< Josué 8 >

1 Yahweh dit à Josué: « Ne crains pas et ne t’effraie point. Prends avec toi tous les hommes de guerre, lève-toi et monte contre Haï. Vois, j’ai livré entre tes mains le roi d’Haï et son peuple, sa ville et son territoire.
Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Usiogope, wala usivunjike moyo. Chukua jeshi lote la vita uende pamoja nalo kuishambulia Ai. Kwa kuwa nimeshamweka mikononi mwako mfalme wa Ai, pamoja na watu wake, mji wake na nchi yake.
2 Tu traiteras Haï et son roi comme tu as traité Jéricho et son roi; seulement vous pillerez pour vous son butin et son bétail. Dresse une embuscade derrière la ville. »
Utafanya Ai na mfalme wake kama ulivyofanya kwa mji wa Yeriko na mfalme wake, isipokuwa mnaweza kuchukua mateka wake na mifugo wake, kwa ajili yenu. Weka waviziaji upande wa nyuma ya mji.”
3 Josué se leva avec tous les gens de guerre, pour monter contre Haï. Josué choisit trente mille hommes vaillants, et les fit partir de nuit.
Basi Yoshua na jeshi lote wakainuka kushambulia Ai. Akachagua watu mashujaa elfu thelathini walio bora miongoni mwa wapiganaji wake, akawapeleka wakati wa usiku
4 Il leur donna cet ordre: « Soyez sur vos gardez: vous vous mettrez en embuscade derrière la ville, mais sans vous éloigner beaucoup de la ville, et tous, tenez-vous prêts.
akiwaagiza: “Sikilizeni kwa makini. Mtavizia nyuma ya mji. Msiende mbali sana na mji. Wote kuweni macho.
5 Moi, et tout le peuple qui est avec moi, nous nous approcherons de la ville; et quand ils sortiront au-devant de nous, comme la première fois, nous fuirons devant eux.
Mimi na watu walio pamoja nami, tutaukabili mji, kisha itakuwa hapo watu watakapotoka nje kupigana nasi, kama walivyofanya hapo kwanza, sisi tutawakimbia.
6 Ils sortiront pour nous poursuivre, jusqu’à ce que nous les ayons attirés loin de la ville, car ils diront: Ils fuient devant nous, comme la première fois. Et nous fuirons devant eux.
Watatufuatilia mpaka tutakapokuwa tumewavuta mbali na mji kwa kuwa watasema, ‘Wanatukimbia, kama walivyofanya hapo awali.’ Hivyo tutakapowakimbia,
7 Alors, sortant de l’embuscade, vous vous emparerez de la ville; Yahweh, votre Dieu, la livrera entre vos mains.
ninyi inawapasa mwinuke mtoke huko mafichoni na kuuteka mji. Bwana Mungu wenu atautia mkononi mwenu.
8 Quand vous aurez pris la ville, vous la brûlerez; vous agirez selon la parole de Yahweh. Voyez: je vous ai donné mes ordres. »
Mtakapokuwa mmeuteka mji, uteketezeni kwa moto. Fanyeni kama vile Bwana alivyoamuru. Angalieni, nimewaagiza.”
9 Josué les fit partir, et ils allèrent se poster en embuscade entre Béthel et Haï, à l’occident d’Haï. Quant à Josué, il passa cette nuit-là au milieu du peuple.
Ndipo Yoshua akawatuma watu, nao wakaenda mahali pa kujificha, wakawa wanavizia kati ya Betheli na Ai, kuelekea upande wa magharibi wa Ai, lakini Yoshua akalala miongoni mwa watu usiku huo.
10 Josué se leva de bon matin et, ayant passé le peuple en revue, il monta à la tête du peuple, lui et les anciens d’Israël, contre Haï.
Asubuhi na mapema siku iliyofuatia, Yoshua akawakutanisha watu wake, na yeye na viongozi wa Israeli wakawa mbele ya watu kwenda Ai.
11 Tous les hommes de guerre qui étaient avec lui montèrent et s’approchèrent; arrivés en face d’Haï, ils campèrent au nord de la ville, ayant la vallée entre eux et Haï.
Watu wote wa vita waliokuwa pamoja naye walipanda, wakakaribia na kufika mbele ya mji. Wakapiga kambi kaskazini mwa Ai, pakiwa na bonde kati yao na huo mji.
12 Josué prit environ cinq mille hommes, et les mit en embuscade entre Béthel et Haï, à l’occident de la ville.
Yoshua alikuwa amewachukua watu wapatao elfu tano, akawaweka katika uavizi kati ya Betheli na Ai, upande wa magharibi wa mji.
13 Lorsque le peuple eut ainsi disposé tout le camp, qui était au nord de la ville, et son embuscade à l’occident de la ville, Josué s’avança durant cette nuit au milieu de la vallée.
Wakawaweka askari katika maeneo yao: wale wote waliokuwa kambini wakawa kaskazini ya mji na wale waliokuwa wakivizia wakawa upande wa magharibi. Usiku huo Yoshua akaenda katika lile bonde.
14 Dès que le roi de Haï vit cela, les hommes de la ville se levèrent en hâte de bon matin, et sortirent à la rencontre d’Israël pour le combattre; le roi s’avança avec tout son peuple vers le lieu convenu, en face de la plaine, ne sachant pas qu’il y avait derrière la ville une embuscade dressée contre lui.
Mfalme wa Ai alipoona jambo hili, yeye pamoja na watu wote wa mji wakatoka kwa haraka asubuhi na mapema, ili kukutana na Israeli katika vita mahali fulani panapotazamana na Araba. Lakini hakujua kwamba kulikuwa kumewekwa waviziaji dhidi yake nyuma ya mji.
15 Josué et tout Israël se laissèrent battre devant eux, et ils s’enfuirent par le chemin du désert.
Yoshua na Israeli wote wakaruhusu kurudishwa nyuma mbele yao, na kuelekea jangwani.
16 Alors tout le peuple qui était dans la ville se rassembla pour les poursuivre; ils poursuivirent Josué et se laissèrent attirer loin de la ville.
Watu wote wa Ai wakaitwa ili kuwafuatia, nao wakavutwa kumfuatia Yoshua mbali na mji.
17 Il ne resta pas un homme dans Haï et dans Béthel qui ne sortit pour poursuivre Israël; laissant la ville ouverte, ils poursuivirent Israël.
Hakuna hata mwanaume mmoja aliyebakia Ai wala Betheli ambaye hakufuatia Israeli. Wakauacha mji wazi na kuwafuatia Israeli.
18 Yahweh dit à Josué: « Etends vers Haï le javelot que tu as à la main, car je vais la livrer en ton pouvoir. » Et Josué étendit vers la ville le javelot qu’il avait à la main.
Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Inua huo mkuki ulio mkononi mwako kuuelekeza Ai, kwa kuwa nitautia huo mji mkononi mwako.” Hivyo Yoshua akauelekeza mkuki wake Ai.
19 Dès qu’il eut étendu sa main, les hommes de l’embuscade se levèrent en hâte du lieu où ils étaient et, prenant leur course, ils entrèrent dans la ville et l’occupèrent; et ils se hâtèrent de mettre le feu à la ville.
Mara tu alipofanya hivi, wale watu waliokuwa mavizioni wakaondoka upesi kutoka mahali pao na kukimbilia mbele. Wakaingia ndani ya mji, wakauteka na kuutia moto kwa haraka.
20 Les hommes d’Haï, regardant derrière eux, aperçurent la fumée de la ville qui montait vers le ciel, et ils ne purent plus se sauver d’aucun côté, le peuple qui fuyait vers le désert se retournant contre ceux qui le poursuivaient.
Watu wa Ai wakaangalia nyuma, wakauona moshi wa huo mji ukielekea angani lakini hawakuwa na nafasi ya kutoroka kwa upande wowote, kwa kuwa wale Waisraeli waliokuwa wanawakimbia kuelekea jangwani walikuwa wamegeuka nyuma kuwakabili wakimbizaji wao.
21 Et Josué et tout Israël, voyant la ville prise par les hommes de l’embuscade, et la fumée de la ville qui montait, se retournèrent et battirent les hommes d’Haï.
Basi Yoshua na Israeli wote walipoona kwamba waviziaji wameshauteka mji na moshi ulikuwa unapaa juu kutoka kwenye mji, wakawageukia watu wa Ai na kuwashambulia.
22 Les autres sortirent de la ville au-devant d’eux, et les hommes d’Haï se trouvèrent enveloppés par les Israélites, par les uns d’un côté, par les autres de l’autre côté. Et les Israélites les battirent, sans leur laisser ni un survivant ni un fugitif;
Wale waviziaji nao pia wakatoka nje ya mji dhidi yao, hivi kwamba wakashikiwa katikati, Waisraeli wakiwa pande zote mbili. Israeli wakawaua, bila kuwaachia yeyote aliyenusurika wala aliyetoroka.
23 ils prirent vivant le roi d’Haï et l’amenèrent à Josué.
Lakini wakamchukua mfalme wa Ai akiwa hai na kumleta kwa Yoshua.
24 Lorsqu’Israël eut achevé de tuer tous les habitants d’Haï dans la campagne, dans le désert, où ils l’avaient poursuivi, et que tous furent jusqu’au dernier passés au fil de l’épée, tout Israël revint dans la ville et la passa au fil de l’épée.
Israeli ilipomaliza kuwaua wanaume wote wa Ai katika mashamba na jangwani walipokuwa wamewafukuzia, na baada ya kila mmoja wao kuuawa kwa upanga, Waisraeli wote wakarudi Ai na kuwaua wale waliokuwa wamebakia mjini.
25 Le nombre total de ceux qui périrent en ce jour fut de douze mille, tant hommes que femmes, tous gens d’Haï.
Watu kumi na mbili elfu, waume kwa wake, waliangamia siku ile, yaani watu wote wa Ai.
26 Josué ne retira pas sa main qu’il tenait étendue avec le javelot, jusqu’à ce qu’il eût traité comme anathème tous les habitants d’Haï.
Kwa maana Yoshua hakuurudisha ule mkono wake uliokuwa umeuinua mkuki hadi alipomaliza kuwaangamiza wote walioishi Ai.
27 Les Israélites prirent seulement pour eux le bétail et le butin de cette ville, selon l’ordre de Yahweh qu’il avait prescrit à Josué.
Lakini Israeli wakajichukulia mifugo na nyara za mji huu, kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Yoshua.
28 Josué brûla Haï, et en fit pour toujours un monceau de ruines, qui subsiste encore aujourd’hui.
Kwa hiyo Yoshua akauchoma moto mji wa Ai na kuufanya kuwa lundo la magofu la kudumu, mahali pa ukiwa hadi leo.
29 Il fit pendre à un arbre le roi d’Haï et l’y laissa jusqu’au soir. Au coucher du soleil, Josué donna l’ordre de descendre son cadavre de l’arbre; on le jeta à l’entrée de la porte de la ville, et on éleva sur lui un grand monceau de pierres, qui subsiste jusqu’à ce jour.
Akamwangika mfalme wa Ai kwenye mti na kumwacha hapo mpaka jioni. Wakati wa jua kutua, Yoshua akawaamuru wautoe mwili wake kwenye mti na kuutupa kwenye ingilio la lango la mji. Kisha wakalundika mawe makubwa mengi juu yake, ambayo yamesalia mpaka leo.
30 Alors Josué bâtit un autel à Yahweh, Dieu d’Israël, sur le mont Hébal,
Kisha Yoshua akajenga madhabahu ya Bwana, Mungu wa Israeli, katika Mlima wa Ebali,
31 selon l’ordre que Moïse, serviteur de Yahweh, avait donné aux enfants d’Israël, comme il est écrit dans le livre de la loi de Moïse, un autel de pierres brutes, sur lesquelles on n’avait pas brandi le fer. Ils y offrirent des holocaustes à Yahweh, et firent des sacrifices pacifiques.
kama Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa amewaamuru Waisraeli. Akaijenga sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose: madhabahu ya mawe yasiyochongwa, ambayo juu yake hakuna chombo cha chuma kilichotumika. Hapo juu yake wakamtolea Bwana sadaka za kuteketezwa na kutoa sadaka za amani.
32 Là Josué écrivit sur les pierres une copie de la loi que Moïse avait écrite en présence des enfants d’Israël.
Pale, mbele ya Waisraeli Yoshua akanakili juu ya hayo mawe sheria ya Mose, aliyokuwa ameiandika.
33 Tout Israël, ses anciens, ses officiers et ses juges, se tenaient des deux côtés de l’arche, devant les prêtres lévitiques, qui portaient l’arche de l’alliance de Yahweh, les étrangers aussi bien que les enfants d’Israël, une moitié du côté du mont Garizim, une moitié du côté du mont Hébal, selon l’ordre que Moïse, serviteur de Yahweh, avait donné auparavant de bénir le peuple d’Israël.
Israeli yote, wageni na wazawa sawasawa, wakiwa na wazee wao, maafisa na waamuzi, walikuwa wamesimama pande zote mbili za Sanduku la Agano la Bwana, wakiwaelekea wale waliokuwa wamelichukua, yaani makuhani, ambao ni Walawi. Nusu ya watu ilisimama mbele ya Mlima Gerizimu na nusu hiyo ingine ikasimama mbele ya Mlima Ebali, kama vile Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa ameamuru hapo mwanzo alipotoa maagizo ya kuwabariki watu wa Israeli.
34 Puis Josué lut toutes les paroles de la loi, la bénédiction et la malédiction, suivant tout ce qui est écrit dans le livre de la loi.
Hatimaye, Yoshua akasoma maneno yote ya sheria, yaani baraka na laana, kama vile ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria.
35 Pas un mot de tout ce que Moïse avait prescrit que n’ait lu Josué en présence de toute l’assemblée d’Israël, des femmes et des enfants, et des étrangers qui vivaient au milieu d’eux.
Hakuna neno lolote katika yale yote ambayo Mose alikuwa ameamuru ambalo Yoshua hakulisomea kusanyiko lote la Israeli, ikiwa ni pamoja na wanawake na watoto, na wageni walioishi miongoni mwao.

< Josué 8 >