< Josué 16 >

1 La part échue par le sort aux fils de Joseph commençait, du côté de l’orient, depuis le Jourdain de Jéricho, jusqu’aux eaux de Jéricho; c’était ensuite le désert qui monte de Jéricho à Béthel par la montagne.
Mgawanyo wa Yosefu ulianzia Yordani ya Yeriko, mashariki mwa miji ya Yeriko na kutoka hapo ulipanda kupitia jangwani na kuingia katika nchi ya vilima ya Betheli.
2 La frontière aboutissait de Béthel à Luz, et passait vers la frontière des Archéens à Ataroth.
Ukaendelea kutoka Betheli (ndiyo Luzu), ukavuka kuingia eneo la Waariki huko Atarothi,
3 De là, elle descendait à l’occident, vers la frontière des Jephlétiens jusqu’à la frontière de Béthoron le Bas et jusqu’à Gazer, et elle aboutissait à la mer.
ukateremkia kuelekea magharibi hadi eneo la Wayafleti ukienea hadi eneo la Beth-Horoni ya Chini hadi Gezeri, ukiishia baharini.
4 Tel est l’héritage que reçurent les fils de Joseph, Manassé et Ephraïm.
Kwa hiyo Manase na Efraimu, wazao wa Yosefu, walipokea urithi wao.
5 Voici la frontière des fils d’Ephraïm, selon leurs familles. La limite de leur héritage était, à l’orient, Ataroth-Addar jusqu’à Béthoron le Haut.
Hili ndilo lilikuwa eneo la Efraimu, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao ulianzia Ataroth-Adari upande wa mashariki hadi Beth-Horoni ya Juu,
6 La frontière aboutissait, du côté de l’occident, vers Machméthath, au nord; et la frontière tournait à l’orient, vers Thanath-Sélo et passait devant elle, vers l’orient de Janoé.
na kuendelea mpaka baharini. Kutoka Mikmeta upande wa kaskazini ulipinda kuelekea mashariki hadi Taanath-Shilo, ukiupita hadi Yanoa upande wa mashariki.
7 De Janoé, elle descendait à Ataroth et à Naaratha, touchait à Jéricho et aboutissait au Jourdain.
Kisha uliteremka kutoka Yanoa hadi Atarothi na Naara, ukagusa Yeriko na kutokea katika Mto Yordani.
8 De Taphuah, elle allait, du côté de l’occident, au torrent de Cana, pour aboutir à la mer. Tel fut l’héritage des fils d’Ephraïm selon leurs familles.
Kutoka Tapua mpaka ulikwenda magharibi hadi Bonde la Kana na kuishia baharini. Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Waefraimu, ukoo kwa ukoo.
9 Les fils d’Ephraïm eurent aussi des villes séparées au milieu de l’héritage des fils de Manassé, toutes avec leurs villages.
Pia ulijumuisha miji yote na vijiji vyake ambavyo vilitengwa kwa ajili ya Waefraimu ndani ya urithi wa kabila la Manase.
10 Ils ne chassèrent pas les Chananéens qui habitaient à Gazer, et les Chananéens ont habité jusqu’à ce jour au milieu d’Ephraïm, mais assujettis à la corvée.
Hawakuwatoa Wakanaani waishio Gezeri; mpaka leo Wakanaani wanaishi miongoni mwa watu wa Efraimu lakini wanatakiwa kufanya kazi ngumu za kulazimishwa.

< Josué 16 >