< Lévitique 3 >

1 Lorsqu’un homme offrira un sacrifice pacifique, s’il offre du gros bétail, mâle ou femelle, il l’offrira sans défaut devant Yahweh.
Kama mtu atoa dhabihu ambayo ni matoleo ya amani ya mnyama kutoka katika kundi, dume au jike, lazima atatoa mnyama asiyena kasoro mbele ya Bwana.
2 Il posera sa main sur la tête de la victime et il l’égorgera à l’entrée de la tente de réunion, et les prêtres, fils d’Aaron, répandront le sang sur les parois de l’autel tout autour.
Ataweka mikono yake juu ya sadaka yake na atamchinja mbele ya mlango wa hema ya kukutania. Kisha wana wa Haruni makuhani watanyunyizia damu yake katika pande za madhabahu.
3 De ce sacrifice pacifique, il offrira en sacrifice par le feu à Yahweh: la graisse qui enveloppe les entrailles et toute la graisse qui est attachée aux entrailles;
Mtu akitoa dhabihu ya amani itolewayo kwa moto kwa ajili ya Bwana. Mafuta yanayofunika au yanayoungana na hizo sehemu za ndani,
4 les deux rognons avec la graisse qui les recouvre et qui tient à la région lombaire; la taie du foie qu’il détachera près des rognons.
figo mbili na mafuta yaliyofunika kiunoni na yanayozunguka ini, pamoja na figo atayatoa pamoja.
5 Les fils d’Aaron feront fumer cela sur l’autel, par-dessus l’holocauste placé sur le bois qui est sur le feu. C’est un sacrifice fait par le feu, d’une agréable odeur à Yahweh.
Wana wa Haruni watayachoma hayo katika madhabahu pamoja na sadaka ya kutekezwa, juu ya kuni zilizo kwenye moto. Zitaleta harufu nzuri mbele ya Bwana; itakuwa sadaka ya itolewayo kwake kwa moto.
6 S’il offre du menu bétail, mâle ou femelle, en sacrifice pacifique à Yahweh, il l’offrira sans défaut.
Kama dhabihu ya amani ya mtu itolewayo kwa Bwana ni kutoka katika mifugo ni mbuzi au kondoo ni dume au jike, atatoa dhabihu isiyo na kasoro.
7 S’il offre en sacrifice un agneau, il le présentera devant Yahweh.
Kama atatoa mwanakondoo kwa ajili ya dhabihu yake, atamtoa mbele za Bwana.
8 Il posera sa main sur la tête de la victime et il l’égorgera devant la tente de réunion, et les fils d’Aaron en répandront le sang sur les parois de l’autel tout autour.
Ataweka mkono wake juu ya ya kichwa cha dhabihu yake na atamchinja mbele ya hema ya kukutania. Ndipo wana wa Haruni watanyunyizia damu pande za madhabahu.
9 De ce sacrifice pacifique, il offrira en sacrifice par le feu à Yahweh: sa graisse, la queue entière, coupée près de l’échine; la graisse qui enveloppe les entrailles et toute la graisse qui est attachée aux entrailles;
Mtu akitoa sadaka ya dhabihu ya amani kama sadaka ya kusogezwa kwa moto kwa Bwana. Mafuta, mafuta ya mkia yatakatwa hapo karibu na mfupa wa kiuno, na mafuta yanayofunika matumbo na mafuta yaliyo katika matumbo,
10 les deux rognons, avec la graisse qui les recouvre et qui tient à la région lombaire; la taie du foie qu’il détachera près des rognons.
na figo zote mbili na mafuta yanayofunika yaliyo karibu na kiuno kitambi kilicho karibu na ini na figo ataziondoa zote.
11 Le prêtre fera fumer cela sur l’autel: c’est l’aliment d’un sacrifice fait par le feu à Yahweh.
Na kuhani atayatekeza yote kwa moto katika madhabahu kama sadaka ya chakula isogezwayo kwa moto kwa Bwana.
12 Si son offrande est une chèvre, il la présentera devant Yahweh.
Kama matoleo ya mtu ni mbuzi, ndipo ataitoa mbele ya Bwana.
13 Il posera sa main sur la tête de la victime, et il l’égorgera devant la tente de réunion, et les fils d’Aaron en répandront le sang sur les parois de l’autel tout autour.
Ataweka mikono yake juu ya kichwa cha mbuzi na atamchinja mbele ya hema ya kukutania. Ndipo wana wa Haruni watanyunyizia damu pande zote za madhabahu.
14 De la victime, il offrira en sacrifice par le feu à Yahweh: la graisse qui enveloppe les entrailles et toute la graisse qui est attachée aux entrailles;
Mtu akitoa dhabihu kwa Bwana kwa njia ya moto. Ataondoa mafuta yanayozunguka matumbo, na mafuta yote yanayozunguka matumbo.
15 les deux rognons, avec la graisse qui les recouvre et qui tient à la région lombaire; la taie du foie qu’il détachera près des rognons.
Ataondoa pia figo mbili na mafuta yanayozunguka, ambayo yanazunguka kiuno na kitambi cha maini pamoja na figo.
16 Le prêtre fera fumer cela sur l’autel: c’est l’aliment d’un sacrifice fait par le feu d’une agréable odeur. Toute graisse appartient à Yahweh.
Kuhani atateketeza yote juu ya madhabahu kama matoleo ya chakula yatolewayo kwa moto, ni sadaka ya kuleta harufu nzuri sana. Mafuta yote ni ya Bwana.
17 C’est ici une loi perpétuelle pour vos descendants, en quelque lieu que vous habitiez: vous ne mangerez ni graisse, ni sang. »
Itakuwa ni amri ya kudumu kwa kizazi cha watu katika maeneo yote mtakapotengeneza makazi, kwamba hamtakula mafuta au damu.”'

< Lévitique 3 >