< Josué 15 >

1 La part échue par le sort à la tribu des enfants de Juda, selon leurs familles, s’étendait vers la frontière d’Edom, jusqu’au désert de Sin vers le midi, à l’extrémité méridionale de Canaan.
Ugawanaji wa nchi kwa kabila la watu wa Yuda, walipewa kwa kufuatana na koo zao, kutoka upande wa kusini hadi mpaka wa Edomu, pamoja na nyika ya Sini iliyokuwa mbali sana kuelekea kusini.
2 Leur frontière du midi partait de l’extrémité de la mer Salée, de la langue tournée vers le sud;
Mpaka wao wa upande wa kusini ulianzia mwisho wa Bahari ya Chumvi, kutoka ghuba iliyokabili upande wa kusini.
3 elle se prolongeait au midi de la montée d’Akrabbim, passait à Sin et montait au midi de Cadès-Barné; de là, elle passait à Esron, montait vers Addar et tournait à Carcaa;
Mpaka wao mwingine ulielekea upande wa kusini wa mlima wa Akrabimu na kupita kuelekea Sini, na kupanda upande wa Kadeshi Barnea, karibu na Hezroni, hadi Addari mahali ambapo ulipinda kuelekea Karika.
4 elle passait ensuite à Asmon et continuait jusqu’au torrent d’Égypte; et la frontière aboutissait à la mer. « Ce sera votre frontière au midi. »
Ulipita katika Azimoni, kuelekea kijito cha Misri, na mwisho ulikuwa katika bahari. Huu ulikuwa ni mpaka wa kusini.
5 La frontière orientale fut la mer Salée jusqu’à l’embouchure du Jourdain. La frontière septentrionale partait de la langue de la mer Salée qui est à l’embouchure du Jourdain.
Mpaka wa mashariki ulikuwa ni Bahari ya Chumvi, katika mdomo wa Yordani. Mpaka wa upande wa kasikazini ulianzia katika ghuba ya bahari katika mdomo wa Yordani.
6 La frontière montait vers Beth-Agla, passait au nord de Beth-Araba, et la frontière montait jusqu’à la pierre de Boën, fils de Ruben;
Ulielekea mpaka Bethi Hogla na ulipita kaskazini mwa Bethi Araba. Kisha ulipanda hata JIwe la Bohani mwana wa Rubeni.
7 et la frontière montait à Débéra à partir de la vallée d’Achor, et tournait vers le nord du côté de Galgala, qui est vis-à-vis de la montagne d’Adommim, au sud du torrent. Et la frontière passait près des eaux d’En-Sémès et aboutissait à En-Rogel.
Basi mpaka ule ulienda hadi Debiri kutoka katika bonde la Akori, kuelekea upande wa kasikazini, kuendelea hadi Giligali, ambayo iko mkabala na mlima Adumimu, iliyo upande wa kusini wa bonde. Kisha mpaka uliendelea hata katika chemichemi za Eni Shemeshi na kufika Eni Rogeli.
8 Et la frontière montait par la vallée de Ben-Ennom, jusqu’au versant méridional de la montagne des Jébuséens, qui est Jérusalem; et la frontière s’élevait ensuite jusqu’au sommet de la montagne qui est vis-à-vis de la vallée d’Ennom à l’occident, et à l’extrémité de la plaine des Rephaïm au nord.
kisha mpaka ulishuka hadi bonde la Beni Hinomu kuelekea upande wa kusini wa mji wa Wayebusi ( ambao ni Yerusalemu). Kisha ulipanda hata katika mlima ulio juu ya bonde la Hinomu, katika upande wa magharibi, ulio mwishoni mwa bonde la Refaimu katika upande wa kasikazini.
9 Du sommet de la montagne, la frontière s’étendait jusqu’à la source des eaux de Nephtoa, aboutissait vers les villes de la montagne d’Ephron; et la frontière s’étendait vers Baala, qui est Cariath-Jéarim.
Kisha mpaka ulitanuka kutoka katika kilele cha milima hata chemichemi ya Nefutoa, na ulipanda kutoka hapo kuelekea miji ya Mlima Efroni. Kisha mpaka ulipiga kona kuelekea Baala ( ambao ndio Kiriathi Yearimu).
10 De Baala, la frontière tournait à l’occident vers le mont Séïr, passait par le versant septentrional du mont Jarim, qui est Cheslon, descendait à Bethsamès et passait par Thamma.
Baadaye mpaka ulizunguka kuelekea magharibi mwa Baala kukabili Mlima Seiri, na kupita kufuata upande wa Mlima wa Yearimu katika upande wa kasikazini (ambao ndio Kesaloni), ulienda chini hadi Bethi Shemeshi na kuvuka hata ng'ambo ya Timna.
11 La frontière aboutissait au versant septentrional d’Accaron; et la frontière s’étendait vers Sécrona, passait par le mont Baala, et aboutissait à Jebnéel; et la frontière aboutissait à la mer.
Mpaka uliendelea karibu na mlima wa kasikazini mwa mlima wa Ekroni, na kisha ukakata kona kuzunguka Shikeroni na kupita kuelekea sambasamba na Mlima Baala, kutoka hapo uliendelea hadi Yabneeli. Mpaka ule ulikomea katika bahari.
12 La limite occidentale était la Grande mer et son territoire. Telles furent de tous côtés les frontières des fils de Juda, selon leurs familles.
Mpaka wa magharibi ulikuwa Bahari Kuu na katika ukanda wa pwani yake. Huu ndio mpaka uliozunguka kabila la Yuda, ukoo kwa ukoo.
13 On avait donné à Caleb, fils de Jéphoné, une part au milieu des fils de Juda, comme Yahweh l’avait ordonné à Josué, savoir la ville d’Arbé, père d’Enac: c’est Hébron,
Katika kulitunza agizo la Yahweh kwa Yoshua, Yoshua alimpa Kalebu mwana wa Yefune mgao wa nchi ya. miongoni mwa kabila la Yuda, alimgawia nchi Kiriathi Arba, ambayo ndio Hebroni (Arba alikuwa ni baba wa Anaki).
14 Caleb en chassa les trois fils d’Enac, Sésaï, Ahiman et Tholmaï, descendants d’Enac.
Kalebu aliwafukuzia mbali wana watatu wa Anaki: Sheshai, Ahimani na Talmai, wazawa wa Anaki.
15 De là il monta contre les habitants de Dabir, qui s’appelait autrefois Cariath-Sépher.
Alipanda kutoka pale kinyume cha wenyeji wa Debiri (Debiri hapo mwanzo iliitwa Kiriathi Seferi).
16 Caleb dit: « A celui qui battra Cariath-Sépher et qui la prendra, je donnerai pour femme ma fille Axa. »
Kalebu akasema, “Mtu atakayeishambulia Kiriathi Seferi na kuiteka, nitampa binti yangau, Akisa, awe mke wake.
17 Othoniel, fils de Cénez, frère de Caleb, s’en empara, et Caleb lui donna sa fille Axa pour femme.
Wakati huo Othinieli mwana wa Kenazi, kaka yake na Kalebu, aliuteka mji, na Kalebu alimpatia Akisa, binti yake awe mke wake.
18 Lorsqu’elle alla chez Othoniel, elle l’excita à demander à son père un champ. Elle descendit de dessus son âne, et Caleb lui dit: « Qu’as-tu? »
Mara baada ya hayo, Akisa alienda kwa Othinieli na alimsihi amwombe baba yake shamba. Na mara aliposhuka kutoka katika punda wake, Kalebu alimwambia Akisa, “Unataka nini?”
19 Elle répondit: « Fais-moi un présent, car tu m’as établie dans le pays sec; donne-moi aussi des sources d’eau. » Et il lui donna les sources supérieures et les sources inférieures.
Akisa akamjibu, “Nifanyie neema. Kwa kuwa umeshanipa nchi ya Negevu, nipe pia baadhi ya chemichemi za maji.” Na Kalebu alimpa chemichemi ya juu na chemichemi ya chini.
20 Tel fut l’héritage de la tribu des fils de Juda, selon leurs familles.
Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Yuda, waliopewa kufuatana na koo zao.
21 Les villes situées à l’extrémité de la tribu des enfants de Juda, vers la frontière d’Edom, dans le Négeb, étaient: Cabséel, Eder, Jagur,
Miji iliyo mali ya kabila la Yuda katika upande wa kusini, kuelekea mpaka wa Edomu, ilikuwa ni Kabzeeli, Eda, Yaguri,
22 Cina, Dimona, Adada,
Kina, Dimona, Adada,
23 Cadès, Asor et Jethnam;
Kadeshi, Hazor, Ithinani,
24 Ziph, Télem, Baloth,
Zifu, Telemu, Bealothi.
25 Asor-la-Neuve et Carioth-Hesron, qui est Asor;
Hazori Hadata, Keriothi Hezroni (mji huu ulijulikana kama Hazori),
26 Amam, Sama, Molada,
Amamu, shema, Molada,
27 Asergadda, Hassemon, Bethphélet,
Hazari Gada, Heshimoni, Bethi Peleti,
28 Hasersual, Bersabée et Baziothia;
Hazari Shuali, Beerisheba, Biziothia.
29 Baala, Jim, Esem,
Baala, Limu, Ezemu,
30 Eltholad, Césil, Harma,
Eltoladi, Kesili, Horma,
31 Siceleg, Médémena, Sensenna,
Ziklagi, Madimana, Sansana,
32 Lebaoth, Sélim, Aen et Rémon: en tout vingt neuf villes et leurs villages.
Lebaothi, Shilihimu, Aini, na Rimoni. Miji hii ilikuwa ishirini na tisa kwa ujumla, kujumlisha na vijiji vyake.
33 Dans la Séphéla: Estaol, Saréa, Asena,
Katika nchi iliyo chini ya mlima upande wa magharibi, kulikuwa na miji ya Eshtaoli, Zora, Ashina,
34 Zanoé, Aen-Gannim, Taphua, Enaïm,
Zanaoa, Eni Ganimu, Tapua, Enamu,
35 Jérimoth, Odollam, Socho, Azéca,
Yarmuthi, Adulamu, Soko, Azeka,
36 Saraïm, Adithaïm, Gédéra et Gédérothaïm: quatorze villes et leurs villages.
Shaaraimu, Adithaimu, na Gedera ( ambayo ndio Gederothaimu). Hesabu ya miji hii ilikuwa ni kumi na nne, pamoja na vijiji vyao.
37 Sanan, Hadassa, Magdal-Gad,
Zena, Hadasha, Migidagadi,
38 Déléan, Masépha, Jecthel,
Dileani, Mizipa, Yokitheeli,
39 Lachis, Bascath, Eglon,
Lakishi, Bozikathi, Egloni.
40 Chebbon, Léhéman, Cethlis,
Kaboni, Lahmamu, Kitilishi,
41 Gideroth, Beth-Dagon, Naama et Macéda: seize ville et leurs villages.
Gederothi, Bethi Dagoni, Naama, Makeda. Hesabu ya miji hii ilikuwa kumi na sita, kujumlisha na vijiji vyao.
42 Labana, Ether, Asan,
Libna, Etheri, Ashani,
43 Jephtha, Esna, Nésib,
Ifuta, Ashina, Nezibu,
44 Céïla, Achzib et Marésa: neuf villes et leurs villages.
Keila, Akizibu, na Maresha. Hii ilikuwa ni miji tisa, kujumlisha na vijiji vyao.
45 Accaron, avec les villes de sa dépendance et ses villages.
Ekroni, pamoja na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka;
46 A partir d’Accaron, du côté de l’occident, toutes les villes près d’Azoth et leurs villages;
kutoka Ekroni kuelekea Bahari Kuu, makazi yote ambayo yalikuwa karibu na Ashidodi, pamoja na vijiji vyake.
47 Azoth, les villes de sa dépendance et ses villages; Gaza, les villes de sa dépendance et ses villages, jusqu’au torrent d’Égypte et à la Grande mer, qui est la limite.
Ashidodi, na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka; Gaza na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka; hata kufika kijito cha Misri, na kuelekea Bahari Kuu pamoja na ukanda wake wa pwani.
48 Dans la montagne: Samir, Jéther, Socoth,
Katika nchi ya milima, kuna miji ya Shamiri, Yatiri, Soko,
49 Danna, Cariath-Senna, qui est Dabir,
Dana, Kiriathi Sana (ambayo ndio Debiri),
50 Anab, Istémo, Anim,
Anabu, Eshitemo, Animu,
51 Gosen, Olon et Gilo: onze villes et leurs villages.
Gosheni, Holoni, na Gilo. Hii ilikuwa ni miji kumi na moja, kujumuisha na vijiji vyake.
52 Arab, Duma, Esaan,
Arabu, Duma, Ehani,
53 Janum, Beth-Thaphua, Aphéca,
Yanimu, Bethi Tapua, Afeka,
54 Athmatha, Cariath-Arbé, qui est Hébron, et Sior: neuf villes et leurs villages.
Humta, Kiriathi Arba (ambayo ndio Hebroni), na Ziori. Hii ilikuwa miji tisa, pamoja na vijiji vyake.
55 Maon, Carmel, Ziph, Jota,
Maoni, Karmeli, Zifu, Yuta,
56 Jezraël, Jucadam, Zanoé,
Yezreeli, Yokdeamu, Zanoa,
57 Accaïn, Gabaa, Thamma: dix villes et leurs villages.
Kaini, Gibea, na Timna. Hii ilikuwa ni miji kumi, kujumuisha na vijiji vyake.
58 Halhul, Bessur, Gédor,
Halhuli, Bethi Zuri, Gedori,
59 Mareth, Beth-Anoth et Eltécon: six villes, et leurs villages.
Maarathi, Bethi Anothi, na Elitekoni. Hii ilikuwa miji sita, pamoja na vijiji vyake.
60 Cariath-Baal, qui est Cariath-Jéarim, et Arebba: deux villes et leurs villages.
Kiriathi Baali (ambayo ndio Kiriathi Yearimu), na Raba. Hii ilikuwa ni miji miwili, pamoja na vijiji vyake.
61 Dans le désert: Beth-Araba, Meddin, Sachacha,
Katika nyika, kulikuwa na miji ya Bethi Araba, Midini, Sekaka,
62 Nebsan, Ir-Hammélach et En-Gaddi: six villes et leurs villages.
Nibushani, mji wa chumvi, na Eni Gedi. Hii ilikuwa miji, pamoja na vijiji vyao.
63 Les fils de Juda ne purent pas chasser les Jébuséens qui habitent à Jérusalem, et les Jébuséens ont habité à Jérusalem avec les fils de Juda jusqu’à ce jour.
Lakini kwa Wayebusi, wenyeji wa Yerusalemu, kabila la Yuda halikuweza kuwafukuza, na hivyo, Wayebusi wanaishi pamoja na kabila la Yuda hadi leo hii.

< Josué 15 >