< Jean 20 >

1 Le premier jour de la semaine, Marie-Madeleine se rendit au sépulcre, dès le matin, avant que les ténèbres fussent dissipées, et elle aperçoit la pierre enlevée du sépulcre.
Mapema siku ya kwanza ya juma, kungali bado giza, Mariamu Magdalena alikuja kaburini; akaliona lile jiwe limeondolewa kaburini.
2 Elle courut donc, et vint trouver Simon-Pierre et l’autre disciple que Jésus aimait, et leur dit: « Ils ont enlevé du sépulcre le Seigneur, et nous ne savons où ils l’ont mis. »
Kwa hiyo akakimbia mbio kwenda kwa Simon Petro na kwa yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, kisha akawaambia, “wamemchukua Bwana kaburini, nasi hatujui kule walikomlaza.”
3 Pierre sortit avec l’autre disciple, et ils allèrent au sépulcre.
Kisha Petro na yule mwanafunzi mwingine wakatoka, kuelekea kaburini.
4 Ils couraient tous deux ensemble, mais l’autre disciple courut plus vite que Pierre, et arriva le premier au sépulcre.
Wote walipiga mbio kwa pamoja; yule mwanafunzi mwingine alikimbia kwa kasi zaidi ya Petro nakufika kaburini wa kwanza.
5 Et s’étant penché, il aperçoit les linceuls posés à terre; mais il n’entra pas.
Akasimama na kisha kuangalia kaburini; akaiona ile sanda ya kitani imelala, lakini hakuingia ndani.
6 Simon-Pierre qui le suivait, arriva à son tour et entra dans le sépulcre; il vit les linges posés à terre,
Kisha Simon Petro naye akafika akaingia ndani ya Kaburi. Akaiona ile sanda ya kitani imelala pale
7 et le suaire qui couvrait la tête de Jésus, non pas posé avec les linges, mais roulé dans un autre endroit.
na ile leso iliyokuwa kichwani pake haikuwa imelala pamoja na zile sanda za kitani bali ilikuwa imelala pembeni peke yake.
8 Alors l’autre disciple qui était arrivé le premier au sépulcre, entra aussi; et il vit, et il crut:
Ndipo yule mwanafunzi mwingine naye alipoingia ndani ya kaburi; akaona na kuamini.
9 car ils ne comprenaient pas encore l’Écriture, d’après laquelle il devait ressusciter d’entre les morts.
Kwa kuwa hadi wakati huo walikuwa bado hawajayajua maandiko kwamba ilimlazimu Yesu afufuke tena katika wafu.
10 Les disciples s’en retournèrent donc chez eux.
Kisha wanafunzi wakaenda tena nyumbani kwao.
11 Cependant Marie se tenait près du sépulcre, en dehors, versant des larmes; et en pleurant elle se pencha vers le sépulcre;
Hata hivyo, Mariamu alikuwa amesimama kaburini akilia, alivyokuwa akiendelea kulia alisimama kisha akatazama kaburini.
12 et elle aperçoit deux anges vêtus de blanc, assis à la place où avait été mis le corps de Jésus, l’un à la tête, l’autre aux pieds.
Akaona malaika wawili wenye sura nyeupe wamekaa mmoja kichwani na mwingine miguuni mahali ambapo Yesu alikuwa amelala.
13 Et ceux-ci lui dirent: « Femme, pourquoi pleures-tu? » Elle leur dit: « Parce qu’ils ont enlevé mon Seigneur, et je ne sais où ils l’ont mis. »
Nao wakamwambia, “Mwanamke, kwa nini unalia?” Naye akawaambia, “Ni kwa sababu wamemchukua Bwana wangu, nami sijui walikomweka.”
14 Ayant dit ces mots, elle se retourna et aperçoit Jésus debout; et elle ne savait pas que c’était Jésus.
Alipokwisha sema hayo, aligeuka na kumwona Yesu akiwa amesimama. Lakini hakutambua kama huyo alikuwa Yesu.
15 Jésus lui dit: « Femme, pourquoi pleures-tu? Qui cherches-tu? » Elle, pensant que c’était le jardinier, lui dit: « Seigneur, si c’est toi qui l’avez emporté, dis-moi où tu l’as mis, et j’irai le prendre. »
Naye Yesu akamwambia, “Mama, kwa nini unalia? Unamtafuta nani?” Naye huku akidhani kuwa ni mtunza bustani akamwambia, “Bwana, kama ni wewe uliyemchukua, niambie ulikomweka, nami nitamchukua.”
16 Jésus lui dit: « Marie! » Elle se retourna et lui dit en hébreu: « Rabbouni! » c’est à dire Maître.
Yesu akamwambia, “Mariamu.” Naye akageuka mwenyewe na kumwambia kwa Kiaramu, “Raboni,” yaani hii ni kusema, “Mwalimu.”
17 Jésus lui dit: « Ne me touchez pas, car je ne suis pas encore remonté vers mon Père. Mais va à mes frères, et dis-leur: Je monte vers mon Père et votre Père, vers mon Dieu et votre Dieu. »
Yesu akamwambia, “Usiniguse, kwani bado sijapaa kwenda kwa baba; bali uende kwa ndugu zangu ukawaambie kuwa nitapaa kwenda kwa Baba yangu ambaye pia ni Baba yenu, Mungu wangu na Mungu wenu.”
18 Marie-Madeleine alla annoncer aux disciples qu’elle avait vu le Seigneur, et qu’il lui avait dit ces choses.
Mariamu Magdalena akaja kuwaambia wanafunzi, “Nimemwona Bwana,” na kwamba amemwambia mambo haya.
19 Le soir de ce même jour, le premier de la semaine, les portes du lieu où se trouvaient les disciples étant fermées, parce qu’ils craignaient les Juifs, Jésus vint, et se présentant au milieu d’eux, il leur dit: « Paix avec vous! »
Na ilipokuwa jioni, siku hiyo, siku ya kwanza ya juma, na milango ikiwa imefungwa mahali wanafunzi walipokuwapo kwa kuwahofia Wayahudi, Yesu alikuja na kusimama katikati yao na kuwaambia, “Amani iwe kwenu.”
20 Ayant ainsi parlé, il leur montra ses mains et son côté. Les disciples furent remplis de joie en voyant le Seigneur.
Alipokwisha sema haya akawaonesha mikono yake na ubavu wake. Nao wanafunzi walipomwona Bwana walifurahi.
21 Il leur dit une seconde fois: « Paix avec vous! Comme mon Père m’a envoyé, moi aussi je vous envoie. »
Kisha Yesu akawaambia tena, “Amani iwe nanyi. Kama vile Baba alivyonituma mimi, vivyo hivyo nami nawatuma ninyi.”
22 Après ces paroles, il souffla sur eux et leur dit: « Recevez l’Esprit-Saint.
Yesu alipokwisha sema hayo, akawavuvia akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu.
23 Ceux à qui vous remettrez les péchés, ils leur seront remis; et ceux à qui vous les retiendrez, ils leur seront retenus. »
Yeyote mmsameheye dhambi, wamesamehewa; na wale mtakaowafungia watafungiwa.”
24 Mais Thomas, l’un des douze, celui qu’on appelle Didyme, n’était pas avec eux lorsque Jésus vint.
Thomaso, mmoja wa wale kumi na wawili, aliyeitwa Didimas, hakuwa na wanafunzi wenzake Yesu alipokuja.
25 Les autres disciples lui dirent donc: « Nous avons vu le Seigneur. » Mais il leur dit: « Si je ne vois dans ses mains la marque des clous, et si je ne mets mon doigt à la place des clous, et ma main dans son côté, je ne croirai pas. »
Wale wanafunzi wengine waka mwambia baadaye, “Tumemwona Bwana.” Naye akawambia, “Kama sitaona alama za misumari katika mikono yake, na kuweka vidole vyangu kwenye hizo alama, na pia kuweka mkono wangu kwenye ubavu wake sitaamini.”
26 Huit jours après, les disciples étant encore dans le même lieu, et Thomas avec eux, Jésus vint, les portes étant fermées, et se tenant au milieu d’eux, il leur dit: « Paix avec vous! »
Baada ya siku nane wanafunzi walikuwa chumbani tena, naye Thomaso alikuwa pamoja nao. Wakati milango ilipokuwa imefungwa Yesu alisimama katikati yao. na akasema, “Amani na iwe nanyi.”
27 Puis il dit à Thomas: « Mets ici ton doigt, et regarde mes mains; approche aussi ta main, et mets-la dans mon côté; et ne sois pas incrédule, mais croyant. »
Kisha akamwambia Thomaso, leta kidole chako na uone mikono yangu; leta hapa mikono yako na uweke kwenye ubavu wangu; wala usiwe asiyeamini bali aaminiye.”
28 Thomas lui répondit: « Mon Seigneur, et mon Dieu! »
Naye Thomaso akajibu na kumwambia, “Bwana wangu na Mungu wangu.”
29 Jésus lui dit: « Parce que tu m’as vu, [Thomas, ] tu as cru. Heureux ceux qui n’ont pas vu et qui ont cru. »
Yesu akamwambia, Kwa kuwa umeniona, umeamini. Wamebarikiwa wao wanaoamini, pasipokuona.”
30 Jésus a fait encore, en présence de ses disciples, beaucoup d’autres signes qui ne sont pas écrits dans ce livre.
Kisha Yesu alifanya ishara nyingi mbele ya wanafunzi, ambazo hazijawahi kuandikwa katika kitabu hiki;
31 Mais ceux-ci ont été écrits, afin que vous croyiez que Jésus est le Christ, le Fils de Dieu, et qu’en croyant vous ayez la vie en son nom.
bali hizi zimeandikwa ili kwamba muweze kuamini kwamba Yesu ndiye Kristo, mwana wa Mungu, na kwamba muaminipo muwe na uzima katika jina lake.

< Jean 20 >