< Lévitique 11 >
1 Yahweh parla à Moïse et à Aaron, en leur disant:
Bwana akawaambia Mose na Aroni,
2 « Parlez aux enfants d’Israël, et dites: Voici les animaux que vous mangerez parmi toutes les bêtes qui sont sur la terre:
“Waambieni Waisraeli: ‘Kati ya wanyama wote waishio juu ya nchi, hawa ndio mtakaowala:
3 Tout animal qui a la corne divisée et le pied fourchu, et qui rumine, vous le mangerez.
Mwaweza kula mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika sehemu mbili na ambaye hucheua.
4 Mais vous ne mangerez pas de ceux qui ruminent seulement, ou qui ont seulement la corne divisée. Tel est le chameau, qui rumine, mais dont la corne n’est pas divisée: il sera impur pour vous.
“‘Kuna wanyama wengine ambao hucheua tu au wenye kwato zilizogawanyika tu, lakini hao kamwe msiwale. Ngamia ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; kwa kawaida ya ibada hiyo ni najisi kwenu.
5 Telle la gerboise, qui rumine, mais qui n’a pas la corné divisée: elle sera impure pour vous.
Pelele ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.
6 Tel le lièvre, qui rumine, mais qui n’a pas la corne divisée: il sera impur pour vous.
Sungura ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.
7 Tel le porc, qui a la corne divisée et le pied fourchu, mais qui ne rumine pas: il sera impur pour vous.
Naye nguruwe ingawa anazo kwato zilizogawanyika sehemu mbili, hacheui; huyo ni najisi kwenu.
8 Vous ne mangerez pas de leur chair, et vous ne toucherez pas à leurs corps morts: ils seront impurs pour vous.
Kamwe msile nyama yao wala kugusa mizoga yao; wao ni najisi kwenu.
9 Voici les animaux que vous mangerez parmi tous ceux qui sont dans les eaux: Tout ce qui a nageoires et écailles, dans les eaux, soit dans la mer, soit dans les rivières, vous le mangerez.
“‘Kuhusu viumbe wote wanaoishi ndani ya maji ya bahari na vijito, mtakula wale wote wenye mapezi na magamba.
10 Mais vous aurez en abomination tout ce qui n’a pas nageoires et écailles, dans les mers et dans les rivières, parmi tous les animaux qui se meuvent dans les eaux et parmi tous les êtres vivants qui s’y trouvent.
Lakini viumbe wote ndani ya bahari au vijito wasio na mapezi na magamba, wakiwa miongoni mwa makundi au viumbe wote ndani ya maji, hao ni machukizo kwenu.
11 Ils seront pour vous une abomination; vous ne mangerez pas de leur chair, et vous tiendrez pour abominables leurs cadavres.
Nao watakuwa machukizo kwenu. Msile nyama yao, nayo mizoga yao itakuwa machukizo.
12 Tout ce qui, dans les eaux, n’a pas de nageoires et d’écailles, vous l’aurez en abomination.
Chochote kinachoishi ndani ya maji ambacho hakina mapezi na magamba kitakuwa chukizo kwenu.
13 Voici, parmi les oiseaux, ceux que vous aurez en abomination; on ne les mangera pas, c’est chose abominable: l’aigle, l’orfraie et le vautour:
“‘Wafuatao ndio ndege watakaokuwa machukizo kwenu, hivyo msiwale kwa sababu ni chukizo: tai, furukombe, kipungu,
14 le milan et toute espèce de faucons;
mwewe mwekundu, aina zote za mwewe mweusi,
15 toute espèce de corbeaux;
aina zote za kunguru,
16 l’autruche, le chat-huant, la mouette et toute espèce d’éperviers;
mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga, shakwe, aina zote za kipanga,
17 le hibou, le cormoran et la chouette;
bundi, mnandi, bundi mkubwa,
18 le cygne, le pélican et le gypaète;
mumbi, mwari, nderi,
19 la cigogne, toute espèce de hérons; la huppe et la chauve-souris.
korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
20 Tout insecte ailé qui marche sur quatre pattes, vous l’aurez en abomination.
“‘Wadudu wote warukao ambao hutembea kwa miguu minne watakuwa chukizo kwenu.
21 Mais, parmi tous les insectes ailés qui marchent sur quatre pattes, vous mangerez ceux qui ont des jambes au-dessus de leurs pattes, pour sauter sur la terre.
Lakini wako viumbe wenye mabawa ambao hutembea kwa miguu minne mtakaowala: wale wenye vifundo katika miguu yao ya kurukaruka juu ya ardhi.
22 Voici ceux d’entre eux que vous mangerez: toute espèce de sauterelles, toute espèce de solam, toute espèce de hargol, toute espèce de hagab.
Miongoni mwa hawa, mtakula nzige wa aina zote, senene, parare au panzi.
23 Toute autre bête ailée ayant quatre pattes, vous l’aurez en abomination.
Lakini viumbe wengine wote wenye mabawa na wenye miguu minne ni machukizo kwenu.
24 Ceux-ci aussi vous rendront impurs: quiconque touchera leur corps mort sera impur jusqu’au soir,
“‘Mtajinajisi kwa wanyama hawa. Yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
25 et quiconque emportera quelque partie de leur corps mort lavera ses vêtements et sera impur jusqu’au soir.
Yeyote atakayebeba mizoga ya viumbe hawa ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
26 Tout animal qui a la corne divisée, mais qui n’a pas le pied fourchu et qui ne rumine pas, sera impur pour vous; quiconque le touchera se rendra impur.
“‘Kila mnyama mwenye ukwato ulioachana lakini haukugawanyika kabisa, au yule asiyecheua, huyo ni najisi kwenu; yeyote agusaye mzoga wowote wa hao atakuwa najisi.
27 Et parmi les animaux à quatre pieds, tout ce qui marche sur la plante des pieds vous sera impur: quiconque touchera leur corps mort sera impur jusqu’au soir;
Miongoni mwa wanyama wote watembeao kwa miguu minne, wale watembeao kwa vitanga vyao ni najisi kwenu; yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
28 et quiconque portera leur corps mort lavera ses vêtements et sera impur jusqu’au soir. Ces animaux seront impurs pour vous.
Yeyote atakayebeba mizoga yao ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni. Wanyama hawa ni najisi kwenu.
29 Voici, parmi les petites bêtes qui rampent sur la terre, celles qui seront impures pour vous: la belette, la souris et toute espèce de lézards;
“‘Kuhusu wanyama watambaao juu ya ardhi, hawa ni najisi kwenu: kicheche, panya, aina yoyote ya mijusi mikubwa,
30 la musaraigne, le caméléon, la salamandre, le lézard vert et la taupe.
guruguru, kenge, mijusi ya ukutani, goromoe na kinyonga.
31 Tels sont ceux qui seront impurs pour vous parmi les reptiles: quiconque les touchera morts sera impur jusqu’au soir.
Hao wote watambaao juu ya ardhi ni najisi kwenu. Yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
32 Tout objet sur lequel il en tombera de morts sera souillé: ustensile de bois, vêtement, peau, sac, tout objet dont on fait usage; on le mettra dans l’eau, et il restera souillé jusqu’au soir; après quoi, il sera pur.
Ikiwa mmoja wao atakufa na kuangukia juu ya kitu fulani, chombo hicho, hata kikiwa cha matumizi gani, kitakuwa najisi, kiwe kimetengenezwa kwa mti, nguo, ngozi au gunia. Kiweke ndani ya maji; kitakuwa najisi mpaka jioni, kisha kitakuwa safi tena.
33 S’il en tombe quelque chose dans le milieu de tout vase de terre, tout ce qui sera dans le milieu du vase sera souillé, et vous briserez le vase.
Ikiwa mmoja wa wanyama aliyekufa ataangukia ndani ya chungu, kila kilichomo katika chungu hicho kitakuwa najisi, nawe ni lazima uvunje chungu hicho.
34 Tout aliment servant à la nourriture et préparé avec de l’eau, sera souillé; toute boisson dont on fait usage, quel que soit le vase qui la contienne, sera souillée.
Chakula chochote ambacho chaweza kuliwa lakini kikawa kimeingia maji kutoka kwenye chungu hicho ni najisi, na kitu chochote cha majimaji ambacho chaweza kunyweka kutoka kwenye chungu hicho ni najisi.
35 Tout objet sur lequel tombera quelque chose de leur corps mort sera souillé; le four et le vase avec son couvercle seront détruits; ils seront souillés et vous les tiendrez pour souillés.
Chochote ambacho mzoga wa mmojawapo utaangukia kitakuwa najisi. Jiko au chungu cha kupikia ni lazima kivunjwe. Ni najisi, nawe ni lazima uvihesabu kuwa najisi.
36 Mais les sources et les citernes, où se forment les amas d’eau, resteront pures; toutefois celui qui touchera le corps mort sera impur.
Lakini chemchemi au kisima, mahali pa kuchota maji, patakuwa safi, lakini yeyote atakayegusa moja ya mizoga hii ni najisi.
37 S’il tombe quelque chose de leur corps mort sur une semence qui doit être semée, la semence restera pure;
Kama mzoga ukianguka juu ya mbegu zozote ambazo ni za kupanda, zinabaki safi.
38 mais si l’on a mis de l’eau sur la semence, et qu’il y tombe quelque chose de leur corps mort, vous la tiendrez pour souillée.
Lakini kama mbegu imetiwa maji na mzoga ukaanguka juu yake, hiyo mbegu ni najisi kwenu.
39 S’il meurt un des animaux qui vous servent de nourriture, celui qui touchera son cadavre sera impur jusqu’au soir.
“‘Kama mnyama ambaye mnaruhusiwa kumla akifa, yeyote atakayeugusa mzoga wake atakuwa najisi mpaka jioni.
40 Celui qui mangera de son corps mort lavera ses vêtements et sera impur jusqu’au soir; celui qui portera son corps mort, lavera ses vêtements et sera impur jusqu’au soir.
Yeyote atakayekula sehemu ya mzoga huo ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni. Yeyote atakayebeba mzoga huo ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
41 Vous aurez en abomination tout reptile qui rampe sur la terre: on n’en mangera point.
“‘Kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi ni chukizo; kisiliwe.
42 Vous ne mangerez d’aucun animal qui rampe sur la terre, soit de ceux qui se traînent sur le ventre, soit de ceux qui marchent sur quatre pieds ou sur un grand nombre de pieds; car vous les aurez en abomination.
Msile kiumbe chochote kitambaacho juu ya ardhi, kiwe kitambaacho kwa tumbo lake, au kitambaacho kwa miguu minne au kwa miguu mingi; ni chukizo.
43 Ne vous rendez pas abominables par tous ces reptiles qui rampent; ne vous rendez pas impurs par eux; vous seriez souillés par eux.
Msijitie unajisi kwa chochote katika viumbe hivi. Msijitie unajisi kwa viumbe hivyo au kutiwa unajisi navyo.
44 Car je suis Yahweh, votre Dieu; vous vous sanctifierez et vous serez saints, car je suis saint; et vous ne vous souillerez pas par tous ces reptiles, qui rampent sur la terre.
Mimi ndimi Bwana Mungu wenu; jitakaseni mwe watakatifu, kwa sababu mimi ni mtakatifu. Msijitie unajisi wenyewe kwa kiumbe chochote kile kiendacho juu ya ardhi.
45 Car je suis Yahweh, qui vous ai fait monter du pays d’Égypte, pour être votre Dieu. Vous serez saints, car je suis saint. »
Mimi ndimi Bwana niliyewapandisha mtoke Misri ili niwe Mungu wenu. Kwa hiyo kuweni watakatifu kwa sababu Mimi ni mtakatifu.
46 Telle est la loi touchant les quadrupèdes, les oiseaux, tous les êtres vivants qui se meuvent dans les eaux, et tous les êtres qui rampent sur la terre,
“‘Haya ndiyo masharti kuhusu wanyama, ndege, kila kiumbe hai kiendacho ndani ya maji, na kila kiumbe kiendacho juu ya ardhi.
47 afin que vous distinguiez entre ce qui est impur et ce qui est pur, entre l’animal qui se mange et celui qui ne se mange pas.
Ni lazima mpambanue kati ya kilicho najisi na kilicho safi, kati ya viumbe hai vinavyoweza kuliwa na vile visivyoweza kuliwa.’”