiyo italiwa siku hiyo inapotolewa, lakini chochote kinachobakia kinaweza kuliwa kesho yake.
17 Ce qui resterait encore de la chair de la victime le troisième jour sera consumé par le feu.
Nyama yoyote ya sadaka inayobaki mpaka siku ya tatu lazima iteketezwe kwa moto.
18 Si un homme mange de la chair de son sacrifice pacifique le troisième jour, ce sacrifice ne sera pas agréé; il n’en sera pas tenu compte à celui qui l’a offert; ce sera une abomination, et quiconque en aura mangé portera son iniquité.
Kama nyama yoyote ya sadaka ya amani italiwa siku ya tatu, Bwana hataikubali. Haitahesabiwa kwake huyo aliyeitoa, kwa kuwa ni najisi. Mtu atakayekula sehemu yake yoyote atahesabiwa hatia.
19 La chair qui a touché quelque chose d’impur ne se mangera pas; elle sera consumée par le feu. Quant à la chair du sacrifice pacifique, tout homme pur pourra en manger.
“‘Nyama ile inayogusa chochote ambacho ni najisi kwa kawaida ya ibada kamwe haitaliwa, ni lazima iteketezwe kwa moto. Kuhusu nyama nyingine, mtu yeyote aliye safi kwa kawaida ya ibada anaweza kuila.
20 Mais celui qui, se trouvant en état d’impureté, aura mangé de la chair de la victime pacifique appartenant à Yahweh, celui-là sera retranché de son peuple.
Lakini kama mtu yeyote najisi akila nyama yoyote ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Bwana, huyo mtu lazima akatiliwe mbali na watu wake.
21 Et celui qui touchera quelque chose d’impur, souillure d’homme ou animal impur, ou toute autre abomination impure, et qui mangera de la chair de la victime pacifique appartenant à Yahweh, celui-là sera retranché de son peuple. »
Kama mtu yeyote akigusa kitu kilicho najisi, iwe ni uchafu wa mwanadamu, au mnyama najisi, au kitu chochote kilicho najisi, kitu cha kuchukiza, kisha akala nyama yoyote ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Bwana, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.’”
22 Yahweh parla à Moïse, en disant:
Bwana akamwambia Mose,
23 « Parle aux enfants d’Israël et dis-leur: Vous ne mangerez pas de graisse de bœuf, de brebis, ni de chèvre.
“Waambie Waisraeli: ‘Msile mafuta yoyote ya ngʼombe, kondoo wala mbuzi.
24 La graisse d’un animal mort ou déchiré par une bête féroce pourra servir à un usage quelconque, mais vous n’en mangerez en aucune manière.
Mafuta ya mnyama aliyekutwa amekufa au ameraruliwa na mnyama pori yanaweza kutumika kwa kazi nyingine yoyote, lakini kamwe msiyale.
25 Car quiconque mangera de la graisse des animaux que l’on offre à Yahweh en sacrifices faits par le feu, sera retranché de son peuple.
Mtu yeyote alaye mafuta ya mnyama ambaye ametolewa sadaka kwa Bwana kwa moto ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
26 Vous ne mangerez pas de sang ni d’oiseau, ni de quadrupède, dans tous les lieux que vous habiterez.
Popote mtakapoishi, kamwe msinywe damu ya ndege yeyote wala ya mnyama.
27 Celui qui mangera d’un sang quelconque, celui-là sera retranché de son peuple. »
Ikiwa mtu yeyote atakunywa damu, mtu huyo lazima akatiliwe mbali na watu wake.’”
28 Yahweh parla à Moïse, en disant:
Bwana akamwambia Mose,
29 « Parle aux enfants d’Israël et dis-leur: Celui qui offrira à Yahweh sa victime pacifique apportera à Yahweh son offrande prélevée sur son sacrifice pacifique.
“Waambie Waisraeli: ‘Mtu yeyote aletaye sadaka ya amani kwa Bwana ataleta sehemu ya sadaka hiyo kama dhabihu yake kwa Bwana.
30 Il apportera dans ses mains ce qui doit être offert par le feu à Yahweh: il apportera la graisse avec la poitrine, la poitrine pour la balancer devant Yahweh.
Ataleta sadaka kwa mikono yake mwenyewe iliyotolewa kwa Bwana kwa moto; ataleta mafuta ya huyo mnyama pamoja na kidari, naye atainua hicho kidari mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
31 Le prêtre fera fumer la graisse sur l’autel, et la poitrine sera pour Aaron et pour ses fils.
Kuhani atayateketeza hayo mafuta juu ya madhabahu, lakini kidari kitakuwa cha Aroni na wanawe.
32 Vous donnerez aussi au prêtre la cuisse droite comme offrande prélevée de vos victimes pacifiques.
Paja la kulia la sadaka zako za amani utampa kuhani kama matoleo.
33 Celui des fils d’Aaron qui offrira le sang et la graisse des victimes pacifiques aura la cuisse droite pour sa part.
Mwana wa Aroni atoaye damu na mafuta ya sadaka ya amani ndiye atakayepewa paja hilo la kulia kuwa fungu lake.
34 Car j’ai pris sur les sacrifices pacifiques des enfants d’Israël la poitrine à balancer et l’épaule prélevée, et je les donne au prêtre Aaron et à ses fils comme une redevance perpétuelle imposée aux enfants d’Israël.
Kutoka kwenye sadaka za amani za Waisraeli, mimi Mungu nimepokea kidari kile kilichoinuliwa pamoja na lile paja lililotolewa, nami nimevitoa kwa kuhani Aroni na wanawe kuwa fungu lao la kawaida kutoka kwa Waisraeli.’”
35 C’est là le droit de l’onction d’Aaron et le droit de l’onction de ses fils sur les sacrifices faits par le feu à Yahweh, à partir du jour où on les présentera pour être prêtres au service de Yahweh.
Hii ndiyo sehemu ya sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, ambazo zilitengwa kwa ajili ya Aroni na wanawe siku ile walipowekwa wakfu ili kumtumikia Bwana katika kazi ya ukuhani.
36 C’est ce que Yahweh a ordonné aux enfants d’Israël de leur donner depuis le jour de leur onction; ce sera une redevance perpétuelle parmi leurs descendants. »
Siku ile walipotiwa mafuta, Bwana aliagiza kwamba Waisraeli wawape hili kama fungu lao la kawaida kwa vizazi vijavyo.
37 Telle est la loi de l’holocauste, de l’oblation, du sacrifice pour le péché, du sacrifice de réparation, de l’installation et du sacrifice pacifique.
Basi haya ndiyo masharti kuhusu sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka, sadaka ya dhambi, sadaka ya hatia, sadaka ya kuwekwa wakfu, na sadaka ya amani,
38 Yahweh la prescrivit à Moïse sur la montagne de Sinaï, le jour où il ordonna aux enfants d’Israël de présenter leurs offrandes à Yahweh dans le désert de Sinaï.
ambayo Bwana alimpa Mose juu ya Mlima Sinai siku ile alipowaagiza Waisraeli walete sadaka zao kwa Bwana, katika Jangwa la Sinai.